AJISALIMISHA KITUO CHA POLISI KUDAI MTOTO WAKE ALIYEMTUPA.
Novemba 15.2025 kipindi Cha Mawio kiliripoti tukio la mtoto mchanga wakike mweye umri wa wiki moja kutupwa huko Kitope ambapo aliyemtupa mtoto hakufahamika
Hatimae Jana Novemba 21.2025 Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Tattu Mohamed mwenye umri wa miaka 26, mkaazi wa Mfenesini Unguja, Zanzibar amejisalimisha katika Kituo cha Polisi Mahonda kudai mtoto wake na kusema sababu zilizopelekea kumtupa mtoto wake ni tatizo la kupatwa na mashetani.
Kamanda wa Polisi Kamishna Msaidizi wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Unguja Benedict Mapujila, amesema Mama huyo alikwenda kujisalimisha Kituo Cha Polisi Mahonda na kukiri kuwa yeye ndiye aliyemtupa mtoto huyo kutokana na kupatwa na matatizo ya mashetani ambaye ni mtoto wake Tatu ingawa alimzaa nje ya ndoa.
Aidha Kamanda Mapujila, amesema kumtupa mtoto ni Kosa Kisheria hivyo Jeshi la Polisi litamshtaki Mama ili Sheria ifate mkondo wake na kutoa wito kwa jamii kutokufanya maamuzi ambayo yako kinyume na Sheria na badala yake kufata Sheria ili kupata ufafanuzi ni changamoto zinawakabili.
Matukio ya watoto kutupwa, kutelekezwa na hata kuuawa yamekuwa yakitokeza mara kwa mara Visiwani Zanzibar, ikumbukwe kuwa Agosti 1.2025 Amina Rashid Abass miaka 22, mkaazi wa Michakweni Shehia ya Kiwani Wilaya ya Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba alishikiliwa na Jeshi la Polisi kwa Kosa la kumtumbukiza mtoto wake mchanga kwenye shimo la Choo baada ya kujifungua kwa kile kinachodaiwa kuwa alihisi aibu baada ya kujifungua nje ya ndoa.
Ijumaa Agosti 29.08.2025 saa 1:30 usiku huko eneo la Mkanjuni Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, alionekana mtoto mchanga anayekadiwa kuwa na wiki moja kutelekezwa pembezoni mwa msikiti na mwezi July 30.2025 Amina Rashid Abass miaka 22, mkaazi wa Michakweni Shehia ya Kiwani Wilaya ya Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba alishikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kujifungua na kumtupa mtoto kwenye shimo la choo na kufariki Dunia.
Comments
Post a Comment