NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Visa vya Watoto kuzaliwa kutelekezwa na kutupwa vinaendelea kuchukua nafasi Kisiwani Pemba, hii ni baada ya mtoto mchanga wakike anaekadiriwa kuwa na wiki moja kukutwa ametelekezwa mbepezoni mwa Msikiti wa Mkanjuni Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Akisimulia kuhusu tukio hilo Sheha Mkoroshoni Zuwena Suleiman Salahi, alisema siku ya Ijumaa Agosti 29.08.2025 saa 1:30 usiku alipata taarifa kutoka kwa mjumbe wake za kuonekana kwa mtoto huyo akiwa ametelekezwa na mtu asiefahamika. Aidha Sheha huyo ametoa wito kwa wanawake kuacha tabia za kuwatelekeza na kuwatupa Watoto kwa kuhisi aibu ya kuzaa nje ya ndoa au sababu nyenginezo kwani kufanya hivyo ni kinyume na Sheria za Serikali na Dini. “Jana siku ya Ijumaa saa 1:30 usiku nilipata taarifa kutoka kwa mjumbe wangu wa sheha kuwa kuna mtoto ametupwa msikiti mkanjuni ndio nikatoka nikaenda nilipofika mtoto alikuwa ameshaondoshwa pale msikitini yupo kwa mjumbe wangu wa sheha nikenda kumuona kisha nikampigia simu M...