Skip to main content

Waandishi wa habari wakumbushwa kuwa mashujaa upatikanaji Usawa wa kijinsia.

Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA-ZNZ) kimewataka waandishi wa habari vijana kuwa mashujaa na mabalozi wazuri wa kusaidia upatikanaji wa usawa wa kijinsia kwa maendeleo ya nchi.


Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa chama hicho Dr. Mzuri Issa Ali wakati wa kufungua mafunzo ya siku tano ya kuendeleza waandishi wa habari vijana kuandika habari za uchambuzi juu ya wanawake na uongozi nchini.


Amesema kwa awamu hii vijana wa kiume wamepewa nafasi kubwa ambapo awamu ya pili waandishi wa kiume walikuwa sita tu lakini awamu hii jumla yao ni 10 ambao watashiriki katika mafunzo kwa lengo la kuwaanda kuwa vijana bora na wa mfano katika kuelimisha jamii juu ya umuhimu wa wanawake kushiriki katika masuala ya uongozi.


“Vijana wa kiume haikuwa bahati mbaya kuwachagua bali tumefanya hivyo kuwajenga kuwa mashujaa, mabalozi na wanaume wa mabadiliko katika kuhamasisha usawa wa kijinsia kwa jamii”


Aidha Dr. Mzuri amaeongeza kuwa, tumechagua vijana wenye taaluma mbali mbali ikiwemo uandishi wa habari, waandaaji na waongozaji wa filamu ambao tunaamini watasaidia kuelimisha jamii masuala ya usawa wa kijinsia na wanawake kushiriki katika vyombo vya maamuzi.


Sambamba na hayo Mkurugenzi huyo amesema, lengo ni kuona ongezeko kubwa la ushiriki wa wanawake kugombea nafasi za uongozi kupitia mipango kazi itakayoandaliwa na vijana hao ambayo itazingatia uchambuzi wa takwimu na maazimio ya nchi yetu yenye kuridhia agenda ya dunia ya kufikia usawa wa 50% kwa 50%.


Nae Msanii na balozi wa habari Zanzibar Mustafa Yussuf, amewaomba baadhi ya wanaume kuondosha dhana potofu kwa wanawake katika uongozi na badala yake kuwasimamia ili kutimiza ndoto zao.


“Tumeona idadi ya wanawake viongozi inaongezeka, na ni waaminifu katika utendaji wao hata katika jamii ukilinganisha na wanaume," Mustafa alieleza.


Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA-ZNZ) imeandaa mafunzo kwa waandishi vijana 25 Unguja na Pemba ambapo wanawake jumla ni 15 na wanaume 10 kwa kushirikiana na Shirika (NED) la nchini Marekani.


 

Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...