Habari Na, Hassan Msellem-Pemba.
Hassan Ali Hassan miaka 20, amefariki dunia baada ya gari aliokuwa amepanda aina ya Hino Lorry yenye namba ya usajili Z 572 ES iliokuwa ikiendeshwa na Ali Juma Hassan miaka 35, mkaazi wa Vitongoji kupata ajali katika eneo la Meli tano Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba.
Akizungumza na Bahari fm Radio Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kusini Pemba Richard Mchomvu, alisema majira ya saa 8 mchana wakati gari hiyo ikitokea maeneo ya Ole kuelekea Ziwani ikiwa imebeba watu sita (6) ilipofika eneo la Meli Tano kutokana na mwendo kasi iliacha njia na kuelekea mabondeni kitendo kilichopelekea mtu mmoja kufariki dunia papo hapo na wengine wa tano kujeruhiwa.
Aidha Kamanda Mchomvu aliwataja majeruhi hao kuwa ni Iddi Omar Mgunya mwenye umri wa miaka 35, mkaazi wa Vitongoji, Said Ali Said miaka 25, mshirazi wa Vitongoji, Khamis Ali Shaaban miaka 19 mkaazi wa Vitongoji, Nassor Said Khamis miaka15 mkaazi wa Vitongoji ambapo wamelekwa hospitali kwa ajili matibabu zaidi na afya zao zinaendelea vizuri.
Katika ajali nyengine kijana mmoja aliyefahamika kwa jina la Ayoub Hamad miaka 22, mkaazi wa Kwale Kisiwani Pemba amepoteza maisha baada ya gari alilokuwa amepanda kupata ajali eneo la Mtuhaliwa baada ya dereva wa gari hiyo ku-over take na kupelekea kugongana uso kwa uso na gari aina ya Carry jambo lililopelekea kijana huyo kupata majeraha maeneo ya kichgwani na kupelekea kupoteza maisha papo hapo.
Akisimulia kuhusu ajali hiyo Kamanda Mchomvu amesema gari hiyo ya abiria yenye namba ya usajili Z105 BL iliokuwa ikitokea Chake Chake kuelekea Mkoani alipofika maeneo ya Mtuhaliwa ili over take msafara wa gari zinazokwenda harusini na kusababisha kutokea kwa ajali hiyo.
Waliopata majeraha katika ajali hiyo ni Suleimana Nassor Shaib 23 mshirazi wa Chake Chake, Said Ali 25 mshirazi wa Ndagoni, Abas Issa 17, mshirazi wa Chake Chake, Hamad Seif 51 na Omar Ali 40 Msingini, amesema majeruhi wote wamefikishwa katika hospitali ya Abdalla Mzee kwa ajili ya kupatiwa matibabu.
"Ni kweli jana majira ya saa 2 asubuhi kijana hassan Ali Hassan miaka 20, amefariki dunia baada ya gari aliokuwa amepanda aina ya Hino Lorry yenye namba ya usajili Z 572 ES iliokuwa ikiendeshwa na Ali Juma Hassan miaka 35, mkaazi wa Vitongoji kupata ajali katika eneo la Meli tano Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba" alisema
Amesema ajali zote mbili zimesababishwa na uzembe wa madereva kwakutozingatia sheria ya usalama barabarani, hivyo basi amewaomba madereva kuwa makini pindi wanapokuwa barabarani na amesema endapo atatokea na dereva yeyote atakaevunja sheria za usalama barabarani hatua kali za kisheria zitakuchukuliwa dhidi yake ikiwemo kunyan’ganywa leseni.
Habari hii niliichapisha kwenye ukurasa wangu wa Facebook August 20, 2021 kwa ushahidi wa kiungo (link) hichi kabla ya kuanzisha blog ya Pemba Post Blog ambayo nimeichapisha habari hii.
Link of Facebook above👇
https://www.facebook.com/share/p/fvjr29RatJGi44LA/?mibextid=oFDknk
Xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
The carelessness of drivers caused the death of 2 people in two separate accidents in Pemba.
Written By, Hassan Msellem-Pemba.
A person known as Hassan Ali Hassan 20, died after the car he was riding in, a Hino Lorry with registration number Z 572 ES, which was driven by Ali Juma Hassan 35, a resident of Vitongoji, after having an accident in Meli tano area.
Speaking to Bahari fm Radio, South Pemba Regional Police Commander Richard Mchomvu said that at around 8 o'clock in the afternoon when the car was coming from Ole area towards Zwani carrying six (6) people, when it reached Meli five area due to high speed, it left the road and headed towards in the valleys, an act that led to the death of one person on the spot and the injury of five others.
In addition, Commander Mchomvu named the injured as Iddi Omar Mgunya, 35, a resident of Vitongoji, Said Ali Said, 25, resident of Vitongoji, Khamis Ali Shaaban, 19, a resident of Vitongoji, Nassor Said Khamis, 15, a resident of Vitongoji, where they were taken to hospital for further treatment and health they are doing well.
In another accident, a young man known as Ayoub Hamad, 22, a resident of Kwale Kisiwani Pemba, lost his life after the car he was riding in met with an accident in Mtuhaliwa area after the driver of the car went overboard and collided head-on with a Carry car. which led to the young man getting injuries in the groin areas and leading to the loss of life on the spot.
Speaking about the accident, Commander Mchomvu said that the passenger car with registration number Z105 BL was coming from Chake Chake towards the Region when he arrived at Mtuhaliwa to take over the convoy of cars going to the wedding and caused the accident.
Suleimana Nassor Shaib, 23, from Chake Chake, Said Ali, 25, from Ndagoni, Abas Issa, 17, from Chake Chake, Hamad Seif, 51, and Omar Ali, 40, were injured in the accident. for treatment.
He said that both accidents were caused by the negligence of the drivers for not following the road safety law, so he asked the drivers to be careful when they are on the road and he said that if he happens to any driver who breaks the road safety laws, strict legal measures will be taken against him, including the confiscation of his license.

Comments
Post a Comment