Skip to main content

TAMWA ZNZ yataka adhabu kali kwa wahalifu wa Udhalilishaji kwa Watoto.

CHAMA cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania Zanzibar, (TAMWA ZNZ) kinawataka wasimamizi wa watoto kuzingatia haki za watoto kwa kuhakikisha wanalindwa na adhabu kali zinatolewa kwa wahalifu wa vitendo vya udhalilishaji kwa mujibu wa sheria.


Ripoti iliyotolewa na Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali Zanzibar hivi karibuni inaonesha jumla ya matukio 165 ya ukatili wa kijinsia yaliripotiwa kwa mwezi Julai 2024, ambapo waathirika wengi walikuwa ni watoto. Ripoti inaonesha idadi ya watoto ni 142 sawa na asilimia 86.1 ya waathirika wote, ambapo wasichana walikuwa 115 sawa na asilimia 81.0 na wavulana 27 sawa na asilimia 19.0.


Hali hii inasikitisha na inahitaji kudhibitiwa na wadau wote wakiwemo Serikali, taasisi za jamiidini, wazee, walimu na watoto wenyewe kupewa elimu ya kujilinda na kujikinga dhidi ya watu waovu.


Wadau pia wanapaswa kuangalia upya ni kwa jinsi gani wanaweza kutatua changamoto zinazopelekea ongezeko la ukatili kwa watoto ambao ki msingi wanahitaji kulindwa kwa nguvu zote. Sheria ya Mtoto ya Zanzibar Na 6 ya mwaka 2011 inapinga udhalilishaji wa watoto wa aina yoyote ile ili kukuza ustawi wa watoto.


Aidha Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Watoto (UNCRC) ya mwaka 1989 ambao umeridhiwa na nchi ya Tanzania ikiwemo Zanzibar unasisitiza kudumisha haki za mtoto ikiwemo ulinzi jambo linalopelekea kujenga jamii na Taifa lenye raia wenye kuheshimiana.


Hivi karibuni, tulishuhudia udhalilishaji wa watoto wasio na hatia uliofanywa na watendaji wa Manispaa ya Magharibi ‘A’, kwa kumkamata mtoto wa miaka miwili (2) na kumchukua pamoja na mlezi wake kwa kisingizio cha wazazi wa mtoto huyo kutolipa ada ya usafi, wakati wazazi wakiwa katika majukumu yao ya kikazi.


Jambo hili lilizua taharuki kwa familia ya mtoto huyo na jamii kwa ujumla, kwa vile ni kitendo kinachokwenda kinyume na haki za mtoto pamoja na haki za binaadamu. Kwa muktadha huo, TAMWA ZNZ inakemea vitendo vya ukatili na udhalilishaji dhidi ya watoto na inataka hatua kali zichukuliwe dhidi ya wale wote wanaokwenda kinyume na sheria.


Tunatoa wito kwa jamii kuwalinda watoto wetu na kuhakikisha hawakumbwi na vitendo vya udhalilishaji.


Imetolewa na kitengo cha Habari na Mawasiliano, TAMWA ZNZ.

Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...