Skip to main content

WANAWAKE WENYE ULEMAVU WAOMBA PUNGUZO LA FOMU ZA KUGOMBEA

Makala Na, Hassan Msellem 



Katika uzinduzi wa programu ya kuinua haki za watu wenye ulemavu ya CADir (Collective Action for Disability Rights) katika kutatua changamoto za watu wenye ulemavu, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imetaja hatua inayochukua katika kuimarisha ushiriki wao katika ngazi za uamuzi kutoka asilimia 2% hadi 5% ifikapo mwaka 20230.

Utambuzi wa watu wenye ulemavu katika azimio la Arusha la mwaka 1967, kuwa miongoni mwa makundi machache yanastahili usaidizi kutoka kila sekta ikiwemo jamii, elimu, ajira na Uongozi ili kuhuisha haki na ustawi wa watu wenye ulemavu nchini.

Wanawake wenye Ulemavu kupitia vyama mbali mbali vya siasa wameomba kupunguziwa kiasi cha kulipia fomu za kugombea nafasi za uongozi ili waweze kushiriki katika haki hiyo.

Wakizungumza na Pemba Post Blog kwa nyakati tofauti baadhi ya wanawake wenye ulemavu wamesema gharama za fomu za kugombea nafasi za kisiasa kama vile Uwakilishi, Ubunge na Uraisi ni kubwa hali inayochangia baadhi yao kushindwa kuhimili gharama hizo.

Mgombea wa Viti Maalum (UWT) kutoka Chama cha Mapinduzi CCM Bi. Awena Rashid, amesema kiasi cha shilingi laki tano kwa wanawake wa kawaida na wenye ulemavu ni kubwa sambamba na utaratibu wa kutakiwa kwenda Dodoma kujadiliwa kwa gharama zao binafsi hali inayowasabaishia usumbufu na mzigo wa gharama

“Kwakweli laki tano kwa mwananchi wa kawaida tena mwenye ulemavu ni kiasi kikubwa mno kwanini wasiweke kiasi ambacho kitakuwa nafuu kwa watu wote na haishii hapo tunatakiwa kwenda Dodoma katika mchakato wa kujadiliwa wakati tumetuma CV zetu ikizingatiwa ghamaza zote ni juu yetu” mgombea wa UWT Mkoa wa Kaskazini Pemba Bi. Awena Rashid 

Katija Mbarouk Ali mgombea wa nafasi ya Uwakilishi katika Jimbo la Kojani, amesema gharama ya fomu ya kugombea nafasi ya Uwakilishi kutoka shilingi laki moja mwaka 2020 hadi laki tano 2025 ni gharama kubwa ambayo imemlazimu kutumia nguvu za ziada kuihimili kiasi ambacho angeweza kukukitumia kwenye harakati nyengine za kimaisha

Katija ameongeza kuwa kiwango hicho kinanyima fursa kwa wanawake hasa wenye ulemavu kugombea nafasi mbali mbali za uongozi ambayo ni haki yao ya msingi 

“Uchaguzi wa mwaka 2020 fomu ilikuwa ni shilingi laki moja lakini lakini mwaka huu 2025 fomu ilikuwa shilingi laki tano mwanamke kama mimi mwenye ulemavu ambaye sina kazi maalumu ya kufanya napataje kiasi hicho” amesema

Makamo Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake Wenye Ulemavu Zanzibar (JUWAUZA) Hidaya Mjaka Ali, amesema kiasi hicho cha fedha za fomu zinachangia wanawake wengi hasa wenye ulemavu kushindwa kuhimili gharama hiyo hivyo ameviomba vyama vya siasa nchini kuwapunguzia watu wenye ulemavu gharama hizo ili waweze kushiriki siasa bila ya vikwazo.

Mwenyekiti wa Jumuiya watu wasiona Zanzibar Kisiwani Pemba (ZANAB) Mansour Nassor, amekiri kupokea kupokea kesi kadhaa kutoka kwa wanawake wenye ulemavu wa macho ambao wamelalamikia kukosa haki ya kugombea kutokana na ukosefu wa fedha za fomu na kampeni 

“Sio mara moja wa mbili kila uchaguzi napokea malalamiko kutoka kwa wanachama wangu hasa wanawake wanaotia nia ya kugombea nafasi za uongozi kuwa fedha ya fomu ni kubwa mno hawana uwezo nayo na hata wakijikusuru kupata pesa ya fomu hawana pesa za kufanyia kampeni” amesema Mwenyekiti huyo

Kamishna wa Chama cha ADC Kanda ya Pemba Mariam Mohammed Muhene, amesema chama cha ADC ni chama cha kwanza kinachozingatia makundi maalumu yakiwemo watu wenye Ulemavu ili nao waweze kupata haki yao ya kushiriki katika siasa na uongozi, hivyo amevitaka vyama vyengine vya kisiasa kulizingatia kundi hilo hasa wanawake 

Kamishna wa Chama cha ADC Kanda ya Pemba Bi. Mariam Mohammed Muhene 

Mkurugenzi wa Jumuiya ya Utetezi wa Kijinsia na Mazingira Pemba (PEGAO) Hafidh Abdi Said, amesema wakati umefika kwa vyama vya siasa kutambua mchango wa wanawake wenye ulemavu katika siasa na uongozi ili nao wawezekapata haki yao ya kuwa viongozi.

Amesema “mwanzo tulikuwa tunawasemea sana wanawake kwa ujumla lakini sasa kuna haja ya kuwasemea wanawake wenye ulemavu kwasababu Kundi hilo linahitaji uangalizi wa ziada ili kuhakikisha wanashiriki ipaswavyo katika mausala ya siasa na uongozi” 



Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...