Skip to main content

MWEZI JULY NA AGOSTI VICHANGA VIWILI VYATELEKEZWA NA KUTUPWA PEMBA.

NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA

 

Visa vya Watoto kuzaliwa kutelekezwa na kutupwa vinaendelea kuchukua nafasi Kisiwani Pemba, hii ni baada ya mtoto mchanga wakike anaekadiriwa kuwa na wiki moja kukutwa ametelekezwa mbepezoni mwa Msikiti wa Mkanjuni Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba.

Akisimulia kuhusu tukio hilo Sheha Mkoroshoni Zuwena Suleiman Salahi, alisema siku ya Ijumaa Agosti 29.08.2025 saa 1:30 usiku alipata taarifa kutoka kwa mjumbe wake za kuonekana kwa mtoto huyo akiwa ametelekezwa na mtu asiefahamika.

Aidha Sheha huyo ametoa wito kwa wanawake kuacha tabia za kuwatelekeza na kuwatupa Watoto kwa kuhisi aibu ya kuzaa nje ya ndoa au sababu nyenginezo kwani kufanya hivyo ni kinyume na Sheria za Serikali na Dini.

“Jana siku ya Ijumaa saa 1:30 usiku nilipata taarifa kutoka kwa mjumbe wangu wa sheha kuwa kuna mtoto ametupwa msikiti mkanjuni ndio nikatoka nikaenda nilipofika mtoto alikuwa ameshaondoshwa pale msikitini yupo kwa mjumbe wangu wa sheha nikenda kumuona kisha nikampigia simu Mkuu wa Wilaya nikawapata taarifa Jeshi la Polisi nikamchukua nikampeleka hospitali akafanyiwa vipimo baada ya kufanyiwa vipimo nikarudi nae nyumbani” alisema 

Akitoa ufafanuzi kuhusu jukumu la Ustawi wa Jamii kwa Watoto wanaotelekezwa na kutupwa, Afisa Ustawi wa Jamii Wilaya ya Mkoani Zuwena Mohammed Mussa, alisema jukumu la Ustawi wa jamii ni kuwatunza na kuwalea Watoto hao kupitia walezi wa malezi (Foster Parent) ambao wanapatikana kila Shehia.

“Kama ikitokea mtoto katelekezwa au katupwa sisi tuna walezi wa malezi (Foster Parent) hawa walezi wa malezi ambao tunawaweka kila Shehia jukumu lao hao ni kuwatunza Watoto hao ili kuwaepesha na madhara ambayo yanaweza kumpata kwa kipindi hicho na hapo atakuwa chini ya uangalizi wa Afisa ustawi wa Wilaya husika na atakaa hapo kwa kipindi tukiwa tunafuatilia je, kuna uwezekano wa kuipata familia yake kwasababu sisi Ustawi tunasema malezi bora ni kwa wazazi, sasa ikiwa haitokea familia au mtu wa karibu sasa hapo ndipo Mkurugenzi Ustawi ataamua wapi ampeleke na kumpeleka ni Unguja kwenye vituo vya kulelea Watoto kwasababu Pemba hatuna vituo hivyo” alifafanua Afisa huyo

Ikumbukwe kuwa July 30.2025 Amina Rashid Abass miaka 22, mkaazi wa Michakweni Shehia ya Kiwani Wilaya ya Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba alishikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kujifungua na kumtupa mtoto kwenye shimo la choo na kufariki Dunia.

Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...