NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA
Wazazi
na walezi wa Vijiji vya Kwa-Azani na Kutukuu Shehia ya Wambaa Wilaya ya Mkoani
Mkoa wa Kusini Pemba, wametakiwa kuwalea Watoto wao katika misingi bora ili
kuepukana na matatizo yanayoweza kujitokeza ikiwemo ajira za utoto na
udhalilishaji.
Akizungumza
na wananchi hao katika Uwanja wa mpira Kwa-Azani Afisa Ustawi wa Jamii Wilaya
ya Mkoani Bimchanga Mussa Mohammed, amesema kumekuwepo na wimbi kubwa la Watoto
wanaojishughulisha na shughuli za Uvuvi na kutumikishwa na wafanya biashara
hali inayosababisha hali inayochangia Watoto hao kuacha kwenda Skuli.
“Jamani tunatakiwa kuwalea Watoto wetu katika misingi bora ya kijamii na kidini sio kuishia tu kuwatunza tu kwa kuwapa chakula na nguo mtoto usipomsimamia ukahakikisha kuwa anawenda Skuli na madrasa vizuri kinachofata ni kujiingiza katika makundi maovu yakiwemo ya udhalilishaji na uhalifu” alisema
Kwa
upande Afisa wa Watu Wenye Wilaya ya Mkoani Warda Wally Mohammed, amesema tafiti
zinaonesha matukio mengi ya vitendo vya udhalilishaji katika jamii hutokea kwa
Watoto waliyoacha masomo na kujiingiza katika vikundi viovu.
Aidha amewataka Wananchi hao kutokuwaficha watoto Wenye Ulemavu na badala yake kuwatoa ili waweze kuchanganyika na wengine, kipata haki yao ya msingi ya elimu sambamba na kuacha kuwaita majina yasifaa ambayo yanaongeza kuwanyanyapaa.
“Ndugu
zangu mtoto anapoacha masomo kuna uwezekanao mkubwa wa kufanyiwa vitendo vya
udhalilishaji aidha na Watoto wenzake au hata watu wazima kwasababu anakuwa
katika mazingira yasiyo rafiki, tofauti na mtoto ambaye muda mwingi yupo shule
au madrasa”
Nae
Afisa Maendeleo ya Jamii Wilaya ya Mkoani Bi. Asia Abdalla Said, amewataka
wazazi na walezi wa vijiji hivyo kuwasimamia Watoto kwenye suala la elimu ili kupata
wataalamu wa fani mbali mbali vijiji humo.
“Jamani
sasa hivi miji na vijiji vinapambana kufaulisha wanafunzi ili kupata wataalamu
na watumishi wa Umma kutoka maeneo yao kwani unapokwenda sehemu kutaka huduma
unapomkuta mtu kutoka kwenu roho inakutua pia anapokuwepo hapa mtaani mutapata
nafuu ya kwenda kutafuta masafa ya mbali” alisisitiza
Nae
afisa Dawati la Jinsia Polisi Mkoani Rehema Omar Mjawiri, wiriamewataka
wananchi hao kutokuwa na muhali na vitendo vya udhalilishaji wa Watoto ili
kuwaepusha na athari za hivyo ambavyo vinaonekana kushamiri.
“Niwasihi
sana kuwalinda Watoto wenu na viashiria vya vitendo vya udhalilishaji kwanini
nasema viashiria, kwasababu mtoto akishadhalilishwa ni vigumu kurudi katika
hali yake ya zamani hali inayochangia kuathirika kisaikolojia na kutokutimiza
ndoto zao”
Sheha
(Mwenyekiti) wa Shehia (Kata) Wambaa Mohammed Suleiman, amewaomba wazazi na
walezi kuyafanyia kazi miongozo na maelekezo walipewa na maafisa hayo ili kuwa
na jamii yenye ustawi bora.
“Tayari
wenzetu wameshamitimiza jukumu lao la kutufikishia ukumbusho, sasa ni juu yetu
kuyafanyia kazi maelekezo na miongozo waliotufikishia tusisubiri yatufike kisha
twende maofisini kwao kuomba msaada wa ushauri huo sio uungwana” Sheha Wambaa
Nao
baadhi ya wananchi wa vijiji hivyo walisema miongoni mwa sababu zinachangia
Watoto wao kuacha masomo ni pamoja wazazi kutokutambua jukumu lao la malezi sambamba
na kutoa vitisho kwa watu wanaosimamia malezi ya watoto wakiwemo Polisi Jamii.
“Kwakweli
asilimia 90% ya wazazi tunakiri kuwa hatutambui jukumu yetu kwa Watoto wetu
zaidi ya kulisha na kuvisha lakini ni wachache sana miongoni mwetu ambao
wanatambua kuwa mtoto kwenda skuli na chuoni ni jukumu lake la msingi cha
kusikitisha zaidi hata wale Polisi jamii ambao kwa hiari yao bila ya malipo
wanajitolea kupambana na vitendo viovu ikiwemo Watoto kutokwenda skuli na kuiba
baadhi ya wazazi wanawatishia amani Polisi Jamii” Kiongozi wa Polisi Jamii Kijiji cha Kutukuu Ussi Haji
Mkutano
huo umefanyika kufuatilia mwandishi wa Habari hizi kushuhudia idadi kubwa ya
Watoto wasio na maendeleo mazuri ya kielimu pamoja na walioacha masomo.
MWISHO









Comments
Post a Comment