Skip to main content

Posts

Showing posts with the label UCHAGUZI

RAHIMA SAID ABDALLAH: MWANAMKE JASIRI ANAYEVUNJA VIKWAZO VYA UONGOZI.

Makala Na Fatma M. Suleiman, Unguja “Sijatokea kwenye familia yenye uzoefu wa kisiasa, nimepata hamasa kuionyesha jamii mwanamke anaweza kuwa kiongozi na kutatua changamoto za jamii Mwanamke ni mlezi, mbunifu na mwenye fikra pevu, kwa hiyo hakuna sababu ya kunizuia kuingia kwenye uongozi wa kisiasa.”  Kauli hii inaakisi Taarifa ya Baraza la Taifa la Wanawake, Tanzania, 2023 inayoeleza kwamba “Kuhakikisha usawa wa kijinsia katika uongozi si chaguo, bali ni wajibu wa kijamii.”  Rahima Said Abdallah ni mfano wa mwanamke jasiri aliyevunja vikwazo vya kijamii na kugombea nafasi ya uwakilishi kupitia Chama cha Ukombozi wa umma (CHAUMMA) Jimbo la Mwanakwerekwe katika Uchaguzi Mkuu wa 2025. Rahima ana miaka 26 amethibitisha kuwa uongozi haujali jinsia, bali ni uwezo, bidii na dhamira ya kweli ya kuwatumikia watu. Kupitia safari yake, amekuwa kielelezo cha matumaini mapya kwa wanawake na vijana wanaotamani kushiriki katika uongozi wa kisiasa nchini. Rahima alizaliwa mwaka 1...

'Ongezeko la viongozi wanawake kwenye vyombo vya maamuzi, chachu ya maendeleo Zanzibar.

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM- PEMBA   Ni miaka mingi sana vyombo vya maamuzi nchini Tanzania vimekuwa vimehodhiwa na wanaume kwa asilimia kubwa kutokana na wanawake kukosa muamko na kunyimwa fursa ya kugombea nafasi za uongozi katika vyama vyao vya siasa licha ya kuwa wao ndio wafuasi wakubwa wa vyama hivyo. Lakini kuanzishwa kwa miradi mbali mbali yenye lengo la kuwawezesha wanawake kushiriki katika haki yao ya siasa na uongozi ikiwemo mradi wa uhamasishaji wanawake kushiriki katika nafasi za uongozi (SWIL) kumeongeza muamko na hamasa ya wanawake kujiunga na vyama vya siasa pamoja na kugombea nafasi mbali mbali za uongozi kama vile udiwani, uwakilishi, ubunge na hata uraisi. Hilo linadhihiri kuelekea Uchaguzi Mkuu Oktoba 29.2025 ambapo kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Chama cha Waandishi wa habari Tanzania Tamwa, Zanzibar Agosti 20.2025 imeeleza kuwa jumla ya wanawake 13 nchini kutoka vyama mbali mbali vya siasa wamegombea nafasi ya uraisi na umakamu wa rais...

MKUNGA HAMAD SADALA – CHACHU YA WANAWAKE KUWA VIONGOZI.

NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Msemo unaosema hata “Mbuyu Ulianza Kama Mchicha” umesadifu kwa Makamo Mwenyekiti wa Mkutano Mkuu Taifa na Mjumbe wa halmashauri Kuu ya ACT Wazalendo Mkunga Hamad Sadala Mkaazi wa Vitongoji Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba ambaye pia ni Mama wa Watoto tisa. Bi. Mkunga alianza kujitumbukiza kwenye dimbwi la siasa mwaka 1992 wakati ambao mfumo wa vyama vingi Nchini Tanzania ndio kwanza unaanza kwa kujiunga na Chama Civil United Front (CUF) na safari ya Bi. Mkunga kisiasa ikaanzia hapo akiwa na umri mdogo huku akiwa mtumishi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kada ya ualimu katika Skuli ya msingi iliopo Vitongoji na kukumbana na dhoruba kali ya kimbunga cha kujiunga na Siasa ya upinzani ambayo ilikuwa ni mwiko kwa watumishi wa umma ambayo ilitamalaki zaidi Kisiwani Pemba kwa kipindi hicho. Lakini moyo wa uzalendo na ujasiri ulimsukuma kuruka vihunzi hivyo na sasa kuwa mwanamke wa kupigiwa mfano Visiwani Zanzibar. Bi. Mkunga Hamad Sadala, mjumbe ...

Rushwa ya ngono, ukosefu wa fedha vikwazo kwa Wanawake kutimiza ndoto zao za kuwa Viongozi

NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA KATIBA ZA VYAMA Katiba za vyama vingi vya Siasa nchini zimezingatia usawa wa Kijinsia katika Uongozi ndani na nje ili kuwepo kwa usawa katika vyama hivyo. Katiba ya Chama cha Mapinduzi CCM, Sura ya Pili Fungu la Pili ibara ya 16 inasema “Kiongozi wa CCM ni kila Mwanachama mwenye dhamana yoyote katika CCM aliyechaguliwa au kuteuliwa kwa mujibu wa Katiba. Ibara ya 17 inaeleza sifa za kiongozi ni pamoja na kutosheka na asiwe mtu aliyetawaliwa na tamaa.  Katiba ya Chama cha Alliance for Change and Transparency - ACT Wazalendo SEHEMU YA PILI, imeeleza Sifa za kuwa kiongozi katika Chama hicho ikiwemo “kuwa na mwenendo mzuri na Maadili ya Viongozi” Lakini licha ya haki ya Usawa wa Kijinsia iliyotolewa na Katiba za vyama Siasa bado Wanawake wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa fedha kuanzia fedha za kuchulia fomu pamoja na kampeni, hali inayosababisha Wanawake wengi kushindwa njia kugombea nafasi za Uongozi kupitia vyama vyao. WANAWAKE WALIOWAHI KUGOMBEA Mgomb...

WILAYA YA MKOANI YAFANYA KONGAMANO LA "AMANI" KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2025.

NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Mkuu wa Wilaya ya Mkoani Miza Hassan Faki, akimkabidhi Nishani Makamo wa Pili wa Rais Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla Viongozi wa vyama vya Siasa wametakiwa kutotumia hotuba zinazochochea Ubaguzi, Chuki na Uhasama katika kampeni zinazotarajiwa kufanyika hivi punde Visiwani Zanzibar ili kuepukana na uvunjifu wa amani. Akifungua Kongamano lililoandaliwa na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Mkoani huko katika Ukumbi wa Umoja ni Nguvu Mkoani, Makamo wa Pili wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla, amesema lengo la Kampeni za Kisiasa ni wagombea kunadai sera na ilani za vyama vyao kwa wananchi ili waweze kuwachagua na sio kutoa hotuba za Ubaguzi, Chuki na Uhasama hali inayoweza kusababisha uvunjifu wa amani nchini. Aidha Mhe. Hemed amewasihi Vijana kutokutumiwa vibaya na wasiasa kwa kisingizio cha Uchaguzi kwani wao ndio wahanga wakubwa vitendo vya uvunjifu wa amani katika kipindi cha Uchaguzi. “Niwaombe sana viongozi wa vyama vya siasa na wagom...

WAANDISHI WA HABARI PEMBA WABEBESHWA ZIGO LA “AMANI” KUELEKEA UCHAGUZI MKUU WA 2025.

NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Waandishi wa Habari Kisiwani Pemba wametakiwa kuzingatia weledi, maadili na taaluma ya Habari katika kuandika na kuripoti taarifa zinazochochea amani na utulivu nchini. Akizungumza na Waandishi hao katika Ukumbu wa Baraza la Mji Chake Chake Afisa mdhamini Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo Mfamau Lali Mfamau katika Kongamano la Kuimarisha Amani kati ya Jeshi Polisi na Vyombo vya habari kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025, amesema waandishi walioshiriki katika Kongamano hilo wanapaswa kuzingatia maelekelezo waliyopatiwa katika kipindi cha Uchaguzi. Aidha Afisa huyo ameliomba Jeshi la Polisi kuwashughulikia Waandishi watakaokiuka maelekezo yaliyotolewa kwenye Kongamono ili iwe mfano kwa waandishi wengine. “Kwa habati mzuri hapa munazungumza Kiswahili kimoja lakini mukikutana fild (eneo la kazi) katika wale watu ambao mumewapa maelekezo halafu mukaja kugundua wale watu wambao tumekaa tumedicuss nao haya mambo umuhimu wa amani kuelekea katika kipindi cha Uchag...

"TUNAOMBA USALAMA WA WAANDISHI WA HABARI, WANAWAKE WAGOMBEA NA WASIMAMIZI WA UCHAGUZI" ZAMECO

NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA KAMATI ya Wataalamu wa Masuala ya Habari Zanzibar (ZAMECO) imeiomba Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) kushirikiana na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) kuhakikisha usalama wa Waandishi wa Habari, Wanawake wagombea, na Wasimamizi wa Uchaguzi (Mawakala) katika kipindi chote cha mchakato wa uchaguzi mkuu wa Zanzibar ambao utafanyika mwishoni mwa mwezi Oktoba mwaka huu. Kamati hiyo imesema inatambua kuwa mazingira salama kwenye masuala muhimu yenye maslahi mapana na mustakabali wa nchi hususan suala la uchaguzi, ni sharti la msingi ili kuhakikisha kila mdau anatekeleza majukumu yake kwa uhuru na bila ya hofu kama ilivyoelezwa katika Ibara ya 15(1) ya Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984: "(Kila mtu anastahiki kuheshimiwa na kupata hifadhi kwa nafsi yake, maisha yake binafsi na ya nyumbani kwake, na pia heshima, na hifadhi ya maskani yake na mmawasiliano yake)." Aidha Kamati imesisitiza kuzingatiwa hatua mahsusi kwa mujibu wa sheria na kanuni za kulind...