Skip to main content

Waandishi wapigwa msasa malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto (ECD)

 NA, HASSAN MSELLEM-PEMBA

Waandishi wa habari Zanzibar wametakiwa kuripoti na kutoa elimu kwa jamii juu ya umuhimu wa malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto ili kuwa na taifa lenye ustawi bora.

Akizungumza na waandishi na wadau hao katika mafunzo ya siku nne yaliyofanyika huko katika ukumbi wa Hoteli ya Jamirex Mwenge Jijini Dar- Es- Salaam Katibu Mkuu kutoka Wizara ya elimu Zanzibar Dkt. Khamis Abdalla, amesema Dira ya maenedeleo endelevu ya 2050 ya Zanzibar itafikiwa endapo watoto watakuwa katika makuzi na malezi bora yenye kujenga maadili na maarifa

Aidha, Dkt. Khamis amewataka waandishi hao kuandaa vipinda, ripoti na Makala mbali mbali zitakazochochea haki za Watoto ikiwemo haki kupata elimu, chanjo, vyeti vya kuzaliwa na kuwalinda na kuwahifadhi.

Kwa upande wake Meneja mradi Bi. Mariam Issa,  amesema Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kupitia Wizara ya Afya imeamuaa kuongeza nguvu katika Malezi, Makuzi na Maendeleo ya awali ya mtoto kutokana na umuhimu wa rika hilo katika makuzi bora ya afya ya mwili na akili ya mtoto.

“kwahivyo licha ya Serikali kupitia Wizara ya afya kuboresha huduma za afya imeona kuna haja kubwa ya kuongeza nguvu katika makuzi, malezi na maendeleo ya awali ya mtoto kuanzia umri mwaka 0 hadi miaka 8 ili kuwa na Watoto wenye afya bora ya kimwili na kiakili” Alisema

Meneja Mradi Bi. Mariam issa

Mapema akizungumza katika mafunzo hayo mtaalamu wa malezi, makazi na maendeleo ya awali ya mtoto kutoka taasisi ya Children in Grassfire Davis Gisuka, amesema malezi na makuzi ya mtoto yanaanza tangu mtoto akiwa tumboni kwa mama hadi kufikia umri wa miaka nane ikiwemo kuwasiliana, lishe na kujifunza.

Alisema “makuzi ya mtoto huanzia tangu akiwa tumboni kwa mama yake na ndio maana tunasema kuanzia 0 hadi miaka 8, hivyo wazazi wanatakiwa kuwasiliana vizuri na mtoto, mama anapaswa kula vyakula vyenye lishe kuwasiliana nae vizuri ili kuimarisha afya ya mtoto kimwili, kiakili na kitabia”

Mtaalamu wa malezi, makazi na maendeleo ya awali ya mtoto kutoka taasisi ya Children Grassfire bwana Devis Gisuka

Naye, Muwezeshaji kutoka Madrasa Childhood Bi. Sharifa Suleiman Majid ameeleza kuwa miongoni mwa mambo yanayochangia mfumo bora wa makuzi ya mtoto ni pamoja na kuwa na afya bora, lishe, elimu ya mapema, malezi yenye uwajibikaji, ulinzi na usalama wa mtoto.

“Shirika la afya Duniani (WHO) UNICEF, Benki ya Dunia NCF wameainisha mambo Matano muhimu yanayohusu makuzi bora ya mtoto ambayo ni lishe, elimu ya mapema, malezi yenye uwajibikaji pamoja na ulinzi na usalama nav yote hivyo hakuna bora zaidi kuliko vyengine vinategemeana kwahivyo munapaswa kuelimisha jamii juu ya mambo hayo ili waweze kufahamu umuhimu wake” Bi. Sharifa Suleiman

Muwezeshaji kutoka Madrasa Childhood Bi. Sharifa Suleiman Majid.

Nao, baadhi ya wanahabari hao wameahidi kuyafanyia kazi mafunzo hayo kwa kuelimisha jamii pamoja kuripoti taarifa za matukio mbali mbali yanayohusu Watoto ili kuhakikisha jamii inapokea mabadiliko chanya kuhusu makuzi, malezi na maendeleo ya awali ya mtoto

“Kwa hakika mafunzo haya yametupa mwanga wakutosha kuhusu mambo ya ECD ni jukumu letu sasa waandishi kuhakikisha tunatoa elimu kwa jamii pamoja kuandika na kuripiti taarifa mbali mbali ya makuzi, malezi na maendeleo ya mtoto ili jamii zetu ziweze kupata mabadiliko chanja juu ya mausla haya na kwa niaba ya waandishi wenzangu tunaahidi kuyafanyia kazi ipaswavyo mafunzo haya” Mwinyimvua Nzukwi Katibu Klabu ya waandishi wa habari Zanzibar (ZPC) 

Mafunzo hayo kuhusu Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto kwa waandishi wa Habari na wadau wa afya Zanzibar yameandaliwa na Taasisi ya Afisi ya Rais Ufuatiliaji na Usimamizi wa Utendaji Serikalini Zanzibar (ZPDB) kwa kushirikiana na Taasisi mbali mbali ikiwemo Wizara ya Afya, Wizara ya Elimu, Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na Watoto na Klabu ya Waandishi wa Habari Tanzania na kunafadhiliwa na UNICEF

Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...