Skip to main content

Upatikanaji wa Sheria Mpya ya Habari Zanzibar, bado Kitendawili.

 NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA

Afisa programu ya mapitio ya Sheria za Habari na Uhuru wa Habari na kujieleza kutoka Tamwa, Zanzibar Zaina Abdalla Mzee, amesema licha ya Wanaharakati, wadau na waandishi wa Habari Visiwani Zanzibar kupaza sauti juu ya kufanyiwa marekebisho Sheria za Habari suala ambalo bado halijafanyiwa kazi ipaswavyo ingawa Baraza la Wawakilishi limeahidi kulifanyia kazi suala hilo katika msimu ujao wa vikao vya Baraza hilo.

Akiwasilisha ripoti kwa Waandishi wa Habari katika Ofisi za Tamwa Mkanjuni Pemba jana Tarehe 24\07\2025, ripoti yenye lengo la kuonesha hali halisi iliyofikiwa kwa kipindi cha miaka miwili ya utekelezaji wa mradi wa miaka miwili unaofadhiliwa na Shirika la #CommonWealth, ripoti iliyoonesha kuwepo kwa Sheria kandamizi kwa vyombo vya Habari, wanahabari na uhuru wa kujieleza kwa wananchi Visiwani Zanzibar.

"Miongoni mwa matokeo (Outcomes) ya mradi huu ni pamoja na kuwajengea uwezo Waandishi wa Habari kuzitambua Sheria za Habari kuona mapungufu yaliyomo katika Sheria hizo, kutoa mapendekezo ili ziweze kufanyiwa marekebisho" alisema 

"Kwa upande wa shughuli ambazo tumezifanya ni pamoja na kuandaa mikutano na wadau mbali mbali wa Habari kama vile watendaji wa Serikali na viongozi wa kisiasa hasa wale ambao tunawaona mara kwa mara wanazungumzia suala Uhuru wa Habari wakiwa katika vikao vya Baraza na mpaka Baraza la Wawakilishi linamaliza muda wake kuna ahadi kuwa katika vikao vijavyo vya Baraza hilo Sheria mpya ya Habari litajadiliwa ipaswavyo" alinena

Nae, Afisa Ufuatiliaji na Tathmini kutoka Tamwa, Zanzibar Mohammed Khatib Mohammed, amesema kuimarika kwa Uhuru wa Habari hutegemea na Sheria za Habari zilizo rafiki kwa Waandishi wa Habari katika utekelezaji wa majukumu yao.

Aidha amesema katika utekelezaji wa mradi huo wamegundua kuwa upatikanaji wa Sheria mpya za Habari sio jambo rahisi kutokana na Serikali kuchelea kufanyia kazi malalamiko ya wadau wa Habari na Waandishi wa Habari kuomba kufanyiwa marekebisho Sheria za Habari zinazowanyima Waandishi fursa ya kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi sambamba na Wananchi kupata fursa ya kutoa maoni.

"Kuimarika kwa Uhuru wa Habari inategemea na Sheria za habari iliyopo, kama Sheria ya Habari ni mzuri basi Uhuru wa Habari utakuwepo na kama ni mbaya Uhuru wa Habari hautokuwepo" aliongoza

Nao Waandishi walioshiriki katika mkutano huo ambao ni sehemu ya utekelezaji wa mradi, wamesema licha ya kuandika habari, makala na Vipindi mbali mbali vinavyohusu kupiga chapuo uhuru wa Habari, bado wanakumbana na changamoto ikiwemo vitosho, dharau pamoja na kukosa mashirikiano kwa baadhi ya watendaji wa Serikali wakati wanapohitaji taarifa katika Habari mbali mbali zenye kuleta maslahi kwa Wananchi na kuchochea uwajibikaji.

"Licha kuandika Habari, makala na kuandaa Vipindi mbali mbali vinavyopiga chapuo uhuru wa Habari na maoni kwa Wananchi bado Waandishi Habari Pemba tunakabiliwa na changamoto mbali mbali kutoka kwa baadhi ya watendaji wa Serikali kama vile wa wakuu wa Mikoa, Wilaya, Jeshi la Polisi, Maafisa wadhamini hali inayotufanya tushindwe kutekeleza majukumu yetu ya kihabari ipaswavyo" Mhariri wa Gazeti la Zanzibar Leo Bakari Mussa 


Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...