Skip to main content

KAMATI ZA MAZINGIRA ZA SHEHIA ZAPIGWA MSASA MABADILIKO YA TABIA YA NCHI.

Kamati za mazingira za Shehia kisiwani Pemba zimetakiwa kuielimisha jamii juu ya masuala ya haki yanayotokana na tabia nchi ili kurekebisha athari za mabadiliko hayo.


Hayo yameelezwa na Mkurugenzi mtendaji wa mwanvuli wa asasi za kiraiya Zanzibar Hassan Khamis Juma katika hafla ya kujengewa uwelewa wanakamati hao juu ya masuala ya haki yanayotokana na tabia nchi huko madungu chake chake Pemba. 


Amesema ikiwa dunia ipo katika janga la mabadiliko ya tabia nchi ni vyema wananchi kwa kushirikiana na kamati kuchanganua haki zao ili kuweza kupata mbinu za kupunguza madhara yanayojitokeza 


Kwa upande wake Mwalimu Khamis Mwalimu kutoka idara ya mazingira Pemba amesema ni vyema kamati za shehia kuitunza na kuilinda miundombinu iliyowekwa katika shehia zao ili kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi 

Naibu katibu wa mwenvuli wa asasi za kiraiya Pemba Alawi Bakari amesema maeneo mengi Tanzania yameshaharibika kutokana na mabadiliko ya labia nchi hivyo ni vyema kushirikiana kwa pamoja katika kuibua hoja, haki na wajibu kwa wanachi na kubuni miradi mbali mbali ili kuyarudisha baadhi ya maeneo yalioharibika na athari hizo .  


Wakizungumza kwa niaba ya washiriki hao mara baada ya kupatiwa mafùnzo ya haki na wajibu katika mabadiliko ya tabia nchi Muhammed Hassan Abdallah na Asha Hamad Ali wamesema kuwa mafunzo hayo watayafanyia kazi kwa vitendo kwa kuyafikisha katika shehia zao sambamba na kutumia namna bora za kuhifadhi mazingira kwa maendeo ya sasa na vizazi vijavyo.

Wamesema athari za mabadiliko ya tabia nchi hupelekea kukosa kufanya shughuli nyingi za kibinaadamu kutokana na maeneo mengi kisiwani pemba kuharibika ikiwa ni pamoja na kuharibika kwa maeneo ya kilimo, ukame , mafuriko , ongezeko la nyuzijoto kuzidi ambapo athari hizo huathiri jamii na nchi nzima kwa ujumla .

Wamesema licha ya jitihada mbali mbali ambazo wamekua wakichukua katika kukabiliana na athari hizo kama kupiga matuta kupanda miti lakini bado hazijazaa matunda ukilinganisha na athari zilizopo.



Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...