Skip to main content

Mkurugenzi wa TAMWA–Zanzibar Dk. Mzuri Aaga Rasmi, Aweka Alama Kubwa ya Mageuzi ya Kijinsia.

HABARI, NA HASSAN MSELLEM.

Baada ya zaidi ya miongo miwili ya kujitolea, uongozi na harakati za kutetea haki za wanawake, watoto na uhuru wa vyombo vya habari, Mkurugenzi wa Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania, Tawi la Zanzibar (TAMWA–ZNZ), Dk. Mzuri Issa Ali ameaga rasmi waandishi wa habari kutokana na kuondoka katika wadhifa wake, akiacha taasisi imara yenye mifumo thabiti na mafanikio yanayotambulika kitaifa na kimataifa.

Akizungumza mbele ya waandishi wa habari, viongozi wa serikali, wadau wa maendeleo na wanachama wa TAMWA–ZNZ, Mkurugenzi huyo amesema waandishi wa habari ndio nguzo kuu ya taasisi hiyo licha ya changamoto kubwa wanazokumbana nazo lakini bado waliendelea kushirikiana na Tamwa Zanzibar katika kutumia kalamu zao kuelezea harakati za shughuli za Tamwa Zanzibar.

“Kama kuna kundi la watu wanaojua kuuliza maswali magumu, kufuatilia ukweli bila kuchoka, na bado malipo yakawa madogo au hakuna kabisa, basi hao ni waandishi wa habari. Na cha kufurahisha zaidi, hao ndio nguzo kuu ya TAMWA–Zanzibar,” alisema.

Alisema kuwa katika kipindi cha kuwa mtendaji mkuu wa Tamwa Zanzibar alifarijika sana na waandishi wa habari kutokana na kutumia vyema kalamu na vipaaza sauti katika kueleza changamoto za kijamii hususan masuala ya haki za binaadamu pamoja na vitendo vya udhalilishaji vya wanawake na watoto.

“kalamu za waandishi ilikuwa ndio nguzo kuu ya kutegemea katika kipindi cha uongozi wangu nikiwa mkurugenzi kalamu zilipaaza sauti za wasio na sauti pamoja na kueleza changamoto za kijamii hususan katika masuala ya ukiukwaji wa haki za binaadamu”, alifafanua mkurugenzi.

Akieleza kuwa mashirikaino hayo ya karibu yameweza kwa kiasi kikubwa kusaidia jamii na kupungua changamoto za wanawake na watoto pamoja na makundi mengine ya pembezoni kama walemavu na wazee.

“Nguvu yetu ilikuwa ni ya waandishi wa habari tukiamini kuwa nguvu ya habari inaweza kuleta mabadiliko chanya katika jamii lakini pia kuibua kero za wananchi pamoja na kuizundua serikali” alisisitiza.

Kupitia miradi mbalimbali, TAMWA–ZNZ imefanikiwa kuwafikia zaidi ya wanawake na watu wenye ulemavu 11,120 kupitia vikundi 572 vya kuweka na kukopa, kuimarisha mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia, na kuchangia mabadiliko ya sheria muhimu ikiwemo Sheria ya Ushahidi, Sheria ya Mahakama ya Kadhi na Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai.

Leo, TAMWA–Zanzibar ina wanachama 82 waandishi wa habari kutoka Unguja na Pemba, wafanyakazi 23 wenye weledi, mifumo imara ya kifedha inayoendeshwa na wahasibu wenye ithibati ya CPA, pamoja na ukaguzi wa hesabu unaofanywa na kampuni zilizosajiliwa kitaifa. Taasisi hiyo pia inamiliki majengo yake yenyewe ambayo yameanza kuchangia mapato ya ndani.

Katika hafla hiyo, Mkurugenzi huyo alitangaza rasmi kukabidhi majukumu kwa Bi. Nairat Abdulla Ali, aliyekuwa Meneja wa Programu, akimtaja kuwa kiongozi mwenye maadili, uwezo na maono thabiti ya kuiendeleza taasisi hiyo.

“Nawaomba wanachama, waandishi wa habari na wadau wote kumpa ushirikiano mkubwa. Taasisi imara haijengwi na mtu mmoja, bali hudumu pale uongozi unapobadilika na dira ikibaki ile ile,” alisema.

Katika hafla hiyo waandsihi wa habari waliohudhuria waliishukuru kwa dhati Tamwa Zanzibar kwa kuwa nao karibu pamoja na kuwajengea uwezo katika kuimarisha weledi na umahiri katika taaluma ya habari.

Khatib Suleiman kutoka Habari leo amesema kuwa Tamwa imetusaidi kutujengea uwezo hususan katika kuandika kwa weledi na kuimarisha uwezo wetu katika namna ya kuripoti masuala ya haki za wanawake na watoto pamoja na haki za binaadamu kwa ujumla.

“Tamwa Zanzibar imekuwa ni chuo katika kuimarisha taaluma ya uandishi na tumeweza kuandika kwa weledi na umahiri huku tukizingatia maadili ya wanahabari”, alifafanua.

Berema Suleiman kutoka Zenji Fm alisema kuwa tamwa Zanzibar imekuwa mstari wa mbele katika kuimarisha taaluma lakini pia katika kuwapatia mafunzo waandishi chipukizi katika kuimarisha utendaji wa kazi zao.

“Mafunzo tuliyoyapata yamesaidia katika kuimarisha taaluma na kutujengea uwezo hususan katika kufuatilia habari zetu pamoja na kuwa na vyanzo tofauti na kuwapa nafasi makundi ya wanawake na vijana pamoja na walemavu”, alifafanua.

Wafanyakazi wa tamwa Zanzibar walishukuru kwa uongozi wa Dk. Mzuri hususan katika kuimarisha utendaji wa kazi zao huku wakizingatia weledi na umahiri katika kuandika ripoti na pia kufanya kazi kwa kuweza kupata matokeo

Zaina Mzee Afisa mwandamizi wa Tamwa Zanzibar alisema kuwa ulipokuja kuongoza taasisi hii, hukurithi tu ofisi na majukumu, bali pia changamoto nyingi. Kwa busara, maono na uongozi wako thabiti, uliweza kuibadilisha taasisi yetu na kuifanya kuwa mfano wa uwajibikaji, mshikamano na utendaji bora. Chini ya uongozi wako, tulijifunza kuwa kazi si wajibu tu, bali ni wito na dhamana ya kulitumikia taifa kwa uadilifu.

Akitoa neno la shukurani mkurugenzi mpya wa Tamwa Zanzibar Nairat Abdulla amesema kuwa napokea dhamana hii nikiwa na ufahamu kwamba uongozi si kauli, bali ni vitendo; si ahadi, bali ni uwajibikaji. Ninapokea nafasi hii nikitambua kuwa taasisi huimarika si kwa mipango iliyoandikwa vizuri pekee, bali kwa utekelezaji thabiti, wenye nidhamu na mwelekeo unaofahamika. 

Ninawaahidi kushirikiana nanyi kwa karibu, kusikiliza kwa makini, na kuchukua hatua kwa wakati. Milango yangu itakuwa wazi kwa hoja, mawazo na suluhisho, kwa sababu uongozi wa pamoja na mashirikiano ni muhimu katika kuimarisha kazi zetu, alisisitiza.

Hafla hiyo ilihitimishwa kwa kutoa zawadi mbali mbali kwa mkurugenzi aliyemalaiza muda Dk. Mzuri Issa ikiwa ni sehemu muhimu ya kutunza kumbukumbu ya utumishi wake uliotukuka.

End. 

Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...