Skip to main content

WANACHAMA 25 WA VIKUNDI VYA KUWEKA NA KUKOPA KUSINI UNGUJA WANOLEWA KIBIASHARA.

NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA 

Jumla ya wanachama 25 kutoka vikundi 16 vya kuweka na kukopa katika Wilaya ya Kusini Unguja wamepatiwa mafunzo ya siku mbili ya kuchagua, kupanga na kusimamia biashara, chini ya Programu ya Mashirikiano ya Pamoja kwa ajili ya Haki za Watu wenye Ulemavu (CADiR) inayotekelezwa na Chama cha waandishi wa Habari wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA ZNZ), Shirikisho la Jumuiya za Watu wenye Ulemavu Zanzibar (SHIJUWAZA) na Jumuiya ya wasioona Zanzibar (ZANAB) kwa ushirikiano mkubwa na Shirika la Watu Wenye Ulemavu la Norway (NAD).

Washiriki hao ambao 16 ni watu wenye ulemavu na 9 ni walezi na wasimamizi wa Watoto wenye ulemavu wamehudhuria mafunzo kama wawakilishi wa vikundi vyao, na wanatarajiwa kuyafikisha maarifa haya kwa wanachama wenzao, ili kila kikundi kinufaike kwa pamoja na kuimarisha biashara zake.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, Aziza Ismail ambae ni Mratibu wa program ya CADiR kutoka NAD, amesema taasisi zinazoshirikiana katika programu hii zina matumaini makubwa kuwa mafunzo haya yatawawezesha wawakilishi wa vikundi kupeleka elimu waliyoipata kwa wenzao, hatimaye kusaidia wanachama wote kuchagua biashara bora na zenye tija. 

“Kwa vile miongoni mwa malengo makuu ya program hii ni kuwawezesha watu wenye ulemavu kuinuka kiuchumi na kupata kipato rasmi, tunaamini mafunzo haya yatasaidia kikamilifu kulifikia lengo hili”, alisisitiza Mratibu huyo.

Mkufunzi wa mafunzo hayo, Muhidini Ramadhan kutoka TAMWA ZNZ amesema kuwa hali ya umasikini inaweza kupungua kwa watu wenye ulemavu iwapo wataelimishwa juu ya ujuzi na miradi ya kiuchumi yenye tija. 

Nae Meneja wa Programu kutoka TAMWA ZNZ Nairat Ali, amesema mafunzo haya ni muhimu kwa ajili ya kuwasaidia wanachama kupanga na kuchagua biashara zenye tija ili vikundi viwe endelevu na viweze kujitegemea kiuchumi.

Kwa upande wake ndugu Khamis Ali, Afisa Program kutoka ZANAB, amewataka washiriki wa mafunzo hayo kujifunza kwa umakini mafunzo hayo ili waweze kuchagua biashara sahihi zitakazowawezesha kupata mikopo na kuweza kurudisha kwa wakati.

Washiriki walijadili na kuandika mipango ya biashara, baadhi wakieleza ndoto zao za kukuza biashara ndogondogo walizonazo, ikiwemo kilimo, ufugaji, kufungua maduka na ushonaji.

Akizungumza kwa niaba ya washiriki wenzake, Yusra Ali Hassan ambaye ni Msaidizi Katibu wa kikundi cha Mtu ni Utu cha Kajengwa, ameshukuru waandaaji wa mafunzo hayo na kusema yamewapa muongozo mzuri wa namna ya kupanga biashara na kutumia vizuri fedha katika kukuza biashara zao. 

“Kupitia mafunzo haya tumejifunza kupanga matumizi kwa uangalifu na kuweka mipango thabiti ya biashara, binafsi nimeona namna biashara ya ushonaji inavyoweza kukua zaidi nikiwa na maarifa haya mapya,” amesema Yusra.

Mafunzo hayo ya siku mbili yamefanyika katika ukumbi wa walimu Kitogani ambayo ni sehemu ya utekelezaji wa program ya CADiR katika eneo la uwezeshaji kiuchumi ambalo linalenga kuanzisha na kuimarisha vikundi vya watu wenye ulemavu vya kuweka na kukopa katika wilaya 11 za Unguja na Pemba. 

Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...