Skip to main content

JUHUDI ZA WAANDISHI NA WADAU WA SHERIA ZA HABARI ZANZIBAR, ZAZAA MATUNDA-TAMWA,ZNZ.

NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA 


Jumla ya makala 253, zinazohusu masuala ya uhuru wa habari Zanzibar zimeripotiwa na kuchapishwa kupitia magazeti, redio za kijamii na kitaifa pamoja na mitandao ya kijamii. Makala hizo zimeandikwa na waandishi wa habari 25 waliopata mafunzo maalum kutoka vyombo mbalimbali vya habari vya Unguja na Pemba.

Hayo yameelezwa na Afisa Programu ya Mapitio ya sheria na uhuru wa habari kutoka TAMWA-ZNZ, Zaina Abdalla Mzee, wakati akiwasilisha ripoti ya utekelezaji wa programu hiyo. Katika wasilisho hilo Zaina alibainisha mafanikio yaliyopatikana, changamoto zilizojitokeza pamoja na mikakati ya baadaye kwa ajili ya kuendeleza juhudi za kulinda na kuimarisha uhuru wa habari visiwani Zanzibar.


Zaina alibainisha kuwa juhudi za ushawishi na uchechemuzi zilizofanywa na wadau wa habari, wakiwemo Wajumbe wa Kamati ya Wataalamu wa Masuala ya Habari Zanzibar (ZAMECO), waandishi na wahariri habari, zimezaa matunda kwa kufanikisha kufanyika kwa mikutano mbalimbali na baadhi ya wajumbe wa Baraza la Wawakilishi, Waziri wa Habari Zanzibar, maafisa wa serikali, pamoja na wakuu wa wilaya na mikoa ya Zanzibar.

Mikutano hiyo imelenga kujenga uelewa, kuhamasisha maboresho ya sheria za habari na kuimarisha mazingira ya kazi kwa wanahabari, ulinzi na usalama pamoja na kuimarisha uhuru wa kujieleza visiwani Zanzibar.

“Tunajivunia mafanikio na hatua kubwa tuliyopiga kupitia juhudi za uchechemuzi na ushawishi unaofanywa na waandishi wa habari pamoja na wadau wa sekta ya habari. Juhudi hizi zimeongeza uelewa wa wanahabari katika kutetea haki zao pamoja na haki za wananchi kwa ujumla,” alieleza Zaina. 

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa TAMWA ZNZ, Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Uchechemuzi TAMWA ZNZ, Bi. Shifaa Said Hassan, amewapongeza waandishi wa habari kwa kazi nzuri waliyoifanya katika kuendeleza uchechemuzi wa sheria mbalimbali zinazominya uhuru wa habari Zanzibar. 

“Ingawa programu hii inafikia tamati, waandishi wanaendelea na majukumu yao ya kila siku. Hivyo ni muhimu kuendeleza juhudi za uchechemuzi ili kuhakikisha sheria mpya na bora ya habari inapatikana ifikapo mwaka 2026,” alisisitiza Bi. Shifaa.


Washiriki wa mkutano huo pia walitoa maoni na mapendekezo ya kuboresha ripoti ya utekelezaji wa programu hiyo, huku wengi wakisisitiza umuhimu wa kuwa na sheria mpya ya habari itakayolinda uhuru wa vyombo vya habari, haki za waandishi, na uwajibikaji wa kitaaluma.

Aidha, baadhi ya waandishi walioshiriki walieleza kuwa programu hiyo imewasaidia kuchukua uamuzi wa kurejea vyuoni kwa ajili ya kujiendeleza kielimu, ili kuhakikisha kuwa wanakidhi vigezo vya kitaaluma na kuepuka kuzuiwa na masharti ya elimu iwapo sheria mpya itapitishwa.



Programu ya kupitia sheria za Habari Zanzibar (ARFEL) imetekelezwa na TAMWA-ZNZ kwa kipindi cha miaka miwili mfululizo kuanzia Ogasti 2023 hadi Julai 2025, yenye lengo la kusaidia na kuimarisha mapitio ya sheria za habari nan a kuimarisha huru wa kujieleza.



Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...