Skip to main content

“TAMWA NA PEGAO” WAWAPIGA PASI WAGOMBEA 35 “WANAWAKE” WA UBUNGE, UWAKILISHI NA UDIWANI-UCHAGUZI 2025.

NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA

Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA) upande wa Zanzibar na Jumuiya Utetezi wa Kijinsia na Mazingira Pemba (PEGAO) zimetoa mafunzo ya siku tatu kwa wagombea 37 wanawake kutoka vyama vya Siasa 17 katika nafasi ya Ubunge, Uwakilishi na Udiwani ili waweze kufanya vizuri katika kampeni kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2025.

Akiwasilisha mada ya Kuwajengea uwezo Wagombea Wanawake watakaosimama katika Majimbo ya Uchaguzi Mkuu 2025, huko katika Ukumbi wa Tamwa Mkanjuni Pemba Muezeshaji Bi. Sabahi Mussa Said, amewataka wagombea hao kuishi na agenda na kuzifanyia kazi na kuzijengea uwelewa zaidi ili ziweze kuwafaa wakati wa kampeni.

Aidha amewasihi kuzifahamu Sera mbali mbali na Sheria muhimu kwa mustakbali wa jamii, Wanawake na Taifa kwa Ujumla.

“Wewe ni mwakilishi wa jamii na wananchi hakikisha unazitambua changamoto za jamii na Jimbo lako ili katika ajenda zako uweze kuzipa kipaumbele hapo ndipo wananchi utawagusa na watahamasika na wewe sio changamoto za jamii au Jimbo lako ni Barabara na Kituo cha Afya wewe unaenda kuzungumzia Maji na Skuli Wananchi hawatakuelewa” Bi. Sabahi Mussa Said

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Jumuiya Utetezi wa Kijinsia Pemba (PEGAO) Hafidh Abdi, amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo wa kujiamini na kujenga hoja wakati wanaponadi Sera zao kwa Wananchi.

Aidha amewataka wagombea hao kuzifahamu Sera na ilani za vyama vyao ili waweze kuandaa ajenda zinazoendana na malengo ya vyama vyao.

“Lengo la mafunzo haya ni kuwajengea uwezo ili muweze kusimama na kujenga hoja kwa wananchi lakini pia kila Chama kina Sera yake rudini katika vyama vyenu muzisome Sera zenu ili muweze kuziwasilisha Sera za vyama vyenu ipaswavyo” Mkurugenzi PEGAO Abdi Said 

Mratibu wa PEGAO Bi. Dina Juma Mkota, amewasisitiza wagombea hao kuyafikia makundi yote ikiwemo Watu Wenye Ulemavu na wanaume wa rika la kati ili kupata idadi kubwa ya watu watakaoweza kuwaunga mkono

“Makundi ya Watu Wenye Ulemavu na akina baba yanatengwa linatengwa kwahivyo wanasihi sana munapokwenda kunadi Sera zenu yafikieni makundi yote musibague kwasababu wote wana haki ya kufikiwa na kusikiliza sera zenu” Mratibu wa PEGAO 

Nao baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wamezishukuru taasisi ya Tamwa, Zanzibar na PEGAO kwa kuwapatia mafunzo hayo na kuahidi kuyafanyia kazi ipaswavyo ili kufikia lengo la kuongeza idadi ya wanawake kwenye vyombo vya kutunga Sheria.

“Kwakweli tuemdelee kuzishukuru taasisi ya TAMWA na PEGAO kwa kuendelea kutushika mkono Wanawake kwenye masuala ya Uongozi kwani wao ndio wamechangia kwa kiasi kikubwa hadi leo zaidi ya akina mama ishiriki kutoka vyama mbali mbali vya siasa tupo hapa kwenye mafunzo ya siku tatu tukiwa tumepata ridhaa ya kuviwakilisha vyama vyetu katika nafasi mbali mbali kama vile Ubunge, Uwakilishi na Udiwani hakika haya ni mafanikio makubwa sana kwetu wanawake na Taifa kwa ujumla kwasababu mwanawake ni kiongozi bora na imara sana” Mgombea wa Chama cha ADA TADEA Asha Said Suleiman 

Mafunzo hayo ya siku tatu kwa Wagombea Wanawake kutoka vyama 20 vya siasa nchini yameandaliwa na taasisi ya Tamwa, Zanzibar na Jumuiya ya Utetezi wa Kijinsi na Mazingira Pemba (PEGAO) kwa ufadhili wa Ubalozi wa Norway Tanzania ikiwa ni muendelezo wa kuwajengea uwezo Wanawake katika kushiriki katika Siasa, Uongozi pamoja na kukuza Demokrasia.



Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...