Wanafunzi Kisiwani Pemba wamehimizwa kushirikiana ili kufanya vizuri kwenye masomo sambamba na kutimiza ndoto walizojiwekea
Akizungumza na wanafunzi
wa Sekondari wa Klabu za Vijana wa Umoja wa Mataifa Upande wa Zanzibar (YUNA CLUB)
huko Skuli ya Sekondari Mkoani Pemba katika maadhimisho ya siku ya wanawake
duniani kwa niaba ya Jaji mkaazi wa mahakama Kuu Pemba mratibu wa mahakama ya
ardhi Pemba Abdalla Omar shamuhuni, amesema katika mkataba wa kimaitafa wa haki
za binadamu, Katiba za nchi na sheria mbali mbali zinapiga vita suala ubaguzi
hivyo wanafunzi wanapaswa kushirikiana ili kufikia malengo la kuanzishwa kwa
klabu hizo
“Nawasihi sana muwe na mashirikiano popote mulipo mshirikiane na musitengane na msibaguane, kwenye haki za binadamu suala la ubaguzi kuanzia kwenye Katiba zetu na kwenye sheria za kimataifa suala la ubaguzi limekatazwa, kinyume cha kuacha ubaguzi ni kushirikiana na kupendana kwa wema” alisema
Nae Afisa Elimu Wilaya Mohammed Abdalla Omar amesema sera ya elimu Zanzibar imetoa fursa sawa kwa wananfuzi wote ili waweze kupata haki yao ya msingi ya elimu
“Tukizungumzia usawa kwasasa
hakuna jinsia ambayo inabaguliwa na kuachwa nyuma kwenye sekta zote ikiwemo sekta
ya elimu kuanzia ngazi ya maandalizi, msingi hadi sekondari watu wote wanapata
elimu sawa, imefika pahala mpaka Serikali imeunda wizara maalumu inayosimamia
mambo yanayowahusu Wanawake na Watoto wakike ili waweze kupatiwa haki zao zote
za msingi” afisa elimu Wilaya ya Mkoani Pemba
Mohammed Hassan Ali ni
Naibu Mkurugenzi wa Klabu za Vijana Umoja wa Mataifa Upande wa Zanzibar (YUNA
CLUB) amesema lengo la kuanzishwa kwa klabu hiyo ni kutoa fursa za maendeleo
kwa vijana pindi wanapokuwa masheleni na baada ya kumaliza
Aliongeza” lengo letu
nikiwaonesha vijana fursa pindi wanapokuwa mashuleni na hata baada ya kumaliza masomo
ili kusudi waweze kuwa wabunifu na kuweza kujitegemea wenyewe”
Kwa upande wake mlezi wa Klabu ya YUNA Skuli ya Uwelini Suleiman Saleh Mohammed, amesema lengo la kuadhimisha siku ya wanawake duniani ni kutoa elimu juu ya umuhimu wa usawa wa kijinsia katika nyanja mbali mbali ikiwemo fursa za uongozi
“Leo tumeadhimisha siku ya Wanawake duniani ambayo kitaifa inaadhimishwa tarahe 8 mwezi March kila mwaka, kwahivyo na sisi kama YUNA CLUB tumeamua kuadhimisha siku hii ya Wanawake ili kukumbushana mambo yanayowahusu Wanawake na Wasicha kama vile kunyimwa, fursa haki zao” mlezi wa Klabu ya YUNA Skuli ya Uwelini Suleiman Saleh Mohammed
Nao baadhi ya wanafunzi
walioshiri katika maadhisho hayo ya siku ya Wanawake duniani walisema
wamejifunza kuwepo kwa usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa Wanawake Nchini
Raya ni mwanafunzi wa Kidato cha sita Skuli ya Sekondari Uweleni alisema “Nichojifunza haswa nikuona kwamba usawa na uwezashaji wa haki za Wanawake upatikana nchini mzima na duniani mzima kwa ujumla”
"Wanawake kwanza tupaswa tushirikiane kwamba tukishirikiana tutaweza kujipatia maendeleo kwenye maisha yetu” Mwajuma Khamis Haji mwanafunzi wa kidato cha tano skuli ya Kiwani Sekondari
Hidaya Salum Mohammed mwanafunzi wa kidato cha tano Skuli ya Sekondari Shamiani alisema “miongoni mwa changamoto zinazowakabili wanawake na wasichana ni udhalilishaji wa kijinsia pamoja na unyanyapaji hali inayochangia kujiona dhaifu na kutokutumiza ndoto zao walizojiwekea”
Katika maadhimisho hayo ya siku ya Wanawake duniani ambayo huadhimishwa kila ifikapo tarehe8 mwezi March kila mwaka yenye kauli mbiu inayosema WANAWAKE NA WASICHANA 2025 TUIMARISHE HAKI, USAWA NA UWEZESHAJI’ maonesho mbali mbali yalifanyika ikiwemo mchezo wa kuigiza, matumizi wa lugha za kigeni pamoja na maswali na majibu juu ya mambo mbali mbali ya kitaifa na kimataifa.
















Comments
Post a Comment