Skip to main content

"Waandishi tumieni kalamu zenu kusisitiza sheria mpya za Habari" Mjumbe wa Bodi Tamwa-ZNZ-Hawra Shamte

 NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA

Mjumbe wa bodi cha cha waandishi wa habari wanawake (Tamwa) Hawra Shamte aliwataka waandishi kuendelea kutumia kalamu zao kuhakikisha sheria ya habari rafiki zinapatikana.


Ameyasema hayo katika kikao cha kutoa mrejesho wa kazi za mapitio ya sheria ya habari zenye vifungu vinavyo kinza uhuru wa habari zilizofanywa kwa mwaka mzima ambacho kimefanyika Tamwa Tunguu Unguja alisema tunategemea sheria zetu zitatoka kwa makatibu wakuu na kuacha kupigwa dana dana kutokana na ahadi tunazopewa kwa sheria zetu kuu mbili za habari ikiwa ni wakala wa usajili magazeti, na tume ya utangazaji kwa sababu tushazisemea sana na tunazidi kuziandikia hadi tuone mafanikio.


Pia alisema kuna vyombo vya habari hawataki kusikia habari kuhusu sheria hizo lakini ipo haja ya kutumia vyombo vyengine ili kuweza kufikia lengo letu la kupata sheria mpya.


Kwa upande wake Afisa mratibu wa sheria za habari Zaina Mzee alisema tunaenda mwaka wapili katika kuhamasisha upatikanaji wa sheria mpya ya habari na tumefakiwa kwa kiasi kikubwa licha ya kuwa hatuja ipata sheria rafiki.


Tulishakutana na viongozi mbali mbali kujali jambo hili kwa jumla ya mikutano mitano ambayo ilifanywa na wadau wa habari (zameco) wakiwa na tume ya marekebisho ya sheria ,tume ya utangazi viongozi wa baraza la wawakilishi na viongozi wengine kujadili suala sheria za habari ambalo bado halija pata muwafaka.


Pia alisema tumeandaa mafunzo kwa waandishi wa habari kwa unguja na pemba lengo la kufanya kuhamishaji kuhusu sheria za habari na tulifanikisha hilo.


Waandishi waliopata mafunzo waliyafanyia kazi kwa kufika mpaka kwa wanasheria kutaka wapate ufafanuzi wa sheria na pia walipata nafasi ya kuwaelimisha wengine juu ya umuhimu wa kuwa na sheria za habari mpya.


Aidha alisema sheria ya habari iliyo rafiki pekee ndio inayoweza kuiheshimisha tasnia ya habari hivyo wadau wa habari wanapambana kuona inajitengemea na haingiliwi na mamlaka yoyote kwani kufanya hivyo kunakosesha uhuru wa kujieleza na kutoa taarifa.



Akiwasilisha mrejesho wa kazi kwa niaba ya afisa mfatiliaji na tathimini khairat Haji alieleza tumewapatia nafunzo waandishi 25 kutoka unguja na pemba ambao walifanikisha kuandika story 161 ambazo ziliwasilizwa katika vyombo tofauti ikiwemo radio, Tv,mitandao ya kijamii na magazeti Lengo ni kufanya uhamasishaji wa kupatiwa sheria mpya.


Wanahabari 25 waliopatiwa mafunzo 15 ni kutoka unguja na 10 ni pemba ambao walitumia elimu hiyo kuhakikisha taarifa walizotoa zinaelimisha umma juu ya kitu wanachokitaka.


Alieleza kuwa mrejesho unaonesha waandishi 15 kutoka unguja walipatiwa elimu hiyo 10 tu ndio walifanikiwa kutoa mrejesho wa kazi walizofanya ambazo ziliweza kuzua maoni tofauti katika vichwa vya watu.


Alisema katika hao 10 walitoa mrejesho wa kazi redio zilikuwa 2, television 4, magazeti 2 na mitandao ya kijamii 2 ambapo Tv ilitowa kazi 7 sawa aslimia 19% magazeti 5 kwa 16% mitandao ya kijamii 6 sawa16 % na radio 19 kwa 51%


Kwa upande wake muandishi mkongwe salim said salim aliwaomba waandishi kutokata tamaa na kuendelea kuandika na kusemezea sheria hizo mpaka kufikia malengo.


Pia alisema tunatakiwa kuandikia story/au makala zitakazo onesha mifano ya nchi waliofanikiwa kuwa na sheria a habari rafiki kama kenya na uganda ili kuleta hamasa zaidi ya kupatiwa sheria mpya.


Nao mwaandishi waliopatiwa mafunzo hayo Asia mwalim na Amrat kombo walisema tuendelee kuandika kwasababu lengo halija timia na sisi ndio wahanga tukipata sheria rafiki itakuwa rahisi kwetu kuweza kupata taarifa bila vikwazo.

Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...