Skip to main content

Posts

Showing posts with the label UKATILI
AJISALIMISHA KITUO CHA POLISI KUDAI MTOTO WAKE ALIYEMTUPA. Novemba 15.2025 kipindi Cha Mawio kiliripoti tukio la mtoto mchanga wakike mweye umri wa wiki moja kutupwa huko Kitope ambapo aliyemtupa mtoto hakufahamika Hatimae Jana Novemba 21.2025 Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Tattu Mohamed mwenye umri wa miaka 26, mkaazi wa Mfenesini Unguja, Zanzibar amejisalimisha katika Kituo cha Polisi Mahonda kudai mtoto wake na kusema sababu zilizopelekea kumtupa mtoto wake ni tatizo la kupatwa na mashetani. Kamanda wa Polisi Kamishna Msaidizi wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Unguja Benedict Mapujila, amesema Mama huyo alikwenda kujisalimisha Kituo Cha Polisi Mahonda na kukiri kuwa yeye ndiye aliyemtupa mtoto huyo kutokana na kupatwa na matatizo ya mashetani ambaye ni mtoto wake Tatu ingawa alimzaa nje ya ndoa. Aidha Kamanda Mapujila, amesema kumtupa mtoto ni Kosa Kisheria hivyo Jeshi la Polisi litamshtaki Mama ili Sheria ifate mkondo wake na kutoa wito kwa jamii kutokufanya maamuzi ambayo yako kinyu...

Mwezi mmoja matukio 106, ya Ukatili na Udhalilishaji Zanzibar, Magharabi ‘B’ yaongoza.

Na, Hassan Msellem, Pemba Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali Zanzibar (OCGS) imetoa takwimu za matukio ya ukatili na udhalilishaji wa kijinsia Zanzibar katoka mwezi Agosti na Septemba 2025, ambapo jumla ya matukio 106 ya ukatili na udhalilishaji wa kijinsia yameripotiwa katika vituo mbali mbali vya Polisi huku Wilaya ya Magharib ‘B’ Unguja kwa kuwa jumla ya matukio 17 sawa na asilimia 16.0 Akitoa takwimu hizo kwa waandishi wa Habari, waratibu wa madawati ya jinsia na wadau wengine Oktoba 22.2025 huko Gombani Pemba Mkurugenzi wa Idara ya Takwimu za Kijamii kutoka Ofisi ya mtakwimu Mkuu Zanzibar Sabina Raphael Daima, amesema jumla ya matukio ya ukatili na udhalilishaji wa kijinsia 106 yameripotiwa mwezi Septemba 2025, ambapo waathirika wakubwa wakiwa ni watoto sawa asilimia 88.7 na wanawake wakiwa asilimia 11. 3 Aidha amesema kuwa miongoni mwa waathrika wa matukio hayo 94, wasichana 82 sawa asilimia 77.4 wavulana 12 sawa na asilimia 10.3 “Takwimu hizi zinaonesha matukio ya ukatili na udh...

JELA MIAKA 106, KWA MAKOSA NANE YA UDHALILISHAJI.

HASSAN MSELLEM, PEMBA Abdalla Rashid Hassan (Mgunya) mwenye umri wa miaka 30 mkaazi wa Ziwani Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba amehukumiwa kwenda chuo cha mafunzo (JELA) kwa muda wa miaka 30 kwa Kutenda makosa nane ya udhalilishaji yakiwemo ya kutorosha, shambulio la aibu na kubaka. MAKOSA MATANO YA KUTOROSHA Mbele ya hakimu wa mahakama ya kupambana na makosa ya udhalilishaji Mkoa wa Kusini Pemba Chake Chake Taki Abdalla Habib imeelezwa na mwendesha mashtaka Othman Mzori kuwa tarehe 3\01\2025 saa 8:30 za mchana huko bonde la Mjananza Ziwani Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba mshtakiwa aliwachukua watoto watano wenye umri kati ya miaka 7, 9, 11, 12 na kuwapeleka maporini katika bonde la Sinanga Ziwani, jambo ambalo ni kosa kisheria kinyume na kifungu cha 113 kifungu kidogo cha kwanza (a) Sheria nambari 6 ya mwaka 2018 Sheria ya Zanzibar. KOSA LA SITA Shambulio la kawaida Tarehe 3\01\2025 saa 9:25 za jioni huko Sininga Ziwani Wilaya ya Chakwe Chake Mkoa wa Kusini Pemba ...

Mama ajifungua kisha kukiua kichanga na kukifukia kwenye tuta- Sizini Pemba

 Habari Na, Hassan Msellem, Pemba  Picha kutoka Maktaba. Mchanga Omar Said anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 35, na mama wa watoto saba Mkaazi wa Shehia ya Sizini Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba, anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kumuua na kisha kumfukia kwenye tuta mtoto wake Mchanga. Akizungumza juu ya tukio Hilo Mkuu wa Wilaya ya Micheweni Mgeni Khatib Yahya, alisema majira ya saa 5 siku ya Tarehe 18\05\2024 wamepokea taarifa za mama huyo akiwa na ujauzito ambalo alijifungua bila ya taarifa za alichojifungua kuonekana, ndipo Wananchi walipofuatilia na kugundua kuwa mama huyo alijifungua na kisha kumuua mtoto na kisha kukizika. Akizungumza kwa niaba ya mganga Mkuu wa hospital ya Micheweni Daudi Rashid Mkasha, alisema walipofika eneo la tukio walikuta sehemu iliyochumbuliwa na kukuta mabaki ya mwili wa mtoto ambayo tayari yameshaharibika. Suleiman Shaame Hamad, ni Sheha wa Sizini alikiri kutokea kwa tukio hilo na kuhuzunishwa nalo pamoja na kuwataka ...