NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA
Licha Serikali kupitia Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar kuanzisha Sera ya elimu mjumuisho lakini ufikiwaji wa Sera hiyo kwa Watoto wenye Ulema wanaoishi vijijini ni changamoto iliyokosa ufumbuzi.
Hali hiyo inasababishwa na miundombinu mibovu ya Barabara, mashule pamoja hali za Watoto wenye Ulemavu kuzidi kuwa mbaya kutokana na kukosa visaidizi kama vile viti mwendo, walimu na vitendea kazi vyakusomea.
Shehia ya Wambaa ambayo inapitakana Wilaya ya Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba ina zaidi ya Watoto 12 wenye ulemavu mchanganyiko wakiwemo Wenye Ulemavu wa Viungo, Uziwi, macho na Ualbino lakini kati yao hakuna hata mmoja aliyepata fursa kupata elimu hata kwa kiwango cha kumaliza elimu ya msingi.
Juma Haji Khamis ni mtoto wa miaka 13 mkaazi wa Kijiji cha Kwa-Azani mwenye Ulemavu wa Viungo (tatizo la kutembea) akiwa mtoto wa 5 katika familia ya Watoto 6 wenye Ulemavu, ameshindwa kuendelea na masomo kutokana na hali yake ya Ulemavu inayosababisha kushindwa kufika Shuleni.
“Watoto wangu sita kati ya Watoto tisa wana ulemavu wa miguu na wakiume ni huyu Juma kwasababu Watoto wangu wengi ni wanawake, kwahivyo huu ulemavu unawafanya washindwe kuendelea na masomo huyu Juma alikuwa anakwenda skuli lakini baadae akawa anashindwa kutokana na hali yake kuzidi kuwa mbaya” alisema mama wa mtoto huyo Fatuma Simai Faki
Hadija Haji Makame miaka 12, mwenye Ulemavu wa Ualbino na mwenye ndoto ya kuwa Daktari Mkaazi wa Chumbageni ambaye ameshindwa kuendelea na masomo na kuishia darasa la tatu, alisema ameshindwa kuendelea na masomo kutokana kushindwa kusoma na kuandika kutokana na kukosa uwezo mzuri wa kuona kwenye madaftari.
Sheha wa Wambaa Mohammed Suleiman, amekiri kuwepo kwa tatizo hilo ambalo alisema linachangiwa na hali duni za kifamilia pamoja miundombinu isiyo rafiki ya Barabara, walimu na vitendea kazi maskulini sambamba na kuahidi kulifanyia kazi tatizo hilo kwa kulitolea taarifa kwa viongozi wa Wilaya.
“Kwanza nikiri kuwepo kwa tatizo hilo ambalo limezoeleka kwa jamii nyingi za vijijini na kuonekana ni jambo la kawaida tu lakini sisi kama wawakilishi wa jamii hua tunapata nafasi kila kuzungumza na viongozi wa Wilaya juu ya matatizo yanayojiri katika Shehia zetu kwahivyo hili nalo tutalifikisha kwa mabosi zetu ili kuona ni kwa namna gani wanaweza kulifanyia kazi”
“Tatizo hilo lipo sana katika jamii nyingi za vijijini binafsi hivi karibuni nimefanikiwa kuwarudisha Skuli, lakini tunashirikiana na kitengo cha Inclusive Education kutoka Wizara ya elimu kuwapeleka na kuwarudisha skuli wale ambao wamesha acha masomo ” Afisa wa Watu Wenye Ulemavu Wilaya ya Mkoani Warda Wally Mohammed
Mratibu wa Baraza la Watu Wenye Ulemavu Mashavu Mabrouk Juma, Sera ya Elimu ya mwaka 2022, imetoa fursa ya elimu kwa Watu Wenye Ulemavu ikiwemo ikiwemo kuboresha miundombinu rafiki maskulini, vifaa vya kufundishia pamoja na walimu wenye taaluma ya elimu mjumuishi.
“Kwakweli Serikali kupitia Wizara ya elimu kwa kushirikiana na Baraza la Taifa la Watu Wenye Ulemavu imepiga hatua kubwa sana kuboresha mazingira ya watu wenye ulemavu katika sekta ya elimu licha ya kuwepo kwa changamoto kadhaa hususan kwa upande wa vijijini kama ulivyosema lakini hilo sisi kama wasaizidizi wa Baraza tutahakikisha tunalifanyia kazi ipaswavyo” alifafanua


Comments
Post a Comment