NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA
Wananchi wa Jimbo la Mtambwe wakiwemo Walimu wa Skuli, Wanafunzi na Vijana, wamesema wanaridhishwa na kasi ya maendeleo inayofanywa na Mgombea wa nafasi ya Uwakilishi kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi CCM Mariam Ali Rashid, kwa kuwapatia misaada mbali mbali ikiwemo Sare, Rim Paper kwa Skuli 10 za Jimbo hilo.
Wakizungumza na Pemba Post Blog kwa nyakati tofauti wananchi hao wamesema moyo wa kujitoa kwa Mgombea huyo kumesaidia kutatua baadhi ya changamoto za ukosefu wa na rim paper hali iliyosaidia kuondokana na changamoto hizo.
“Ni kweli baadhi ya wanafunzi walikuwa hawana sare lakini Bi. Mariam alikuja kuwapatia sare wanafunzi hao na sasa wanaendelea na masomo vizuri tunamshukuru sana” Mwalimu Mkuu Skuli ya Mleteni Hadija Ali Hamad
Nae Mtakwimu wa Skuli hiyo Bishara Mbarouk Hamad, alisema Bi. Mariam ni Mgombea wa kwanza kutoa msaada tangu kuanzishwa kwa Skuli hiyo mwaka 2023
“kwakweli Bi. Mariam ni mgombea wa kwanza kabisa kutupa msaada katika skuli yetu tangu ilipoanzishwa mwaka 2020 kwahivyo anaonesha mwanzo nzuri kabla hajapata nafasi ya kuwa mwakilishi, hivyo basi ni Imani yetu kuwa akipata ridhaa ya kuwa muakilishi atatufanyia makubwa zaidi” alisema
Mwalimu Mkuu wa Skuli za Kijumbani Kisiwani Hamad Khamis Hamad, alisema walikuwa wanakabilishwa na changamoto ya rim paper hasa kipindi cha mitihani ya muhula lakini kupatiwa msaada huo wa rim paper kumetatua changamoto hiyo.
Kwa upande wake Mwalimu Mkuu Sekisheni Skuli ya Piki Tauhida Mohammed Hemed, amewaomba wananchi na wanachama wa CCM wa Jimbo la Mtambwe kumchagua Bi. Mariam kutokana na moyo wake wa kujitoa na Uzalendo ili kanufaika na mazuri aliyoyapanga kwa wananchi wa Jimbo hilo
“Mimi ni wasihi tu wananchi wa Jimbo la Mtambwe hasa wanachama wa CCM, kumpa ridhaa Bi. Mariam kuongoza Jimbo hili kwasababu Bi. Mariam ana moyo wa kujitoa na uzalendo kama bado hajapata ridhaa na ameanza kutuonesha mfano nzuri wa kuwasaidia wananchi katika sekta ya elimu je, akipata ridhaa” alisema
Nao wananchi wa Jimbo hilo walisema wanamfahamu Bi. Mariam kama kijana mwenzao mwenye maono na ubunifu katika uongozi na kuahidi kumchagua ili aendeleze juhudi zake za kuwaletea maendeleo.
“Yani ameanza vizuri sana sana kwasababu bado hajawa muakilishi anaanza kuwasaidia wananchi kiasi hichi Imani yetu akipata nafasi wananchi wa Jimbo Mtambwe tutanufaika sana katika Nyanja mbali mbali” Time Shaaban Seif Mkaazi wa Kisiwani
"Kwakweli Vijana tumeridhika sana kuona kijana mwenzetu shupavu amepewa ridhaa na chama kwenda Barazani kuwakilisha Jimbo letu la Mtambwe pamoja na kutuwakilisha Vijana wenzake kwakweli tunamkubali tunaimani nae tunampenda na tunamuahidi kumchagua kwa kura nyingi sana na tunaamini atashinda kwa kishindo” Mahfudh Sudi Seif Dereva Bodaboda Mzambarauni











Comments
Post a Comment