NA, HASSAN MSELLEM-PEMBA
Waandishi wa habari Zanzibar wametakiwa kuripoti na kutoa elimu kwa jamii juu ya umuhimu wa malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto ili kuwa na taifa lenye ustawi bora.
Akizungumza na waandishi na wadau hao katika mafunzo ya siku nne yaliyofanyika huko katika ukumbi wa Hoteli ya Jamirex Mwenge Jijini Dar- Es- Salaam Katibu Mkuu kutoka Wizara ya elimu Zanzibar Dkt. Khamis Abdalla, amesema Dira ya maenedeleo endelevu ya 2050 ya Zanzibar itafikiwa endapo watoto watakuwa katika makuzi na malezi bora yenye kujenga maadili na maarifa
Aidha, Dkt. Khamis amewataka waandishi hao kuandaa vipinda, ripoti na Makala mbali mbali zitakazochochea haki za Watoto ikiwemo haki kupata elimu, chanjo, vyeti vya kuzaliwa na kuwalinda na kuwahifadhi.
Kwa upande wake Meneja mradi Bi. Mariam Issa, amesema Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kupitia Wizara ya Afya imeamuaa kuongeza nguvu katika Malezi, Makuzi na Maendeleo ya awali ya mtoto kutokana na umuhimu wa rika hilo katika makuzi bora ya afya ya mwili na akili ya mtoto.
“kwahivyo licha ya Serikali kupitia Wizara ya afya kuboresha huduma za afya imeona kuna haja kubwa ya kuongeza nguvu katika makuzi, malezi na maendeleo ya awali ya mtoto kuanzia umri mwaka 0 hadi miaka 8 ili kuwa na Watoto wenye afya bora ya kimwili na kiakili” Alisema
![]() |
| Meneja Mradi Bi. Mariam issa |
Alisema “makuzi ya mtoto huanzia tangu akiwa tumboni kwa mama yake na ndio maana tunasema kuanzia 0 hadi miaka 8, hivyo wazazi wanatakiwa kuwasiliana vizuri na mtoto, mama anapaswa kula vyakula vyenye lishe kuwasiliana nae vizuri ili kuimarisha afya ya mtoto kimwili, kiakili na kitabia”
“Shirika
la afya Duniani (WHO) UNICEF, Benki ya Dunia NCF wameainisha mambo Matano muhimu
yanayohusu makuzi bora ya mtoto ambayo ni lishe, elimu ya mapema, malezi yenye
uwajibikaji pamoja na ulinzi na usalama nav yote hivyo hakuna bora zaidi kuliko
vyengine vinategemeana kwahivyo munapaswa kuelimisha jamii juu ya mambo hayo
ili waweze kufahamu umuhimu wake” Bi. Sharifa
Suleiman
Nao,
baadhi ya wanahabari hao wameahidi kuyafanyia kazi mafunzo hayo kwa kuelimisha
jamii pamoja kuripoti taarifa za matukio mbali mbali yanayohusu Watoto ili
kuhakikisha jamii inapokea mabadiliko chanya kuhusu makuzi, malezi na maendeleo
ya awali ya mtoto
“Kwa hakika
mafunzo haya yametupa mwanga wakutosha kuhusu mambo ya ECD ni jukumu letu sasa
waandishi kuhakikisha tunatoa elimu kwa jamii pamoja kuandika na kuripiti
taarifa mbali mbali ya makuzi, malezi na maendeleo ya mtoto ili jamii zetu
ziweze kupata mabadiliko chanja juu ya mausla haya na kwa niaba ya waandishi
wenzangu tunaahidi kuyafanyia kazi ipaswavyo mafunzo haya” Mwinyimvua Nzukwi Katibu Klabu ya waandishi wa habari Zanzibar (ZPC)
Mafunzo hayo kuhusu Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto kwa waandishi wa Habari na wadau wa afya Zanzibar yameandaliwa na Taasisi ya Afisi ya Rais Ufuatiliaji na Usimamizi wa Utendaji Serikalini Zanzibar (ZPDB) kwa kushirikiana na Taasisi mbali mbali ikiwemo Wizara ya Afya, Wizara ya Elimu, Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na Watoto na Klabu ya Waandishi wa Habari Tanzania na kunafadhiliwa na UNICEF













Comments
Post a Comment