Skip to main content

Posts

Showing posts from September, 2025

UBALOZI WA NORWAY TANZANIA, WAKUTANA NA WADAU WA MRADI WA ‘SWIL’ PEMBA.

NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Ubalozi wa Norway Nchini Tanzania umekutana na wadau mbali mbali Kisiwani Pemba wakiwemo Viongozi wa Jumuiya zisizo za Kiserikali (NGOs), Wahamasishaji wajamii(CBs) Waandishi wa Habari pamoja na Wagombea Wanawake kutoka vyama vya Siasa kujadili Mafanikio yanayotokana na Mradi wa Uhamasishaji Wanawake kushiriki katika nafasi za Uongozi, Strength Women In Leadership (SWIL). Akizungumza na wadau hao huko katika Ofisi za TAMWA Mkanjuni Pemba Balozi Norway Tanzania Tonnis Tinnes, amesema ripoti zinaonesha mradi huo umewawesha wanawake zaidi ya elfu mbili kupata elimu na hamasa ya kushiriki katika vyama vya siasa na uongozi kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025. Aidha Balozi Tonnis huyo amesema Ubalozi Norway Tanzania utaendelea kushirikiana na wadau hao katika kukuza na kuongeza ushiriki wa Wanawake katika Siasa na Uongozi. Mshauri Mkuu wa Masuala ya Jinsia Anette Otilie kutoka Norway, amesema Ushiriki wa Wanawake katika Siasa, Uongozi na Demokrasia kusaidia katika kwa kiasi...

WANACHAMA 25 WA VIKUNDI VYA KUWEKA NA KUKOPA KUSINI UNGUJA WANOLEWA KIBIASHARA.

NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA  Jumla ya wanachama 25 kutoka vikundi 16 vya kuweka na kukopa katika Wilaya ya Kusini Unguja wamepatiwa mafunzo ya siku mbili ya kuchagua, kupanga na kusimamia biashara, chini ya Programu ya Mashirikiano ya Pamoja kwa ajili ya Haki za Watu wenye Ulemavu (CADiR) inayotekelezwa na Chama cha waandishi wa Habari wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA ZNZ), Shirikisho la Jumuiya za Watu wenye Ulemavu Zanzibar (SHIJUWAZA) na Jumuiya ya wasioona Zanzibar (ZANAB) kwa ushirikiano mkubwa na Shirika la Watu Wenye Ulemavu la Norway (NAD). Washiriki hao ambao 16 ni watu wenye ulemavu na 9 ni walezi na wasimamizi wa Watoto wenye ulemavu wamehudhuria mafunzo kama wawakilishi wa vikundi vyao, na wanatarajiwa kuyafikisha maarifa haya kwa wanachama wenzao, ili kila kikundi kinufaike kwa pamoja na kuimarisha biashara zake. Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, Aziza Ismail ambae ni Mratibu wa program ya CADiR kutoka NAD, amesema taasisi zinazoshirikiana katika programu...

WALIMU, VIJANA NA WANANCHI WARIDHISHWA NA MGOMBEA UWAKILISHI WA JIMBO LA MTAMBWE-MARIAM ALI RASHID

NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA  Wananchi wa Jimbo la Mtambwe wakiwemo Walimu wa Skuli, Wanafunzi na Vijana, wamesema wanaridhishwa na kasi ya maendeleo inayofanywa na Mgombea wa nafasi ya Uwakilishi kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi CCM Mariam Ali Rashid, kwa kuwapatia misaada mbali mbali ikiwemo Sare, Rim Paper kwa Skuli 10 za Jimbo hilo. Wakizungumza na Pemba Post Blog kwa nyakati tofauti wananchi hao wamesema moyo wa kujitoa kwa Mgombea huyo kumesaidia kutatua baadhi ya changamoto za ukosefu wa na rim paper hali iliyosaidia kuondokana na changamoto hizo. Mgombea wa Uwakilishi Jimbo la Mtambwe kwa tiketi ya CCM Bi. Mariam Ali Rashid  “Ni kweli baadhi ya wanafunzi walikuwa hawana sare lakini Bi. Mariam alikuja kuwapatia sare wanafunzi hao na sasa wanaendelea na masomo vizuri tunamshukuru sana” Mwalimu Mkuu Skuli ya Mleteni Hadija Ali Hamad Mwalimu Mkuu wa Skuli ya Mleteni, Hadija Ali Hamad Nae Mtakwimu wa Skuli hiyo Bishara Mbarouk Hamad, alisema Bi. Mariam ni Mgombea wa kwanza ku...

WILAYA YA MKOANI YAFANYA KONGAMANO LA "AMANI" KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2025.

NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Mkuu wa Wilaya ya Mkoani Miza Hassan Faki, akimkabidhi Nishani Makamo wa Pili wa Rais Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla Viongozi wa vyama vya Siasa wametakiwa kutotumia hotuba zinazochochea Ubaguzi, Chuki na Uhasama katika kampeni zinazotarajiwa kufanyika hivi punde Visiwani Zanzibar ili kuepukana na uvunjifu wa amani. Akifungua Kongamano lililoandaliwa na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Mkoani huko katika Ukumbi wa Umoja ni Nguvu Mkoani, Makamo wa Pili wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla, amesema lengo la Kampeni za Kisiasa ni wagombea kunadai sera na ilani za vyama vyao kwa wananchi ili waweze kuwachagua na sio kutoa hotuba za Ubaguzi, Chuki na Uhasama hali inayoweza kusababisha uvunjifu wa amani nchini. Aidha Mhe. Hemed amewasihi Vijana kutokutumiwa vibaya na wasiasa kwa kisingizio cha Uchaguzi kwani wao ndio wahanga wakubwa vitendo vya uvunjifu wa amani katika kipindi cha Uchaguzi. “Niwaombe sana viongozi wa vyama vya siasa na wagom...

“TAMWA NA PEGAO” WAWAPIGA PASI WAGOMBEA 35 “WANAWAKE” WA UBUNGE, UWAKILISHI NA UDIWANI-UCHAGUZI 2025.

NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA) upande wa Zanzibar na Jumuiya Utetezi wa Kijinsia na Mazingira Pemba (PEGAO) zimetoa mafunzo ya siku tatu kwa wagombea 37 wanawake kutoka vyama vya Siasa 17 katika nafasi ya Ubunge, Uwakilishi na Udiwani ili waweze kufanya vizuri katika kampeni kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2025. Akiwasilisha mada ya Kuwajengea uwezo Wagombea Wanawake watakaosimama katika Majimbo ya Uchaguzi Mkuu 2025, huko katika Ukumbi wa Tamwa Mkanjuni Pemba Muezeshaji Bi. Sabahi Mussa Said, amewataka wagombea hao kuishi na agenda na kuzifanyia kazi na kuzijengea uwelewa zaidi ili ziweze kuwafaa wakati wa kampeni. Aidha amewasihi kuzifahamu Sera mbali mbali na Sheria muhimu kwa mustakbali wa jamii, Wanawake na Taifa kwa Ujumla. “Wewe ni mwakilishi wa jamii na wananchi hakikisha unazitambua changamoto za jamii na Jimbo lako ili katika ajenda zako uweze kuzipa kipaumbele hapo ndipo wananchi utawagusa na watahamasika na wewe sio changamoto za...