Skip to main content

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA

Picha kutoka mtandaoni

Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba.

Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi.

Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio

Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazini kuja nyumbani kushuhudia tukio hilo

Daktari dhamana wa Hospitali ya Wilaya ya Micheweni Mkubwa Habib, amethibitisha kufikishwa mwili wa marehemu huyo hospitalini hapo na kuufanyia uchunguzi na kutoa wito kwa wazazi kuwa karibu na watoto wao ili kufahamu changamoto wanazopitia ili waweze kuzipatia ufumbuzi.

“Sasa hivi jamani kuna michezo mbali mbali kuna watu wanaigiza vitu vingi ambavyo vyengine ni vya hatari sana sasa kwa umri wa mtoto hawezi kupambanua kuwa yale ni maigizo, sasa wao wanayachukua yale kwenye Kichwa chake siku ikitokea kukerwa nae anafanya kama vile alivyoona kwenye TV” amesema 

Katika tukio la pili tarehe 9.10.2025 mwandishi Siajabu Abdalla aliripoti tukio la mtoto mwenye umri wa miaka mitano (5) mkaazi wa Kikwajuni Mjini Magharibi Unguja kufariki dunia kwa kujinyonga kwa kutumia kamba ya Kitambulisho.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Kamishna Msaidizi wa Polisi Abuubakar Khamis Ali, amesema tarehe 7.10.2025 saa 4:20 usiku huko Kikwajuni Gongoni mtoto mwenye umri wa miaka mitano aliyefahamikwa jina la ya Yassir Mohammed amekutwa ameshafariki dunia ndani ya chumba anacholala baada ya kujitundika kwenye msumari ulioko kwenye mlango wa chumba hicho kwa kutumia kamba ya Kitambulisho 

Aidha Kaimu Kamanda huyo amesema uchunguzi wa tukio hilo unaendelea ili kubaini chanzo na kutoa wito kwa wazazi na walezi kuwa waangalifu kwa watoto wao ili kufahamu matatizo yanayowakabili.

Hali hiyo imeibua hoja na maswali mazito ambayo majibu yake hayakuweza kupatikana kirahisi, hivyo Wananchi wanaziomba Mamlaka za Serikali kufanya utafiti ili kugundua chanzo hasa cha matukio hayo ni nini ili jinamizi hili lisiendelee kuwakaba koo Wananchi Visiwani humo.

Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...