Skip to main content

Ahukumiwa kwenda Chuo cha Mafunzo (JELA) miaka 106, kwa makosa 8 ya Udhalilishaji.

HASSAN MSELLEM, PEMBA

Abdalla Rashid Hassan (Mgunya) mwenye umri wa miaka 30 mkaazi wa Ziwani Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba amehukumiwa kwenda chuo cha mafunzo (JELA) kwa muda wa miaka 30 kwa Kutenda makosa nane ya udhalilishaji yakiwemo ya kutorosha, shambulio la aibu na kubaka.

MAKOSA MATANO YA KUTOROSHA

Mbele ya hakimu wa mahakama ya kupambana na makosa ya udhalilishaji Mkoa wa Kusini Pemba Chake Chake Taki Abdalla Habib imeelezwa na mwendesha mashtaka Othman Mzori kuwa tarehe 3\01\2025 saa 8:30 za mchana huko bonde la Mjananza Ziwani Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba mshtakiwa aliwachukua watoto watano wenye umri kati ya miaka 7, 9, 11, 12 na kuwapeleka maporini katika bonde la Sinanga Ziwani, jambo ambalo ni kosa kisheria kinyume na kifungu cha 113 kifungu kidogo cha kwanza (a) Sheria nambari 6 ya mwaka 2018 Sheria ya Zanzibar.

KOSA LA SITA

Shambulio la kawaida

Tarehe 3\01\2025 saa 9:25 za jioni huko Sininga Ziwani Wilaya ya Chakwe Chake Mkoa wa Kusini Pemba alimshambulia kwa kumpiga bakora sehemu mbali mbali za mwili wake watoto wakike mwenye umri wa miaka 11 kwa kumpiga sehemu mbali mbali za mwili wake jambo ambalo ni kosa kisheria kinyume na kifungu cha 229 cha Sheria nambari 6/2018 Sheria ya Zanzibar.

KOSA LA SABA

Shambulio la aibu 

Kinyume na kifungu 114 kifungu kidogo cha 1 Sheria nambari 6 ya mwaka 2018 Sheria ya Zanzibar, mnamo tarehe 3\01\2025 saa 9:30 za jioni huko bonde la Sininga Ziwani Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba bila ya halali na kwa njia ya aibu alimvua nguo mtoto wakike mwenye umri wa miaka 11 na kumshambulia kwa kumchezea sehemu ya kifuani na kumtia mikono katika sehemu yake ya siri ya mbele.

KATIKA KOSA LA NANE

Kubaka 

Kinyume na kifungu cha 108 kifungu kidogo cha 1 kifungu kidogo cha 2 kifungu kidogo cha i na kifungu cha 109 na kifungu kidogo cha 1 cha Sheria nambari 6.2018 Sheria ya Zanzibar, tarehe 3/01/2025 saa 9:35 za jioni katika bonde la Sininga Ziwani Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba alimbaka mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 12.

Kwa mara ya kwanza kesi hiyo ilisomwa 11/02/2025 na jumla ya mashahidi saba walitoa Ushahidi wao mahakamani hapo Ushahidi uliouwezesha mahakama kumtia hatiani na kuamuru kwenda chuo cha mafunzo kwa muda wa miaka 106 kwa makosa yote 8 adhabu hizo ziende sambamba hivyo atatakiwa kutumikia chuo cha mafunzo kwa muda wa miaka 30.

Ikumbukwe kuwa Oktoba 22.2025 mwandishi wa Habari hizi aliripoti taarifa ya Hakimu Said Hakimu mwenye umri wa miaka 36 mkaazi wa Jondeni Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba kuhukumiwa kutumikia chuo cha mafunzo miaka thelathini (30) kwa kosa la kumbaka mtoto wakike mwenye umri wa miaka 7 kwa mujibu wa hati ya mahakama ingawa wazazi wake walisema ana umri wa miaka nne.

Kwa mujibu wa Takwimu za matukio ya ukatili na udhalilishaji wa kijinsia zilizotolewa na Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali kwenye Ukumbi wa Wizara ya Fedha Gombani Pemba Oktoba 22.2025 zinaeleza jumla ya matukio 106 ya ukatili na udhalilishaji wa kijinsia yameripotiwa katika mwezi Septemba, 2025 ambapo waathirika wengi wakiwa ni watoto sawa asilimia 88.7 ni wanawake na 11.3 wanaume. Miongoni mwa waathirika watoto 94, wasichana wakiwa 82 sawa na asilimia 77.4 na wavulana ni 12 sawa na asilimia 10.3

Aidha takwimu hizo zimeeleza idadi ya matukio ya ubakaji kwa mwezi huo wa Septemba Zanzibar yalikuwa ni 57, waathirika 54 ni wasichana, kulawiti matukio 11, kuingilia kinyume na maumbile matukio 5, kutosha 15. Kuingilia maharimu 1 na kutoa mimba tukio moja (1).

Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...