Skip to main content

VYAMA VYA SIASA VYAPEWA KIBARUA, KUWATEUA WANAWAKE UCHAGUZI MKUU 2025.


Wadau wa masuala ya wanawake na uongozi wamevitaka vyama vya siasa nchini kuhakikisha vinawateua wanawake waliokidhi vigezo kugombea nafasi za uongozi katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 2025, hususan kwenye nafasi za uwakilishi, ubunge na udiwani zinazoshindaniwa majimboni.

Wakizungumza katika taarifa yao kwa vyombo vya habari, wadau hao wameeleza kuwa kwa muda mrefu wanawake wamekuwa wakipewa nafasi za viti maalum pekee, hatua inayowanyima nafasi ya kushindana moja kwa moja na wanaume na kuonesha uwezo wao katika siasa za ushindani.

Katika kipindi hiki cha mchakato wa chaguzi za ndani ya vyama kuelekea uchaguzi mkuu, wanawake wengi wamejitokeza kuchukua fomu, licha ya kuwa idadi yao bado ni ndogo kulinganisha na wanaume.

Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuhusu Zanzibar, wanachama 1,640 wamechukua na kurejesha fomu za kugombea Ubunge, Uwakilishi na Udiwani, ambapo kati yao wanawake ni 406, sawa na asilimia 24.7.

Chama cha ACT Wazalendo kwa upande wake kimeripoti kuwa kati ya wanachama 435 waliotangaza nia ya kugombea nafasi hizo visiwani humo, wanawake ni 40 pekee, sawa na asilimia 9.2.

Vyama hivyo vinasubiri vikao vya Kamati Kuu na Kamati Maalum kupitisha rasmi majina ya wagombea, mchakato unaotarajiwa kukamilika mwishoni mwa Julai hadi Agosti 2025.

Wadau wametoa pongezi kwa wanawake hao kwa ujasiri wa kujitokeza lakini wakasisitiza kuwa hatua hiyo haitoshi iwapo hawatapewa nafasi halisi ya kugombea majimboni.

Katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2020, Zanzibar ilifanikiwa kupata wanawake wanane pekee (sawa na asilimia 16) katika Baraza la Wawakilishi na wabunge wanne (asilimia 8), kupitia siasa za ushindani.

“Tunaomba wajumbe wa vikao vya uteuzi kwenye vyama mbalimbali kuwapigia kura wanawake wakati wa mchakato wa kuwapata wagombea wa mwisho. Huu ni wakati wa kufanya mabadiliko halisi ya kisiasa na kijamii kwa kuzingatia usawa wa kijinsia,” imesema sehemu ya taarifa hiyo" walisema

Wadau wamesisitiza kuwa uwepo wa wanawake kwenye nafasi za juu za uongozi ni chachu ya maendeleo ya taifa, kwani tafiti mbalimbali zinaonesha kuwa wanawake ni viongozi waadilifu, wanaoweka mbele maslahi ya familia na jamii, na ni wasikivu na wenye kujitoa.

Wakirejea Mkataba wa Kimataifa wa Kuondoa Aina Zote za Ubaguzi Dhidi ya Wanawake (CEDAW) wa mwaka 1979, wadau hao wamekumbusha wajibu wa Tanzania kama nchi mwanachama kuhakikisha inachukua hatua za kuongeza ushiriki wa wanawake katika vyombo vya maamuzi.

Taarifa hiyo imetolewa kwa ushirikiano wa taasisi kadhaa za wanawake zikiwemo Jumuiya ya Wanawake wenye Ulemavu Zanzibar (JUWAUZA), Jumuiya ya Wanasheria Wanawake Zanzibar (ZAFELA), Jumuiya ya Mazingira, Jinsia na Utetezi Pemba (PEGAO) na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania – Zanzibar (TAMWA ZNZ), kwa kushirikiana na Ubalozi wa Norway.

Wamewatia moyo wanawake waliotia nia wasikate tamaa bali waendelee kuwa imara na waaminifu kwa dhamira ya uongozi kwa maslahi ya jamii na taifa kwa ujumla.


Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...