Skip to main content

Maumivu ya kukosa sheria mpya ya habari Zanzibar.

Na, Thuwaiba Habibu



Raha na furaha ya safari ni kufika ulikokusudia kwa salama na amani.

Baadhi ya safari huwa ngumi na huwa zenye maumivu na athari nyingi

Miogoni mwa safari hizi ni ya waandishi wa habari kutaka kuwa na sheria zenye mazingira bora ya kazi zao.

Kwa Takribani miaka 20 sasa waandishi na wadau wengine wa habari wamekuwa wakionyesha vifungu vya sheria ya habri vinavyominya uhuru wa habari na wa kujieleza.

Lengo ni kutaka sheria rafiki itakayofanya mazingira ya kukusanya na kutoa habari Zanzibar kuwa rafiki na kuweza kuchangia vizuri maendeleo ya visiwa vya Unguja na Pemba.

Lakini kelele hizo zimekuwa kama zile za msemo maarufu wa Kiswahili wa kelele za mpangaji hazimzuwii mwenye nyumba kulala.

Zanzibar ilikuwa na historia nzuri na ya kuvutia ya habari na vijana wake kuchangia maendeleo ya sekta ya habri, hasa ya kufungua idhaa za Kiswahili katika nchi mbali mbali duniani.

Kutoka zama hizo na hadi leo visiwa hivi vimetoa manguli wa taaluma ya habari kwa nyakati mbali mbali.

Ni kwa kuwa na sheria ya habari rafiki ndio Zanzibar inaweza kurejesha hadhi na heshima yake na kutoa nafasi kwa waandishi wa kizazi cha hivi sasa na baadaye kuweza kuonyesha uwezo wao mkubwa wa kuelimisha jamii, kukosoa na kuishauri serikali, pamoja kupelekea sauti za wanyonge na watu wanaodai hawakutendewa haki kusikika.

Sheria nzuri za habari zitapelekea kuondokana na mwenendo wa sasa wa kutoa habari za huyu kasema, Yule kapongoza na mwengine katoa wito.

Badala yake zitasaidia kuibua masuala muhimu yayoigusa jamii na watu kuweza kuelewa serikali yao inafanya nini, bali hata kuiambia serikali wanataka nini.

Hii ikiwa na pamoja na kueleza wanataka vitu gani vipewe umhimu.


Kwa sasa vyombo vya habari vya Zanzibar haviwapi watu wanachokitaka na umma umekuwa ukipokea salamu tu za viongozi, lakini watu hawana nafasi ya kutosha ya wao kuwaambia viongozi wanachotaka au kuishauri serikali yao

Kwa muhtasari, waandishi wa habari wa Zanzibar wamekuwa kama matarishi wa kupeleka ujumbe kutoka kwa viongozi kwenda kwa wananchi na sio kuchukua salamu za wananchi kwenda kwa viongozi.

Mingoni mwa sheria zinazolalamiki kuwa zinawabana mbavu na koo waandishi wa habari wanaofanya kazi Zanzibar ni za Baraza la Wawakilishi, uchaguzi na ya mitandao. Sheria hizi zinahitaji kupigwa tochi ili ziwe na mazingira rafiki kwa waandishi wa habari.

Kuwepo kwa sheria hizi kumepelekea ulinzi wa waandishi wa habri kuwa hatarini na hii imethibitika kwa waandishi kupigwa marufuku , kupigwa kunyang’anywa vifaa vya kazi, kufunguliwa mashitaka bandia na baadhi ya vituo vya radio na magazeti kufungiwa.

Kwa mfano, panapotokea mwalimu wa skuli kufanya makosa hatuoni skuli kufungwa bali mwalimu aliyeenda kosa kuwajibishwa kisheria na hivyo hivyo daktari au muuguzi akikosa kufuata maadili huwajibishwa yeye na sio kufunga hospitali.

Lakini mwandishi akionekana labda ameipotosha umma au kafanya kosa utaona chombo chake kinaadhibiwa na hata kufungwa.


Tujiulize hivyo hii ni haki au uonevu kwa kutumia sheria ambazo nikandamizi?

Kwa kuwa na sheria ngumu na hatarishi kazi ya uwandishi wa habari Zanzibar imekuwa ngumu na hata kupelekea waandishi kutoweza kufuatilia habari ambazo wananchi wanataka ukweli wake.

Katika kila nchi waandishi wa habari sio tu mawakala wa kuleta mabadiliko ya kheri bali pia ndio sauti ya wanyonge. Sasa kama waanadishi wanatarajiwa kuzisikiliza sauti za wanyongwe, wamefungwa midomo na wananyang’anywa vifaa vyao vya kazi wataweza kuifanya kazi hii?

Hii ndio inayopelekea wananchi, kama wale ambao ardhi na mashamba yao kuporwa, kubaki wanalia na hawana wa kuwanyamaza.

Mtu akiibiwa hupeleka malalamiko yake polisi na uchunguzi hufanyika kumpata mhalifu, lakini watu wakiwa na malalamiko ya kukosa maji au huduma kuwa mbovu katika kituo cha afya hawawezi kwenda polisi kuweka riporti.

Kimbilio lao huwa kwa vyombo vya habari na kama waandishi mikono imefungwa pingu na midomo imefungwa wananchi watabaki kulalamika pembeni na sauti zao hazisikiki.

Wazo la kufanyanyiwa marekebisho ya sheria za habari limeshawahi kutolewa maelezo kuwa ndio nyezo itakayo fanya wanahabari kuwa na hamu ya kutoa taarifa zilizo na mvuto zaidi kutokana na baadhi ya wadau kuviorozesha vifungu visivyotoa fursa kwa waandishi kuteleza wajibu wao ipasavyo.

Wadau wa habari wanaonekana kuchoshwa na ahadi za serikali za kila siku kuambiwa zoezi la kurekebisha sheria za habari na kujieleza zipo mbioni.

Sasa ni zaidi ya miaka 20 tokea kusikika kuanza kwa hizo mbio. Ni vizuri hizo mbio zikafikia kwenye mfundo ili twende na wakati.

Ni kweli maneno matamu humtoa nyoka pangoni, lakini akitoka hutarajia hio ahadi aliopewa anaiona baada ya kutoka pangoni.

Kwani maneno mengine matamu hayamshibishi mtoto mwenye njaa anayetaka kunyonya

Anachohitaji ni chakula na sio maneno mazuri au kupakwa uturi.

Mwisho.

Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...