NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA
Waandishi
wa Habari Kisiwani Pemba wametakiwa kuzingatia weledi, maadili na taaluma ya Habari
katika kuandika na kuripoti taarifa zinazochochea amani na utulivu nchini.
Akizungumza
na Waandishi hao katika Ukumbu wa Baraza la Mji Chake Chake Afisa mdhamini
Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo Mfamau Lali Mfamau katika Kongamano la Kuimarisha
Amani kati ya Jeshi Polisi na Vyombo vya habari kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025, amesema
waandishi walioshiriki katika Kongamano hilo wanapaswa kuzingatia maelekelezo
waliyopatiwa katika kipindi cha Uchaguzi.
Aidha
Afisa huyo ameliomba Jeshi la Polisi kuwashughulikia Waandishi watakaokiuka
maelekezo yaliyotolewa kwenye Kongamono ili iwe mfano kwa waandishi wengine.
“Kwa
habati mzuri hapa munazungumza Kiswahili kimoja lakini mukikutana fild (eneo la
kazi) katika wale watu ambao mumewapa maelekezo halafu mukaja kugundua wale watu wambao tumekaa tumedicuss nao haya mambo umuhimu wa amani kuelekea katika
kipindi cha Uchaguzi halafu mule miongoni mwao mwandishi wa Habari mukamkuta kaingia katika shida sasa niwaombeni sana mtu kama
huyo wala musimuache mumshughulikie vizuri sana, yes narejea tena naomba hii moni note vizuri sana sasa niwaombe sana Jeshi la Polisi kwenye hili jambo musiwe na muhali wala musimuone mtu huruma kwasababu hakuna mbadala kwenye Amani” alisema
Akifungua
Kongamano hilo Kamishna wa Jeshi la Polisi Zanzibar Kombo Khamis Kombo ambaye alikuwa
Mgeni Rasmi, amesema ushirikiano kati ya Jeshi la Polisi na Waandishi wa Habari
ni nguzo muhimu katika kujenga amani na mshikamano kuelekea uchaguzi wa 2025”
“Nadhani
sote ni mashahidi yaliyotokea na yanayoendelea katika taifa mbali mbali duniani
baada ya amani kutoweka, hivyo basi kwa umoja wetu na taaluma zetu tunapaswa kuwa
na mashirikiano ya karibu katika kuhakikisha tunaitunza na kuilinda amani na
mashirikiano tuliyonayo katika taifa letu katiki kipindi chote cha uchaguzi na
baada” Kamishna wa Jeshi la Polisi Zanzibar Kombo Khamis Kombo
Akiwasilisha
mada ya Miiko na Maadili ya Vyombo vya Habari kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 Mkuu
wa Wilaya ya Micheweni Khatib Juma Mjaja, amewataka waandishi hao kutumia
taaluma yao kwa weledi kuripoti matukio yanayojiri kipindi cha uchaguzi ili
kuepukana na madhara yanayoweza kujitokeza.
“Niwasihi
tu licha ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Zanzibar kutupa fursa
ya kupokea na kutoa taarifa bila ya kuathiri Usalama wa Taifa nyinyi kama
waandishi munapaswa kutumia taaluma na weledi mulionao katika kuripoti matukio
ambayo hayatochochea machafuko na taharuki kwa taifa” Mkuu wa Wilaya Micheweni Khatib
Juma Mjaja
Kwa
upande Katibu wa Klabu ya Waandishi wa Habari Pemba Ali Mbarouk, amewasihi wanahabari
hao kuzichuja taarifa zao kabla ya kuzichapisha na kuzirusha kwenye vyombo sambamba
na kujiepusha na uchapishaji wa taarifa za uzushi na uongo.
“Hata
kama ni taarifa ulionayo nayo ni kweli lakini kama mwandishi wa Habari unapaswa
kuzichuja taarifa zako kabla kuzirusha pamoja kujiuliza je, Habari hii nikitoa
italeta athari gani kwa Taifa? Tutamubue kuwa hakuna Habari kubwa kama usalama
wako na taifa upo hatarini” Ali Mbarouk Katika PPC
Wakichangia
mada na hoja mbali mbali juu ya Kongamano hilo baadhi ya wanahabri hao wamesema
kumekuwepo na tabia ya baadhi ya Makamanda wa Jeshi la Polisi kutokutoa
ushirikiano kwa waandishi wa Habari hali inayochangia kuwarudisha nyuma
waandishi hao kufanya kazi kwa ukaribu na Jeshi hilo.
“Kwakweli
waandishi wa Habari Pemba tunakabiliwa changamoto nyingi sana miongoni mwa
changamoto hizo ni kwa upande wa Jeshi la Polisi baadhi ya Makamanda wa Mikoa
hawana mashirikiano na sisi waandishi unatafuta balance (usawa) kwa Jeshi la Polisi
kuhusu tukio fulani mwezi mzima unaambiwa mara kamanda hayupo mara yupo busy mpaka
unakata tamaa unaamua kuifanya hiyo Habari pasi na kauli ya Kamanda hiyo hali
inaturudisha nyuma sana kwakweli” Fatma Faki Salim, Mwandishi kutoka Blog ya
Pemba ya Leo
Suala
la usalama kwa waandishi wa Habari katika kipindi cha kupiga kura ni miongoni
mwa hoja iliyoibuka ambapo waandishi walisema kumekuwepo na matukio kadhaa ya
waandishi wa Habari kutishiwa amani na maafisa wa Jeshi la Polisi wakati
wanatekeleza majukumu hali inayosababisha kushindwa kutuekeleza majukumu yao
ipaswavyo.
“Kwa
miongo tofauti kumekuwepo na matukio ya waandishi wa Habari kutishiwa amani na watu
ambao tunashindwa kufahamu kuwa ni maafisa wa Jeshi la Polisi ama laa maana
hata mavazi yao sio ya Kipolisi, baadhi yao wameficha sura (mazombi) lakini
wanatumia magari ya poilisi na vikosi sasa kwakweli hali hiyo inatupa wakati
mgumu sana waandishi wa Habari kipindi cha Uchaguzi” Is-haka Mohammed Rubea,
mwandishI Zenj Fm Radio
Akitoa
ufafanuzi juu ya hoja hizo Mkuu wa Polisi Jamii Kamisheni ya Polisi Zanzibar Kamishna
Mwandamizi wa Polisi SACP Jonas Mahanga, ali0wataka waandishi hao kutoa taarifa
kwa viongozi wa Jeshi la Polisi pindi wanaoona viashiria vyovyote vya kuvunjiwa
usalama wao pamoja kuizuliwa kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa sheria.
Kongamano
hilo lenye lengo la Kuimarisha Amani Kupitia Hoja Na Mijadala Ya Maelewano
Baina Jeshi La Polisi Na Vyombo Vya Habari Kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025”
limebeba Kauli Mbiu inayosema
“AMANI,
UTULIVU, NA USALAMA KABLA YA WAKATI, NA BAADA YA UCHAGUZI 2025 NI JUKUMU LETU
SOTE”




Comments
Post a Comment