Skip to main content

UBALOZI WA NORWAY TANZANIA, WAKUTANA NA WADAU WA MRADI WA ‘SWIL’ PEMBA.

NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA

Ubalozi wa Norway Nchini Tanzania umekutana na wadau mbali mbali Kisiwani Pemba wakiwemo Viongozi wa Jumuiya zisizo za Kiserikali (NGOs), Wahamasishaji wajamii(CBs) Waandishi wa Habari pamoja na Wagombea Wanawake kutoka vyama vya Siasa kujadili Mafanikio yanayotokana na Mradi wa Uhamasishaji Wanawake kushiriki katika nafasi za Uongozi, Strength Women In Leadership (SWIL).

Akizungumza na wadau hao huko katika Ofisi za TAMWA Mkanjuni Pemba Balozi Norway Tanzania Tonnis Tinnes, amesema ripoti zinaonesha mradi huo umewawesha wanawake zaidi ya elfu mbili kupata elimu na hamasa ya kushiriki katika vyama vya siasa na uongozi kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025.

Aidha Balozi Tonnis huyo amesema Ubalozi Norway Tanzania utaendelea kushirikiana na wadau hao katika kukuza na kuongeza ushiriki wa Wanawake katika Siasa na Uongozi.

Mshauri Mkuu wa Masuala ya Jinsia Anette Otilie kutoka Norway, amesema Ushiriki wa Wanawake katika Siasa, Uongozi na Demokrasia kusaidia katika kwa kiasi kikubwa kukuza usawa wa kijinsia kuanzia ngazi ya jamii na Taifa kwa ujumla.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA) upande wa Zanzibar Mzuri Issa, amesema mradi wa SWIL umeleta mwanga wa mabadiliko chanya Visiwani Zanzibar katika dhana ya Wanawake na Uongozi kutokana hali iliyosaidia kuongeza idadi ya wanawake kuongezeka maradufu katika Shughuli za Kisiasa na Maendeleo.

Nae Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Pemba (PPC) Bakari Mussa, amawashukuru waendashaji wa mradi huo kutokana na mafunzo mbali mbali waliowapatia juu ya Uwezeshaji wa Wanawake katika Sias ana Uongozi sambamba na kuwapa tunzo waandishi waliofanya vizuri katika mradi huo.

“Na sasa hivi sisi watu wa Habari niseme tumefaidika kwasababu waandishi wengi kisiwani Pemba wana uwezo nzuri wa kuandika Habari za wanawake zenye kuleta tija kwao na kwa taifa kwa ujumla” Mwenyekiti PPC, Bakari Mussa

Nao Wahamasishaji Jamii (Citizen Brigade) na Wanaume wa Mabadiliko (Male Change Agent) wameupongeza Ubalozi wa Norway Tanzania na Tamwa, Zanzibar kwa jitihada zao za kuelimisha jamii juu haki za Wanawake ikiwemo kushiriki katika Demokrasia na Uongozi elimu ambayo imechangia idadi ya wanawake waliogombania nafasi mbali mbali za uongozi kuelekea Uchaguzi wa 2025 kuongezeka maradufu.

“Niwapongeze kwa mradi huu ule mwaka 2019 haikuwa rahisi katika Visiwa hivi vya Unguja na Pemba kuwaambia mwanamke kushiriki katika uongozi sio kazi rahisi, lakini tunaona leo TAMWA wametoa Kitabu hichi kinachoelezea wanawake kushiriki katika na Uongozi na wakatoa na muongozo wa Viongozi wa dini kuhusu uchaguzi na laiti fomu ya Urais isingekuwa laki tano wanawake wote wangegombea” Omar Mjaka Ali, mwanamme wa mabadiliko kutoka Kilindi

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tumaini Jipya Pemba (TUJIPE) Tatu Abdalla Msellem, amesema Taasisi ya TUJIPE imenufaika kwa kikubwa kupitia mradi wa SWIL kwa kutoa elimu ya Uongozi kwa Viongozi na watendaji wa Taasisi hiyo pamoja na kuwaomba wadau hao kuendelea kushirikiana na taasisi hiyo katika kuendeleza mradi huo.

“Binafsi niseme TUJIPE tumefarajika sana katika awamu zote mbili za mradi huu wa SWIL awamu ya kwanza tulishirikishwa kikamilifu kama NGOs tukawa tunashiriki katika kazi mbali mbali ikiwemo kutoa elimu katika jamii ambapo kuna wadau wengi tuliwafikia wengi wao wakiwa ni wanawake” alifafanua

Wakitoa neno la shukurani kwa waendeshaji wa mradi wa SWIL wagombea Wanawake kutoka vyama mbali mbali vya Siasa, wamesema elimu na hamasa walizopata kutoka kwa wadau wa mradi huo ndio nguvu pekee iliyowawezesha kujiamini na kuwa na uthubutu wa kugombania nafasi mbali mbali ikiwemo Urais, Ubunge, Uwakishi na Udiwani.

“Mimi ni Mgombea wa chama cha Ukombozi wa Umma CHAUMA nimeshikwa mkono na TAMWA, PEGAO NA ZAFELA kusema kweli tumepata mafunzo mazuri nilikuwa siwezi kusimama nikasema chochote lakini sasa naweza kusema popote nikasema chochote lakini sasa naweza, kwa maana hiyo elimu na hamasa iliyotolewa na jumuiya hizi ni kubwa mno” Mariam Saleh Juma kutoka Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMA) 


Mradi wa Uhamasishaji Wanawake kushiriki katika nafasi za Uongozi, Strength Women In Leadership (SWIL) Zanzibar, ulianzishwa mwaka 2020 unatekelezwa na TAMWA, ZANZIBAR, Chama cha Wanasheria Zanzibar (ZAFELA) Jumuiya ya Utetezi wa Kijinsi na Mazingira Pemba (PEGAO) kwa ufadhili wa Ubalozi wa Norway Tanzania.

Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...