Skip to main content

Mwezi mmoja matukio 106, ya Ukatili na Udhalilishaji Zanzibar, Magharabi ‘B’ yaongoza.

Na, Hassan Msellem, Pemba


Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali Zanzibar (OCGS) imetoa takwimu za matukio ya ukatili na udhalilishaji wa kijinsia Zanzibar katoka mwezi Agosti na Septemba 2025, ambapo jumla ya matukio 106 ya ukatili na udhalilishaji wa kijinsia yameripotiwa katika vituo mbali mbali vya Polisi huku Wilaya ya Magharib ‘B’ Unguja kwa kuwa jumla ya matukio 17 sawa na asilimia 16.0

Akitoa takwimu hizo kwa waandishi wa Habari, waratibu wa madawati ya jinsia na wadau wengine Oktoba 22.2025 huko Gombani Pemba Mkurugenzi wa Idara ya Takwimu za Kijamii kutoka Ofisi ya mtakwimu Mkuu Zanzibar Sabina Raphael Daima, amesema jumla ya matukio ya ukatili na udhalilishaji wa kijinsia 106 yameripotiwa mwezi Septemba 2025, ambapo waathirika wakubwa wakiwa ni watoto sawa asilimia 88.7 na wanawake wakiwa asilimia 11. 3

Aidha amesema kuwa miongoni mwa waathrika wa matukio hayo 94, wasichana 82 sawa asilimia 77.4 wavulana 12 sawa na asilimia 10.3

“Takwimu hizi zinaonesha matukio ya ukatili na udhalilishaji wa kijinsia Zanzibar bado ni mengi na wahanga wakubwa wakiwa ni wanawake na watoto hivyo tuna jukumu kubwa la kila mmoja kusimama kwenye nafasi yake kupambana na makosa haya” amesema Mkurugrenzi huyo kutoka OCGS

Akiwasilisha mada katika utoaji wa takwimu hizo Mtakwimu kutoka Ofisi ya mtakwimu mkuu wa Serikali, Kitengo cha Jinsia na Ajira Asha Mussa, amesema watoto wenye umri kati ya miaka 15 hadi 17 ndio wahanga wakubwa wa matukio ukatili na udhalilishaji sawa na asilimia 54.3 ya matukio yote.

Ameongeza kuwa jumla ya majalada 85 yamepokelewa katika Afisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka kwa mwezi Septembea ambapo wathumiwa wakuu wa wafanyaji wa matukio ya ukatili na udhalilishaji ni wapenzi matukio 38, watu wasiojuilikana matukio 28, majirani matukio 22, watu wengine matukio 17 na baba mdogo tukio moja

Kwa upande wake Mkuu wa Divisheni ya Tawkimu Jinsia na Ajira Fahima Mohammed Mussa, amewataka wadau hao kuandaa vipindi na mikakati itakayosaidia kupunguza idadi ya matukio hayo katika jamii.

Idadi ya matukio ya ukatili na udhalilishaji wa kijinsia kwa Wilaya zote za Unguja na Pemba kwa mwezi September 2025, ni kama ifuatavyo

WILAYA YA MATUKIO

Magharib ‘B’ 

Matukio 17

 Magharaib ‘A’ 

Matukio 16 

Kaskazini 'A' 

Tukio 1

 Kaskazini ‘B’

Matukio 13

Wilaya ya Kati

Matukio 15

Wilaya ya Kusini

Matukio 8

Wilaya ya Chake Chake

Matukio 9

Wilaya ya Mkoani

Matukio 6

Wilaya ya Wete

Matukio 5

Wilaya ya Micheweni

Matukio 2

Lengo la kuu la takwimu hizi za matukio ya ukatili na udhalilishaji wa kijinsia ni kutoa msaada kwa watunga Sera, waandishi wa habari na wanahakati ili Sera na kazi juu ya ukatili na udhalilishaji wa kijinsia zenye kuendana na hali halisi ya tatizo hilo.



Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...