NA, HASSAN MSELLEM – PEMBA
Waandishi wahabari wachanga Visiwani Zanzibar wamepatiwa mafunzo ya kutambua taarifa sahihi katika kuelekea Uchanguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba 29. 2025.
Akifungua mafunzo hayo kwa waandishi vijana kutoka Unguja na Pemba Mkurugenzi kutoka Muungano wa Klabu ya Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) Kenneth Simbaya katika Ukumbi wa Kituo cha Huduma za Sheria Kijangwani Mjini Unguja, amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwandaa Waandishi Habari vijana kutekeleza majukumu ya kihabari kwa weledi katika Dunia ya sasa yaliyotawaliwa na matumzi mabaya ya ‘AKILI UNDE’
Aidha Mkurugenzi huyo amewasisitiza waandishi hao umuhimu wa kujifunza matumizi sahihi ya ‘AKILI UNDE’ katika kuhakikisha taarifa zinazosambazwa mitandaoni kuelewa usahihi wake.
“Ngudu waandishi kama munavyofahamu kuwa katika dunia ya leo tumegubikwa na matumizi mazuri na mabaya Artificial Intelligence (AKILI UNDE) hivyo lengo la mafunzo haya kwenu ni kuona ni kwa namna gani mutaweza kutambua kati ya taarifa sahihi na zisizosahihi kupitia njia mbali mbali” Mkurugenzi kutoka Muungano wa Klabu ya Waandishi wa Habari Tanzania
“Kuna njia nyingi zinazoweza kuwasaidia katika kuzitambua taarifa za uongo na upotoshaji iwe maelezo, picha au hata video unaweza kuingiza sehemu ya maudhui hayo kwenye programu kama vile Google lens, Google Earth, True Caller nakdhalika na ukaweza kupata usahihi wa taarifa hizo” Mkufunzi wa masuala ya Digitali Ephraim Muchemi
Kwa upande wake, Afisa programu kutoka Muungano wa Klabu ya Waandishi Tanzania Andrew Marawiti, amewataka waandishi hao kuendelea kuyafanyia mafunzo kwa vitendo mafunzo hayo ili yaweze kuleta tija kwao na kwao na taifa kwa ujumla
“Kuwa kwenu hapa leo haikuwa Bahati mbaya tambueni kuwa mulikuwa wengi sana kwenye maombi ila nyinyi ndio tumeona munafaa zaidi kutokana na maelezo yenu kwenye maombi hivyo basi tunawaomba sana mukaendelee kuyatumia mafunzo haya kwa vitendo ili yaweze kuwajenga zaidi” amesisitiza
Akifunga mafunzo hayo Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Zanzibar (ZPC) Abdalla Mfaume, amesema katika zama hizi za maendeleo ya Sayansi na Teknolojia kumekuwa na ongezeko la ahabari za uongo na upotoshaji, hivyo amewaomba waandishi hao kuyafanyia kazi mafunzo hayo hususan katika kipindi hichi cha kabla na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29.2025
“Katika kipindi hichi cha maendeleo ya sayansi na teknolojia changamoto za Habari za upotoshaji na uongo zimekuwa nyingi sana hivyo jukumu lenu ni kuhakikisha munazitambua taarifa hizo ili zisiweze kuleta athari kwenu na taifa kwa ujumla” Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Zanzibar (ZPC) Abdalla Mfaume
Baadhi ya Waandishi hao wamepata nafasi ya kutoa neno ikiwemo kuushukuru Muungano wa Klabu ya Waandishi wa Habari Tanzania kwa kuwapatia mafunzo hayo na kuahidi kuendelea kuyafanyia kazi hususan katika kipindi cha kuelekea Uchaguzi Mkuu.
"Kwanza nianze kwa kuwashukuru UTPC kwa mafunzo haya adhimu kwetu maana kwakweli mitandaoni hali sio shwari na sisi Waandishi ndio wahanga wa kubwa taarifa za uongo na upotoshaji kwa maana ya kutumia taarifa hizo" Salma Shaali Juma mwandishi kutoka Idara ya Uvuvi Zanzibar na Habari FM Radio
Mafunzo hayo ya siku moja yalisyoshirikisha waandishi wa Habari Vijana kutoka Kisiwani Unguja na Pemba yameandaliwa na Muungano wa Klabu ya Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) kwa ufadhili wa Netherlands (NL)








Comments
Post a Comment