Skip to main content

"ZAMECO" YASISITIZA KUWEPO KWA HAKI, UHURU WA KUTOA NA KUPATA TAARIFA.

HASSAN MSELLEM - PEMBA

Kamati ya Wataalamu wa Masuala ya Habari Zanzibar (ZAMECO) inaungana na wanaharakati, wanahabari, na watetezi wa haki za binadamu duniani kote, kuadhimisha siku ya Haki za Binaadamu ambayo hufanyika kila ifikapo tarehe 10 Disemba ya kila mwaka. 

Kaulimbiu ya mwaka huu, haki za binadamu kama “Mahitaji ya Kila Siku”, inasisitiza kuwa haki hizi lazima zilindwe bila kusuasua kila siku, kwa kila mtu, na katika kila mazingira.

Katika maadhimisho ya mwaka 2025, ZAMECO inasisitiza kwamba uhuru wa kupata na kutoa taarifa ni nguzo muhimu ya utawala bora na msingi wa kulinda haki nyingine zote za binadamu. 

Haki hii haipaswi kutazamwa kama ridhaa ya mamlaka bali kama wajibu wa kikatiba na kimataifa unaopaswa kuheshimiwa, kulindwa na kutekelezwa.

Tunawakumbusha wadau wote kuwa tangu kupitishwa kwa Tamko la Ulimwengu la Haki za Binadamu (UDHR) mwaka 1948 uhuru wa kujieleza umeendelea kuwa nguzo muhimu katika kuhakikisha kwamba jamii inakuwa na nguvu ya kushiriki, kuuliza, na kuhoji madaraka.

Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Zanzibar katika Ibara ya 18 zimeeleza haki hiyo ya kujieleza na kupata taarifa.

Hii hupelekea upatikanaji wa taarifa sahihi, waandishi wa habari na wananchi wanapata uwezo wa kuhoji, kushiriki, kuwawajibisha watawala na kuchochea uwazi katika masuala ya kijamii, kisiasa na kiuchumi.

Hata hivyo, pamoja na msingi huu muhimu, bado tasnia ya habari Zanzibar inakumbana na vikwazo vinavyozuia utekelezaji kamili wa haki hizi. Sheria zilizopitwa na wakati, mazingira ya hofu, vitisho dhidi ya waandishi, pamoja na ukosefu wa upatikanaji wa taarifa za umma kwa wakati. 

Hali hii inadhoofisha uwezo wa vyombo vya habari kufanya kazi yao kwa uhuru na uadilifu na kuwanyima wananchi haki ya kupata taarifa sahihi, jambo ambalo linaathiri ushiriki wao katika maamuzi ya nchi.

Sheria hizo ni pamoja na Sheria ya Wakala wa Habari, Magazeti na Vitabu ya mwaka 1988 ilifanyiwa marekebisho mwaka 1997 pamoja na Sheria ya Tume ya Utangazaji Zanzibar ya mwaka 1997 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2010 ambazo zinaendelea kutoa mamlaka makubwa kwa taasisi za usimamizi na kuathiri uhuru wa vyombo vya habari kufanya kazi kwa weledi na bila ya hofu.

Katika taarifa yake ya mwisho kwa waandishi wa habari, kabla ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025, ZAMECO ilieleza masikitiko yake ya kuzorota kwa mazingira ya upatikanaji wa habari na ukiukwaji wa haki za kujieleza na kupata habari.

Miongoni mwa ukiukwaji huo ni kunyimwa taarifa muhimu kwa waandishi wa habari, kutishiwa kufungiwa kwa baadhi ya vyombo vya habari kutokana na kutokulipa ada na kurusha maudhui ambayo hayakuelezwa bayana tatizo lake.

Pamoja na changamoto hizo, ZAMECO inaona umuhimu mkubwa wa wadau wote kushirikiana kurejesha imani na kujenga mazingira salama na huru kwa uandishi wa habari. 

Tunatoa wito kwa Serikali ya Zanzibar kufanya mapitio ya kina ya sheria za habari ili ziendane na hali ya sasa ya soko huria, maendeleo ya teknolojia, matakwa ya Katiba, viwango vya kikanda na kimataifa. Katika Maadhimisho ya Siku ya Haki za Binadamu ya mwaka huu, ZAMECO inasisitiza kuwa uhuru wa habari ni uti wa mgongo wa utawala bora na msingi wa demokrasia jumuishi. 

Hakuna maendeleo, uwajibikaji, wala uchaguzi huru bila habari huru na waandishi walio salama. Kwa msingi huo, ZAMECO itaendelea kusimama imara kutetea haki, usalama, na maslahi ya waandishi wa habari Zanzibar, huku tukihamasisha wadau wote kutambua haki zao na kuzidai pale zinapokiukwa. 

IMETOLEWA NA

Klabu ya Waandishi wa Habari Zanzibar (ZPC), Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA-ZNZ) Waandishi wa Habari za Maendeleo Zanzibar (WAHAMAZA) Baraza la Habari Tanzania, Zanzibar (MCT, ZNZ) Jukwaa la Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania, Zanzibar (THRDC, ZNZ).


MWISHO.

Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...