Skip to main content

Posts

Showing posts with the label MAZINGIRA

KAMATI ZA MAZINGIRA ZA SHEHIA ZAPIGWA MSASA MABADILIKO YA TABIA YA NCHI.

Kamati za mazingira za Shehia kisiwani Pemba zimetakiwa kuielimisha jamii juu ya masuala ya haki yanayotokana na tabia nchi ili kurekebisha athari za mabadiliko hayo. Hayo yameelezwa na Mkurugenzi mtendaji wa mwanvuli wa asasi za kiraiya Zanzibar Hassan Khamis Juma katika hafla ya kujengewa uwelewa wanakamati hao juu ya masuala ya haki yanayotokana na tabia nchi huko madungu chake chake Pemba.  Amesema ikiwa dunia ipo katika janga la mabadiliko ya tabia nchi ni vyema wananchi kwa kushirikiana na kamati kuchanganua haki zao ili kuweza kupata mbinu za kupunguza madhara yanayojitokeza  Kwa upande wake Mwalimu Khamis Mwalimu kutoka idara ya mazingira Pemba amesema ni vyema kamati za shehia kuitunza na kuilinda miundombinu iliyowekwa katika shehia zao ili kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi  Naibu katibu wa mwenvuli wa asasi za kiraiya Pemba Alawi Bakari amesema maeneo mengi Tanzania yameshaharibika kutokana na mabadiliko ya labia nchi hivyo ni vyema kushirik...

Kukosekana Udhamin ligi za wanawake wadumaza maendeleo ya michezo.

Na, Amina Mchezo. Udhamini ni chachu ya kulifanya jambo au shughuli Kwa urahisi na Kwa uhakika wa hali ya juu. Udhamini inategemea na namna ya makubaliano yenu haijalishi iwe fedha, ama bidhaaa au vifaa ilimradi unahakikisha unafanya jambo lako likiwa na usimamizi kamili. Udhamini katika michezo unatoa fursa na hamasa ya wachezaji kuona Wanapata heshima na kuwekewa sawa maslahi yao pamoja na clabu yao. Wadau mbalimbali wa michezo wamesema timu za wanawake hazina udhamini kutokana na kukosa mvuto  kutokana na wanawake wengi Kwa Zanzibar hawana mwamko wa kimichezo. Wameendelea kusema kuwa Kwa Zanzibar wanawake kucheza mpira imekuwa na mitazamo tofauti na ndio maana wadau wengi wanashindwa kuwekeza fedha zao katika timu au ligi za wanawake. Wakizungumza na mwandishi wa makala hii wadau hao wamesema udhamini wowote unatakiwa uwe na faida pia Kwa pande Zote huku mdhamini akitumainia kutangaza biashara, taasisi au kampuni yake. "Unajua Kila kitu ni mwamko wa watu uwanjani na ndio unaosa...

“Bado kuna pengo kubwa kwa Waandishi wa Habari kuandika Habari za mabadililo ya tabia ya Nchi na Usawa wa Kijinsi” Dr. Mzuri Issa Mkurugenzi Tamwa, Zanzibar

  Waandishi wa Habari Zanzibar wametakiwa kuongeza bidii katika kuandika Habari zinazohusu Usawa wa Kijinsia na Mabadiliko ya Tabia ya Nchi ili kuleta msukumo wa mabadiliko katika jamii na Taifa. Akizungumza na Waandishi wa Habari na wadau mbali mbali Mkutano wa Uchambuzi kwa vyombo vya Habari juu Usawa wa Kijinsia na Uongozi na Mabadiliko ya Tabia ya Nchi Mkurugenzi wa Tamwa Zanzibar Dr. Mzuri Issa, amesema tafiti zinaonesha bado kuna nafasi ndogo kwa vyombo vya Habari kuandika na kuripoti Habari za Usawa wa Kijinsia na Mabadiliko ya Tabia ya Nchi hali inayobabisha ufahamu mdogo wa jamii katika Nyanja hiyo.   “Utafiti unaonesha ushiriki wa Waandishi wa Habari kuandika Habari za usawa wa kijinsia na mabadiliko ya tabia ya nchi bado ni mdogo sana na badala yake waandishi wa Habari wanaelekeza zaidi macho yao kwenye Habari za udhalilishaji, michezo kiasi kwamba hata kwenye vyombo vyao Habari za usawa wa kijinsia na mabadiliko ya tabia ya nchi hazipewi kipaumbele” alisema...