Skip to main content

Posts

Mkurugenzi wa TAMWA–Zanzibar Dk. Mzuri Aaga Rasmi, Aweka Alama Kubwa ya Mageuzi ya Kijinsia.

HABARI, NA HASSAN MSELLEM. Baada ya zaidi ya miongo miwili ya kujitolea, uongozi na harakati za kutetea haki za wanawake, watoto na uhuru wa vyombo vya habari, Mkurugenzi wa Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania, Tawi la Zanzibar (TAMWA–ZNZ), Dk. Mzuri Issa Ali ameaga rasmi waandishi wa habari kutokana na kuondoka katika wadhifa wake, akiacha taasisi imara yenye mifumo thabiti na mafanikio yanayotambulika kitaifa na kimataifa. Akizungumza mbele ya waandishi wa habari, viongozi wa serikali, wadau wa maendeleo na wanachama wa TAMWA–ZNZ, Mkurugenzi huyo amesema waandishi wa habari ndio nguzo kuu ya taasisi hiyo licha ya changamoto kubwa wanazokumbana nazo lakini bado waliendelea kushirikiana na Tamwa Zanzibar katika kutumia kalamu zao kuelezea harakati za shughuli za Tamwa Zanzibar. “Kama kuna kundi la watu wanaojua kuuliza maswali magumu, kufuatilia ukweli bila kuchoka, na bado malipo yakawa madogo au hakuna kabisa, basi hao ni waandishi wa habari. Na cha kufurahisha zaidi, hao ndio ngu...
Recent posts

"ZAMECO" YASISITIZA KUWEPO KWA HAKI, UHURU WA KUTOA NA KUPATA TAARIFA.

HASSAN MSELLEM - PEMBA Kamati ya Wataalamu wa Masuala ya Habari Zanzibar (ZAMECO) inaungana na wanaharakati, wanahabari, na watetezi wa haki za binadamu duniani kote, kuadhimisha siku ya Haki za Binaadamu ambayo hufanyika kila ifikapo tarehe 10 Disemba ya kila mwaka.  Kaulimbiu ya mwaka huu, haki za binadamu kama “Mahitaji ya Kila Siku”, inasisitiza kuwa haki hizi lazima zilindwe bila kusuasua kila siku, kwa kila mtu, na katika kila mazingira. Katika maadhimisho ya mwaka 2025, ZAMECO inasisitiza kwamba uhuru wa kupata na kutoa taarifa ni nguzo muhimu ya utawala bora na msingi wa kulinda haki nyingine zote za binadamu.  Haki hii haipaswi kutazamwa kama ridhaa ya mamlaka bali kama wajibu wa kikatiba na kimataifa unaopaswa kuheshimiwa, kulindwa na kutekelezwa. Tunawakumbusha wadau wote kuwa tangu kupitishwa kwa Tamko la Ulimwengu la Haki za Binadamu (UDHR) mwaka 1948 uhuru wa kujieleza umeendelea kuwa nguzo muhimu katika kuhakikisha kwamba jamii inakuwa na nguvu ya kushiriki, ku...

"ZU" YAANDAA MAHAFALI YA 23, DISEMBA 17.2025.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA UONGOZI WA CHUO KIKUU CHA ZANZIBAR (ZU) UNAYOFURAHA KUWAALIKA WAHITIMU WOTE WA MWAKA WA MASOMO 2024/2025, PAMOJA NA WAZAZI, WALEZI, NDUGU, JAMAA, MARAFIKI, NA WADAU WOTE WA MAENDELEO YA ELIMU KUSHIRIKI KATIKA MAHAFALI YA 23 YA CHUO KIKUU CHA ZANZIBAR (ZU). MAHAFALI HAYO YANATARAJIWA KUFANYIKA SIKU YA JUMAATANO 17 MWEZI DISEMBA 2025, KATIKA KIWANJA CHA CHUO KIKUU TUNGUU KIBELE KUANZIA SAA MBILI ASUBUHI, AMBAPO MGENI RASMI KATIKA MAHAFALI HAYO ANATARAJIWA KUWA RAISI WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI DKT. HUSSEIN ALI MWINYI. UONGOZI WA CHUO UNAWASHAURI WAHITIMU WOTE KUKAMILISHA TARATIBU ZOTE IKIWA NI PAMOJA NA KUCHUKUWA MAJOHO KUANZIA SIKU YA ALHAMISI YA TAREHE 11 HADI TAREHE 15.  MAZOEZI YA MAHAFALI YANI REHASAL ITAFANYIKA TAREHE 16. WATU WOTE WANAKARIBISHWA KATIKA MAHAFALI HAYO. CHUO KIKUU CHA ZANZIBAR (ZU) NI CHEM CHEM YA MAADILI NA TAALUMA. KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NA SIMU NAMBARI  0714843480/0718321095/0778777878 AHSANTENI

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Ongezeko la Madiwani Wanawake Vijana 2025, Tumaini Jipya Wanawake kuwa Viongozi.

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA. Ongezeko la madiwani wanawake katika ngazi mbali mbali Mkoa wa Kusini Pemba limekuwa ishara ya mabadiliko ya kijamii, kiuchumi na kisiasa, pamoja na mwamko mpya wa jamii kutambua uwezo wa wanawake kama viongozi bora na chachu ya maendeleo. Miongoni mwa Madiwani Wanawake vijana waliopata fursa ya kuteuliwa kushika nafasi hizo na kuwawakilisha Wanawake wenzako vijana ni pamoja Amria Seif Saleh, ambaye ameteuliwa kuwa Diwani wa Baraza la Mji Mkoani na Fatma Khamis Ali, ambaye ni Diwani wa Wadi Kibokoni Vitongoji, wote wakiwa ni vijana chipukizi katika ulingo wa siasa na uongozi Kisiwani Pemba. Mabadiliko ya Kijamii na Kuongezeka kwa Uelewa k atika kipindi cha miaka ya karibuni, kumekuwa na kampeni mbalimbali zinazoendeshwa na mashirika ya kiraia, Serikali na taasisi binafsi zinazolenga kuongeza ushiriki wa wanawake katika uongozi, Elimu kwa jamii kuhusu umuhimu wa usawa wa kijinsia na nafasi ya mwanamke katika maamuzi imechangia kwa kiasi kikubwa kupungu...
AJISALIMISHA KITUO CHA POLISI KUDAI MTOTO WAKE ALIYEMTUPA. Novemba 15.2025 kipindi Cha Mawio kiliripoti tukio la mtoto mchanga wakike mweye umri wa wiki moja kutupwa huko Kitope ambapo aliyemtupa mtoto hakufahamika Hatimae Jana Novemba 21.2025 Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Tattu Mohamed mwenye umri wa miaka 26, mkaazi wa Mfenesini Unguja, Zanzibar amejisalimisha katika Kituo cha Polisi Mahonda kudai mtoto wake na kusema sababu zilizopelekea kumtupa mtoto wake ni tatizo la kupatwa na mashetani. Kamanda wa Polisi Kamishna Msaidizi wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Unguja Benedict Mapujila, amesema Mama huyo alikwenda kujisalimisha Kituo Cha Polisi Mahonda na kukiri kuwa yeye ndiye aliyemtupa mtoto huyo kutokana na kupatwa na matatizo ya mashetani ambaye ni mtoto wake Tatu ingawa alimzaa nje ya ndoa. Aidha Kamanda Mapujila, amesema kumtupa mtoto ni Kosa Kisheria hivyo Jeshi la Polisi litamshtaki Mama ili Sheria ifate mkondo wake na kutoa wito kwa jamii kutokufanya maamuzi ambayo yako kinyu...

PENYE NIA PANA NJIA: SAFARI YA KISIASA YA ZULEKHA ALI JUMA.

Na, Fatma Muhammed Suleiman, Unguja  Zulekha Ali Juma ni mama mwenye maono na dhamira ya kweli ya kutimiza ndoto zake. Alizaliwa mwaka 1971 visiwani Zanzibar, na safari yake ya elimu ilianza mwaka 1980 katika Skuli ya Haile Salasi Zanzibar, ambako alisoma darasa la kwanza hadi la nne. Aliendelea na masomo katika Skuli ya Konde, Micheweni Pemba, hadi kidato cha kwanza. Bi Zulekha alipendelea zaidi somo la siasa kwa sababu alikuwa na ndoto ya kuwa mwanasiasa, alipenda somo la historia na kujua asili ya nchi yake na maendeleo , na jiografia kwa shauku ya kutembelea maeneo mbalimbali. Akiwa skuli alikuwa kiongozi wa darasa ambapo pia alishiriki michezo mbalimbali. Alichagukliwa kuwa mwenyekiti wa chipukizi wa skuli na hatimae mwenyekiti wa chipukizi Mkoa wa Kaskazini Pemba. Ingawa alishindwa kuendelea na masomo kutokana na changamoto zilizo nje ya uwezo wake, hakukata tamaa ya kutimiza malengo yake. Ndoto yake ilitimia rasmi mwaka 1993 alipojiunga na chama cha CUF ambapo alipata nafa...