Skip to main content

Posts

Showing posts with the label HABARI

WAANDISHI WA HABARI VIJANA ZANZIBAR 'WASUKWA' KUZITAMBUA HABARI ZA UONGO.

NA, HASSAN MSELLEM – PEMBA Waandishi wahabari wachanga Visiwani Zanzibar wamepatiwa mafunzo ya kutambua taarifa sahihi katika kuelekea Uchanguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba 29. 2025. Akifungua mafunzo hayo kwa waandishi vijana kutoka Unguja na Pemba Mkurugenzi kutoka Muungano wa Klabu ya Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) Kenneth Simbaya katika Ukumbi wa Kituo cha Huduma za Sheria Kijangwani Mjini Unguja, amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwandaa Waandishi Habari vijana kutekeleza majukumu ya kihabari kwa weledi katika Dunia ya sasa yaliyotawaliwa na matumzi mabaya ya ‘AKILI UNDE’  Aidha Mkurugenzi huyo amewasisitiza waandishi hao umuhimu wa kujifunza matumizi sahihi ya ‘AKILI UNDE’ katika kuhakikisha taarifa zinazosambazwa mitandaoni kuelewa usahihi wake. “Ngudu waandishi kama munavyofahamu kuwa katika dunia ya leo tumegubikwa na matumizi mazuri na mabaya Artificial Intelligence (AKILI UNDE) hivyo lengo la mafunzo haya kwenu ni kuona ni kwa namna gani mutaweza kutamb...

"TUNAOMBA USALAMA WA WAANDISHI WA HABARI, WANAWAKE WAGOMBEA NA WASIMAMIZI WA UCHAGUZI" ZAMECO

NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA KAMATI ya Wataalamu wa Masuala ya Habari Zanzibar (ZAMECO) imeiomba Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) kushirikiana na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) kuhakikisha usalama wa Waandishi wa Habari, Wanawake wagombea, na Wasimamizi wa Uchaguzi (Mawakala) katika kipindi chote cha mchakato wa uchaguzi mkuu wa Zanzibar ambao utafanyika mwishoni mwa mwezi Oktoba mwaka huu. Kamati hiyo imesema inatambua kuwa mazingira salama kwenye masuala muhimu yenye maslahi mapana na mustakabali wa nchi hususan suala la uchaguzi, ni sharti la msingi ili kuhakikisha kila mdau anatekeleza majukumu yake kwa uhuru na bila ya hofu kama ilivyoelezwa katika Ibara ya 15(1) ya Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984: "(Kila mtu anastahiki kuheshimiwa na kupata hifadhi kwa nafsi yake, maisha yake binafsi na ya nyumbani kwake, na pia heshima, na hifadhi ya maskani yake na mmawasiliano yake)." Aidha Kamati imesisitiza kuzingatiwa hatua mahsusi kwa mujibu wa sheria na kanuni za kulind...

MWANAHABARI TEMMY MAHONDO AFARIKI DUNIA.

Mwanahabari Temigunga Mahondo amefariki Dunia Hospital ya Benjamin Mkapa Jijini Dodoma. Mahondo alikuwa mwandishi wa habari na meneja wa kituo kikongwe cha Radio cha Country Fm cha mkoani Iringa na baada ya hapo alifanya kazi na taasisi za kimataifa za kihabari kama mkufunzi kwa wabahabari. Mahondo pia amekuwa msaada mkubwa kwa chombo cha Matukio Daima Media kwani hadi mauti yanamkuta ndie alikuwa mkuu wa kitendo cha mafunzo ya kuwajengea uwezo waandishi katika Matukio Daima Media . Mahondo pindi alipolazwa Hospitali ya Mlonganzila wanakundi wa Iringa Daima ambako alikuwa ni mmoja wa waanzilishi wa kundi hilo ambalo Admin wake mkuu ni mkurugenzi wa Matukio Daima Media Francis Godwin walimchangia zaidi ya Tsh milioni 3 na yeye alitoa sehemu ya pesa hiyo kuchangia ujenzi wa ICU Hospital ya Rufaa ngazi ya mkoa ya Tosamaganga pesa alizokwenda kukabidhi mwenyewe na baadhi ya wanakundi huku akihamasisha jamii kuchangia zaidi. Siku nne kabla ya kifo chake uongozi wa Iringa Daima ulikwenda kum...

JUHUDI ZA WAANDISHI NA WADAU WA SHERIA ZA HABARI ZANZIBAR, ZAZAA MATUNDA-TAMWA,ZNZ.

NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA  Jumla ya makala 253, zinazohusu masuala ya uhuru wa habari Zanzibar zimeripotiwa na kuchapishwa kupitia magazeti, redio za kijamii na kitaifa pamoja na mitandao ya kijamii. Makala hizo zimeandikwa na waandishi wa habari 25 waliopata mafunzo maalum kutoka vyombo mbalimbali vya habari vya Unguja na Pemba. Hayo yameelezwa na Afisa Programu ya Mapitio ya sheria na uhuru wa habari kutoka TAMWA-ZNZ, Zaina Abdalla Mzee, wakati akiwasilisha ripoti ya utekelezaji wa programu hiyo. Katika wasilisho hilo Zaina alibainisha mafanikio yaliyopatikana, changamoto zilizojitokeza pamoja na mikakati ya baadaye kwa ajili ya kuendeleza juhudi za kulinda na kuimarisha uhuru wa habari visiwani Zanzibar. Zaina alibainisha kuwa juhudi za ushawishi na uchechemuzi zilizofanywa na wadau wa habari, wakiwemo Wajumbe wa Kamati ya Wataalamu wa Masuala ya Habari Zanzibar (ZAMECO), waandishi na wahariri habari, zimezaa matunda kwa kufanikisha kufanyika kwa mikutano mbalimbali na baadhi ya...

Upatikanaji wa Sheria Mpya ya Habari Zanzibar, bado Kitendawili.

 NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Afisa programu ya mapitio ya Sheria za Habari na Uhuru wa Habari na kujieleza kutoka Tamwa, Zanzibar Zaina Abdalla Mzee, amesema licha ya Wanaharakati, wadau na waandishi wa Habari Visiwani Zanzibar kupaza sauti juu ya kufanyiwa marekebisho Sheria za Habari suala ambalo bado halijafanyiwa kazi ipaswavyo ingawa Baraza la Wawakilishi limeahidi kulifanyia kazi suala hilo katika msimu ujao wa vikao vya Baraza hilo. Akiwasilisha ripoti kwa Waandishi wa Habari katika Ofisi za Tamwa Mkanjuni Pemba jana Tarehe 24\07\2025, ripoti yenye lengo la kuonesha hali halisi iliyofikiwa kwa kipindi cha miaka miwili ya utekelezaji wa mradi wa miaka miwili unaofadhiliwa na Shirika la #CommonWealth, ripoti iliyoonesha kuwepo kwa Sheria kandamizi kwa vyombo vya Habari, wanahabari na uhuru wa kujieleza kwa wananchi Visiwani Zanzibar. "Miongoni mwa matokeo (Outcomes) ya mradi huu ni pamoja na kuwajengea uwezo Waandishi wa Habari kuzitambua Sheria za Habari kuona mapungufu yali...

TAMWA ZNZ yataka adhabu kali kwa wahalifu wa Udhalilishaji kwa Watoto.

CHAMA cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania Zanzibar, (TAMWA ZNZ) kinawataka wasimamizi wa watoto kuzingatia haki za watoto kwa kuhakikisha wanalindwa na adhabu kali zinatolewa kwa wahalifu wa vitendo vya udhalilishaji kwa mujibu wa sheria. Ripoti iliyotolewa na Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali Zanzibar hivi karibuni inaonesha jumla ya matukio 165 ya ukatili wa kijinsia yaliripotiwa kwa mwezi Julai 2024, ambapo waathirika wengi walikuwa ni watoto. Ripoti inaonesha idadi ya watoto ni 142 sawa na asilimia 86.1 ya waathirika wote, ambapo wasichana walikuwa 115 sawa na asilimia 81.0 na wavulana 27 sawa na asilimia 19.0. Hali hii inasikitisha na inahitaji kudhibitiwa na wadau wote wakiwemo Serikali, taasisi za jamiidini, wazee, walimu na watoto wenyewe kupewa elimu ya kujilinda na kujikinga dhidi ya watu waovu. Wadau pia wanapaswa kuangalia upya ni kwa jinsi gani wanaweza kutatua changamoto zinazopelekea ongezeko la ukatili kwa watoto ambao ki msingi wanahitaji kulindwa kwa nguvu zot...

Waandishi wa habari wakumbushwa kuwa mashujaa upatikanaji Usawa wa kijinsia.

Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA-ZNZ) kimewataka waandishi wa habari vijana kuwa mashujaa na mabalozi wazuri wa kusaidia upatikanaji wa usawa wa kijinsia kwa maendeleo ya nchi. Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa chama hicho Dr. Mzuri Issa Ali wakati wa kufungua mafunzo ya siku tano ya kuendeleza waandishi wa habari vijana kuandika habari za uchambuzi juu ya wanawake na uongozi nchini. Amesema kwa awamu hii vijana wa kiume wamepewa nafasi kubwa ambapo awamu ya pili waandishi wa kiume walikuwa sita tu lakini awamu hii jumla yao ni 10 ambao watashiriki katika mafunzo kwa lengo la kuwaanda kuwa vijana bora na wa mfano katika kuelimisha jamii juu ya umuhimu wa wanawake kushiriki katika masuala ya uongozi. “Vijana wa kiume haikuwa bahati mbaya kuwachagua bali tumefanya hivyo kuwajenga kuwa mashujaa, mabalozi na wanaume wa mabadiliko katika kuhamasisha usawa wa kijinsia kwa jamii” Aidha Dr. Mzuri amaeongeza kuwa, tumechagua vijana wenye taaluma mbali mbali ikiwem...

"Waandishi tumieni kalamu zenu kusisitiza sheria mpya za Habari" Mjumbe wa Bodi Tamwa-ZNZ-Hawra Shamte

 NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Mjumbe wa bodi cha cha waandishi wa habari wanawake (Tamwa) Hawra Shamte aliwataka waandishi kuendelea kutumia kalamu zao kuhakikisha sheria ya habari rafiki zinapatikana. Ameyasema hayo katika kikao cha kutoa mrejesho wa kazi za mapitio ya sheria ya habari zenye vifungu vinavyo kinza uhuru wa habari zilizofanywa kwa mwaka mzima ambacho kimefanyika Tamwa Tunguu Unguja alisema tunategemea sheria zetu zitatoka kwa makatibu wakuu na kuacha kupigwa dana dana kutokana na ahadi tunazopewa kwa sheria zetu kuu mbili za habari ikiwa ni wakala wa usajili magazeti, na tume ya utangazaji kwa sababu tushazisemea sana na tunazidi kuziandikia hadi tuone mafanikio. Pia alisema kuna vyombo vya habari hawataki kusikia habari kuhusu sheria hizo lakini ipo haja ya kutumia vyombo vyengine ili kuweza kufikia lengo letu la kupata sheria mpya. Kwa upande wake Afisa mratibu wa sheria za habari Zaina Mzee alisema tunaenda mwaka wapili katika kuhamasisha upatikanaji wa s...

Uchechemuzi mapungufu Sheria za Habari kusaidia upatikanaji sheria mpya

IMEELEZWA juhudi za Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA ZNZ) kwa kushirikiana na wadau na waandishi wa habari Zanzibar kufanya ushawishi na utetezi wa mabadiliko ya sheria zenye vifungu vinavyokwaza uhuru wa habari zimesaidia kuweka matumaini ya baadhi ya sheria hizo kufanyiwa marekebisho. Hayo yameelezwa na wadau katika kikao cha tathimini ya utekelezaji wa programu ya uchechemuzi wa sheria za habari Zanzibar kilichowashirikisha waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali kisiwani Pemba. Zaina Mzee ambaye ni afisa programu hiyo kutoka TAMWA ZNZ, amesema program ya uchechemuzi wa mabadiliko ya sheria za habari zinazokwaza uhuru wa habari Zanzibar imeonyesha kuleta mabadiliko ya maboresho kwenye baadhi ya vifungu vya sheria za habari ambazo ni kandamizi. Alieleza, kupitia programu hiyo tayari TAMWA ZNZ kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo Kamati ya Wataalamu wa Masuala ya Habari Zanzibar ZAMECO wamefanya vikao na taasisi za serikali ambazo zinahusika...

Kamati ya kitaifa GEF yazitaka taasisi za uwezeshaji wananchi kiuchumi kuungana kutatua vikwazo ufikiaji Usawa Kiuchumi.

ZANZIBAR. KAMATI ya Kitaifa ya Ushauri kuhusu utekelezaji wa Programu ya Kizazi Chenye Usawa imezitaka taasisi zinazohusika na uwezeshaji wananchi kiuchumi kuweka mkakati wa kuungana kufanya kazi kwa pamoja ili kuzitaftia ufumbuzi changamoto zinazokwaza ufikiaji wa haki na usawa wa kiuchumi kwa wanawake. Wito huo umetolewa kufuatia ziara ya wajumbe wa kamati yenye lengo la kufuatilia utekelezaji wa Programu hiyo Zanzibar kubaini kuwepo kwa baadhi ya changamoto zinazowakwaza wanawake kupata haki na usawa wa kiuchumi. Makamo mwenyekiti wa kamati hiyo ambaye pia ni Naibu Spika wa Baraza la wawakilishi Zanzibar, Mhe. Mgeni Hassan alieleza licha ya wananchi hasa wanawake kuonesha utayari wa kujishughulisha na shughuli za kiuchumi hasa kilimo cha mwani lakini wanakabiliwa na vikwazo vingi vinavyowakatisha tamaa zaidi. Alibainisha kutokana na changamoto hizo kugusa sekta mbalimbali ni muhimu taasisi husika kama Wakala wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Zanzibar (ZEEA), Uchumi wa Buluu na nyingi...

Maumivu ya kukosa sheria mpya ya habari Zanzibar.

Na, Thuwaiba Habibu Raha na furaha ya safari ni kufika ulikokusudia kwa salama na amani. Baadhi ya safari huwa ngumi na huwa zenye maumivu na athari nyingi Miogoni mwa safari hizi ni ya waandishi wa habari kutaka kuwa na sheria zenye mazingira bora ya kazi zao. Kwa Takribani miaka 20 sasa waandishi na wadau wengine wa habari wamekuwa wakionyesha vifungu vya sheria ya habri vinavyominya uhuru wa habari na wa kujieleza. Lengo ni kutaka sheria rafiki itakayofanya mazingira ya kukusanya na kutoa habari Zanzibar kuwa rafiki na kuweza kuchangia vizuri maendeleo ya visiwa vya Unguja na Pemba. Lakini kelele hizo zimekuwa kama zile za msemo maarufu wa Kiswahili wa kelele za mpangaji hazimzuwii mwenye nyumba kulala. Zanzibar ilikuwa na historia nzuri na ya kuvutia ya habari na vijana wake kuchangia maendeleo ya sekta ya habri, hasa ya kufungua idhaa za Kiswahili katika nchi mbali mbali duniani. Kutoka zama hizo na hadi leo visiwa hivi vimetoa manguli wa taaluma ya habari kwa nyakati mbali mbal...

Kichanga chafariki kwa kukosa huduma ya OXYGEN Hospitali ya Chake Chake.

  Taarifa na Mwandishi Wetu. Inadaiwa taarifa za kichanga hicho kufariki dunia zilisambaa jana April 28, 2024 baada ya mama anayefahamika kwa jina la Saumu Hamduni Juma Mkaazi wa Michungwani Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, kujifungua watoto mapacha akiwa na ujauzito wa miezi sita katika hospitali ya Chake Chake na kusababisha hali za vichanga hivyo kuhitaji huduma ya dharura ya oksijini, ambayo ilikosekana katika hospitali hiyo.   Kwa mujibu wa Afisa Ustawi wa Wilaya ya Chake Chake, Afisa Ustawi wa Wilaya, Afisa Afya wa Wilaya ya Chake Chake Abdalla Haji Ali na Daktari Dhama wa Wilaya ya Chake Chake  (DMO) Sharif  Hamad Khatib a mbao walinukuliwa na afisa watu wenye ulemavu Wilaya ya Chake Chake Mwadini Juma  Ali alisema   “Nikweli jana majira ya mchana alifikishwa mama mjamzito katika Hospital ya Chake Chake na hatimaye kujifungua watoto wawili pacha ila mama huyo alijifungua akiwa bado muda wa kujifungua kitaalamu kufika ambapo ni mie...

Uzembe wa madereva wasababisha vifo vya watu 2 katika ajali mbili tofauti Pemba.

  Habari Na, Hassan Msellem-Pemba. Hassan Ali Hassan miaka 20, amefariki dunia baada ya gari aliokuwa amepanda aina ya Hino Lorry yenye namba ya usajili Z 572 ES iliokuwa ikiendeshwa na Ali Juma Hassan miaka 35, mkaazi wa Vitongoji kupata ajali katika eneo la Meli tano Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Akizungumza na Bahari fm Radio Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kusini Pemba Richard Mchomvu, alisema majira ya saa 8 mchana wakati gari hiyo ikitokea maeneo ya Ole kuelekea Ziwani ikiwa imebeba watu sita (6) ilipofika eneo la Meli Tano kutokana na mwendo kasi iliacha njia na kuelekea mabondeni kitendo kilichopelekea mtu mmoja kufariki dunia papo hapo na wengine wa tano kujeruhiwa. Aidha Kamanda Mchomvu aliwataja majeruhi hao kuwa ni Iddi Omar Mgunya mwenye umri wa miaka 35, mkaazi wa Vitongoji, Said Ali Said miaka 25, mshirazi wa Vitongoji, Khamis Ali Shaaban miaka 19 mkaazi wa Vitongoji, Nassor Said Khamis miaka15 mkaazi wa Vitongoji ambapo wamelekwa hospitali kwa ajili matibabu...

Jeshi la Polisi Mkoa wa Kusini Pemba likusanya Shillingi laki saba na eflu tisini na tano kutokana na faini za makosa ya usalama barabarani.

Habari Na, Hassan Msellem, Pemba Jeshi la Polisi Mkoa wa Kusini Pemba limekusanya Shillingi laki Saba na elfu tisini na tano kutoka tarehe 24\02\2022 hadi March 02\2022 kutokana na operesheni ya ukaguzi wa vyombo vya maringi mawili na Matatu yani Pikipiki na Bajaji ambapo Kwa kipindi hicho takriban vyombo 105 vilikamatwa Kwa makosa mbali mbali ikiwemo Madereva kutokuwa na leseni, uzembe, vyombo kukosa pasi nakadhalika ambapo Madereva 60 walifikishwa mahakamani na kutozwa faini. Hayo yamesemwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kusini Pemba Kamishna msaidizi wa Polisi Richard Tadeo Mchomvu wakati akizungumza na Waandishi wa Habari huko Ofisini kwake Madungu Chake Chake. Aidha Kamanda Richard ametoa wito waendeshaji wa vyombo vya Moto hususan madereva Bodaboda kuwa Makini na kufuata Sheria za Usalama Barabarani ili kuepukana na Ajali zisizo za lazima.