Skip to main content

JELA JELA MIAKA 60 KWAJELA MIAKA 60 KWA KUMBAKA MSICHANA WA MIAKA 16.

NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA

Mahakama ya Kupambana na Makosa ya Udhalilishaji Mkoa wa Kusini Pemba Chake Chake, Jana April 14 imemuhukumu kutumikia Chuo cha Mafunzo Ismail Ussi Makame miaka 19, mkaazi wa Mikarafuuni kwa makosa mawili ya Ubakaji.

Mbele ya Hakimu wa Mahakama hiyo Taki Abdalla Habib, imeelezwa na mwendesha Mashtaka Asia Ibrahim Mohamed, kuwa tarehe 19.12.2025 saa  7:00 za usiku huko Kinyasini Mkoani Wilaya ya Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba, mshtakiwa alimbaka msichana wa miaka 16 baada ya kumtorosha msichana huyo kutoka nyumbani kwao na kwenda nae sehemu anayolala, jambo ambalo ni kosa kisheria kwa mujibu wa kifungu cha 108(1)(2) na 109(1) Shehia ya adhabu Sheria Nambari 6 ya mwaka 2018 Sheria ya Zanzibar likiwa ni kosa la kwanza.

Katika kosa la pili, tarehe 20.12.2025 saa 7:30 za usiku mshtakiwa alimbaka tena msichana huyo.

Kesi hiyo ilianza kusikilizwa Mahakamani hapo  06.01.2026 na idadi ya mashahidi 6 walitoa ushahidi ambao haukuacha chembe ya shaka, hivyo Mahakama imemtia hatiani mshtakiwa na kumuhukumu kutumikia chuo cha Mafunzo miaka 30 kwa kosa la kwanza na miaka 30 kwa kosa la pili, hata hivyo Mahakama imeamua adhabu hizo ziende sambamba hivyo mshtakiwa atatumikia Chuo cha Mafunzo miaka 30 mshtakiwa ili iwe fundisho kwake na kwa wengine wenye tabia kama hizo.

Hukumu hii inafikisha jumla ya hukumu saba (7) za makosa ya Udhalilishaji na Ubakaji ambazo zimetolewa na Mahakama ya kupambana na Makosa ya Udhalilishaji Mkoa wa Kusini Pemba Chake Chake kutoka mwezi March, 2026 Hadi May 14.2026 ambapo katika kesi hizo washtakiwa sita (6) ambao wengi wao ni Vijana wenye umri kati ya miaka 18 na 20 walitiwa hatiani na kuhukumiwa vifungo tofauti  ikiwemo miaka 15 na 30.

Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...