HABARI NA, HASSAN MSELLEM-PEMBA
![]() |
Waandishi
wa Habari Kisiwani Pemba wametakiwa kuwa mabalozi kwa watu Wenye Wenye Ulemavu
kwa kuandika na kuripoti taarifa zao ili kutoa elimu kwa jamii kuhusu Kundi
hilo.
Hayo
yamenenwa na Afisa Programu na Mawasiliano wa Chama cha Waandishi wa Habari
Wanawake Tanzania (TAMWA) kanda ya Zanzibar Khairat Ali Haji, wakati akifungua
mafunzo ya siku tatu za kuwapiga msasa waandishi wa Habari Kisiwani Pemba
katika kuandika Habari jumuishi zitakazokuza ustwahi na haki za Watu Wenye Ulemavu.
Amesema
lengo la mafunzo hayo ni kuongeza utetezi kwa Watu Wenye Ulemavu ili kupata
haki zao kama ikiwemo haki ya kuchanganyika na wengine, elimu, kazi pamoja na
kushiriki kwenye siasa.
“Lengo la mafunzo ya kwenu ni kuwapiga msasa kusudi muwe na uwezo mzuri wa kuandika na kuripoti Habari za Watu Wenye Ulemavu ili nao waweze kupatiwa haki zao za msingi ambazo wamezikosa kwa muda mrefu sana kama vile haki ya kuchanganyika na wengine, haki ya elimu, kufanya kazi na kushiriki kwenye siasa ili waweze kuchagua na kuchaguliwa” alisema
Akiwasilisha
mada katika mafunzo hayo Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake Wenye Ulemavu Zanzibar (JUWAUZA) Bi. Salma Haji Saadat, amesema kwa mujibu wa matokeo ya Sensa ya Watu na Makaazi ya
2022, kati ya Wazanzibari milioni 1 na laki nane asilimia 11.4% ni wenye
ulemavu idadi inayoonekana kuongezeka maradufu kutoka asilimia 5.4% kwa mujibu
wa Sensa ya Watu na Makaazi ya 2012.
Ameongeza
kuwa kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) 2025 idadi ya
Watu Wenye Ulemavu imefikia asilimia 16% saw ana ongezeko la asilimia 1 kutoka
asilimia 15% kutoka mwaka 2011 wakati Dunia ikiwa idadi ya watu zaidi ya
bilioni saba
“Tafiti
zinaonesha idadi ya watu wenye ulemavu inaongezeka kila uchao na hii inatokana
na sababu mbali mbali ikiwemo vita kama tunavyoshuhudia vita vya muda mrefu
Izrael na Palestina, Izrael na Iran, Urusi na Ukrine, umasikini, ajali nakadhalika”
alisema
Aliongozekuwa
changamoto kubwa inayowakabili watu wenye ulemavu ni kutokukubaliwa na katika
jamii licha ya uwezo mkubwa walionao katika Nyanja mbali mbali kama vile vipawa
vya kielimu, uongozi, sanaa, biashara na ujasiriamali.
Alisema
“Watu Wenye Ulemavu hawana matatizo matatizo wanayo wanajmii wenyewe
kutokuwakubali na kuwaamini watu wenye ulemavu kutokana na ulemavu wao wakati
watu wenye ulemavu wana uwezo na vipawa vya kufanya vizuri kama wasio na
ulemavu jambo la msingi ni kuaminiwa na kupewa nafasi ili waweze kuonesha uwezo
na vipawa vyao”
Nao
waandishi wa Habari walioshiriki katika mafunzo hayo wameahidi kuyatumia
mafunzo waliopatiwa katika kuandika na kuripoti Habari za utetezi wa haki za
watu wenye ulemavu ili waweze kutimiza ndoto na malengo waliyojiwekea
Mafunzo
hayo ya siku 3 kwa waandishi wa Habari 10 Kisiwani Pemba, yametolewa na
TAMWA-ZNZ kupitia mradi wa miaka mitano wenye jina la Collective Actions for
Disability Right (CADiR) wenye lengo la kutetea na kukuza haki za Watu Wenye Ulemavu
kwa kushirikiana na Taasisi ya Watu Wenye Ulamavu ya Norway (NAD)



Comments
Post a Comment