Na Amina Mchezo
Uhamasishaji michezoni unatokana na uwepo wa watu maalum ambao hutumia muda wao mwingi kutafakari namna gani ya kuwaleta watu karibu na Kwa mbinu gani.
Michezo kikawaida huhitaji mvuto mkubwa Kwa jamii kwani uwepo wake huleta furaha na kujuana na watu mbalimbali.
Maafisa habari kwenye michezo wananafasi kubwa ya kutoa taarifa zinazohusu vilabu na wanachama wengine.
Inaelezwa kuwa ili upatiwa leseni ya timu yako na shirikisho la mpira wa miguu ni lazima uwe umetimiza vgezo ikiwemo kipengele Cha kuwa na afisa habari wa timu.
Huku cha kusikitisha zaidi ni Kuona timu ambazo zinategemewa kibeba Zanzibar hata hawaoni umuhimu. kuwa na afisa habari.
Hadi Sasa maafisa wa habari wanawake katika michezo ni wawili tu Kwa Zanzibar huku Timu Zote 16 znazoshiriki ligi kuu Zanzibar hakuna timu yenye msemaji mwanamke, wakati ligi daraja la kwanza Kanda ya unguja timu Moja tu kati ya timu 18 ndio yenye msemaji mwanamke na timu Moja tu ilio mkoa ndio yenye msemaji mwanamke.
Hali hii si Kwa wanawake wenyewe Bali hata wadau mbalimbali wa michezo wanaona ni khatari katika kuupoteza ushiriki wa wanawake michezoni.
Nd. Ali Khamis na nd. Mtumwa Mzee ni wadau wa michezo Zanzibar wamekuwa wakifuatilia Kwa karibu sana maafisa wa habari wanawake walio nje ya Zanzibar na kufanya vizuri kwenye vilabu vyao katika kuleta hamasa za michezo.
"Dunia Kwa Sasa inamuhitaji mwanamke katika Kila nyanja hivyo wanawake kwenye michezo wanaongeza mvuto Kwa wanawake wengine lakini pia ni fursa kwao katika mapambano" Wamesema.
Wameendelea kusema kwamba Kwa upande wa Zanzibar wanawake wengi wamekuwa na hofu ya kuchukua jukumu la kuisemea timu hasa za wanaume ingawa wakipewa nafasi wanafanya vizur.
Zainab Haroub Mohd ni afisa habari wa kwanza mwanamke katika michezo alikuwa aliisemea timu ya Kilimani city ilikuwa daraja la kwanza Kanda amesema uwamuzi wake uliibua hisia kubwa na kuwafanya wanawake wengine kutamani kuwa katika nafasi hiyo.
Zainab amesema uwepo wake kwenye timu ulileta tija kubwa kutokana na utofauti wa kiongozi huku mashabiki na wadau wakivutiwa nae.
Amebainisha kwamba mwanamke kuwa afisa habari wa timu za mpira wa miguu hasa za wanaume sio sababu ya kujivunjia heshima huku akisifu ushirikiano anaopatiwa kutoka Katika uongozi wa timu yake.
"Najivunia Sana kujitoa kwangu kuwa msemaji wa timu za michezo Zanzibar kumevutia wanawake wengi kuwa wanamichezo na kuona kumbe nao ni sehemu ya ushiriki wao" amesema Zainab
Kazija Thabit Vuai msemaji wa timu ya Ras Kazoni ya wanaume ilio daraja la kwanza Kanda ya unguja nae amebaisnisha fursa wanazozipata hasa za uvutiaji wa mashabiki katika timu.
Amesema ingawa timu hiyo Haina mashabiki wengi lakini uwepo wake ulionesha hamasa Kwa wachezaji wakiamini mwanamke ana ushawishi mkubwa wakati akitoa taarifa za timu husika.
"Yaani nikipata changamoto ya kutokuwepo kwangu uwanjani wachezaji wengi na viongozi wa timu hunipigia kunieleza bila uwepo wangu hakuna hamasa ya kutosha" amesema Kazija.
Kazija amebainisha kwamba ushiriki wa mwanamke katika michezo hakumpelekea mwanamke huyo kuvunjiwa heshima endapo atajiheshimu.
Kepteni wa timu ya Raskazoni Ramadhani Yussuf Issa maaruf OK amesema timu yao kuwa na msemaji mwanamke wanajivumia Sana huku wakisema wanatamani afisa wao huyo aendelee zaidi na zaidi
Ramadhani amesema wanamuangalia kazija kama mwanamke mwenye thamani kubwa kubwa Sana kwani amekuwa akifanya kazi Kwa kujitoa na kuhakikisha timu yake inakuwa Bora katika ligi.
"Afisa wetu Kwa kweli tinajitajidi kwenda nae vizuri na timu nyengine nazo pia hutuonea choyo kutokana na kumuona ana tumia nafasi yake vizur ya kuisemea timu yetu na imekuwa Kila mara ikisikika kupitia vyombo vya habari.
Mbali ya maafisa hao wa habari ama wasemaji wa timu za michezo wanawake kufurahia kazi wanayoifanya huku wakiona Ina tija Kwa namna Moja au nyengine lakini zipo timu ambazo zilikuwa na maafisa wanawake na baadae kuachia ngazi.
Kujiuzulu Kwa baadhi ya maafisa wa habari wanawake nao Kuna sababu kadhaa kama alivyoelezea bi Mwajuma Juma akise

Comments
Post a Comment