Skip to main content

WANAWAKE WAHIMIZWA KUTUMIA VYOMBO VYA HABARI KUTANGAZA KAZI ZAO

 NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA


Meneja miradi kutoka Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA ZNZ) Nairat Abdulla amewaomba wanawake kutumia vyombo vya habari kwa lengo la kutangaza kazi zao wanazozifanya.

Akifungua mafunzo ya siku mbili ya kuwajengea uwezo wakulima viongozi kutoka shehia nne (4) za Unguja, juu ya umuhimu wa kutumia vyombo vya habari, yaliofanyika ofisi za TAMWA-ZNZ Tunguu, Mkoa wa Kusini Unguja, amesema wanawake wanajishughulisha na harakati mbalimbali zikiwemo za uzalishaji pamoja na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi lakini bado sauti zao hazisikiki ipasavyo kupitia vyombo vya habari.

Hivyo amewaomba wanawake hao kutumia vyombo vya habari hasa mitandao ya kijamii, kuelezea mafanikio na changamoto zinazowakabili katika kupambana na mabadiliko ya tabianchi ili kufikisha ujumbe kwa wahusika na hatimae kupatiwa ufumbuzi.

Akiwasilisha mada inayohusu vyombo vya habari, Meneja Mawasiliano kutoka TAMWA ZNZ, Sofia Ngalapi amesema wanawake wakulima viongozi wanafanya kazi nzuri ya kutunza mazingira na kukabiliana na mbadiliko ya tabianchi, hivyo wapaze sauti kutangaza kazi wanazozifanya kupitia vyombo vya habari kwa lengo la kuhamasisha jamii kuwa vinara kupitia masuala ya mabadiliko ya tabianchi.

Khairat Haji, Afisa mawasiliano kutoka TAMWA ZNZ akiwasilisha mada inayohusu mitandao ya kijamii, amesema mitandao ya kijamii ni njia moja wapo ya kujitangaza endapo itatumika ipasavyo hasa katika dunia hii ya sayansi na teknolojia.

Aidha amesema ili kuepuka udhalilishaji kupitia mitandao ya kijamii, ni vyema kuepuka kuchapisha taarifa na picha zinazohusu maisha yao binafsi kwa kulinda usalama wao na badala yake kuitumia kama njia moja ya kujiongezea kipato.

Nao wakulima viongozi kutoka shehia nne (4) za Unguja, Mkoa wa Kusini, ambazo ni Bungi, Unguja Ukuu, Uzi na Ng’ambwa wamesema wamefarajika kupata mafunzo hayo kupitia program ya Zanzadapt na wameahidi kuwa mabalozi wazuri kwa kufikisha ujumbe kwa jamii.

Mradi unaohusu nafasi ya mwanamke kiongozi katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, (Zanzadapt) umejikita kuangalia maeneo manne yakiwemo uhifadhi wa mikoko, kilimo mseto, wanawake viongozi na masuala ya jinsia ambao unatekelezwa kwa pamoja na TAMWA ZNZ, Jumuiya ya misitu Pemba (CFP), Jumuiya ya misitu Kimataifa (CFI) kwa kushirikiana na Ubalozi wa Canada.



MWISHO

Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...