Skip to main content

"AMINA" KINARA WA UOGELEAJI BONANZA LA UTALII PEMBA

 NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA

"AMINA" KINARA WA UOGELEAJI BONANZA LA UTALII PEMBA

Na, Hassan Msellem, Pemba

Ni msichana wa miaka 15, Mkaazi wa Tumbe Mashariki anayesoma kidato cha Pili aliwashangaza wengi walioshiriki mashindo ya mchezo wa kuogelea yaliyofanyika huko Vuma Wimbi katika Pwani ya Msuka Kaskazini mwa Kisiwa Cha Pemba kwa kipawa chake cha kupiga mbizi na kuwashinda wapiga mbizi wenzake 14 na hatimae kuibuka mshindi wa pili.

Msichana huyo mwenye umri mdogo zaidi kuliko waogeleaji wote walioshiriki mchezo huo aliwaacha vinywa wazi watu wote waliokuwa wakishuhudia mtanange huo wapasua maji pasi na msaaada wowote wa waongoza mashindano hayo yaliyojumuisha urefu wa mita 20

Baada ya ushindi huo mwandishi wa Makala hii alipata nafasi ya kuzungumza na msichana huyo ilikufahamu siri ya kuibuka mshindi wa pili na kusema kufanya mazoezi kwa bidii ndio siri pekee iliyofanya awe na uwezo wa kupasua mawimbi zaidi kuliko wenzake ambao walionekana mapafu yao kukomaa zaidi na kwamba ndoto yake ni kuwa mpiga mbizi maarufu kisiwani Pemba na Zanzibar kwa ujumla

“kwakweli siri ya kuibuka mshindi ni kufanya mazoezi kwa bidii mimi na wenzangu hua tunafanya mazoezi kila siku jioni hasa siku za Jumamosi na Jumapili ambazo siendi Skuli” alisema

Amesema Kitita cha Shilingi laki saba kimempa shauku na hamasa ya kuendelea kufanya mazoezi kwa bidii zaidi na kujipanga na mashindano mengine mwakani na kila fursa ya mashindano inapotokea

“kwakweli fedha hizi zimenipa hamasa sana sasa ya kuamini kuwa mchezo wa kuogelea unalipa na sio mimi hata wenzangu pia kwahivyo tunaahidi kuzidisha bidii ya kufanya mazoezi ili kuendelea kufanya vizuri mwakani na kila inapotokea fursa ya mashindano” alisema msichana Amina

Amefafanua kuwa hakuweza kuamini kuwa ataweza kuibuka mshindi wa pili kwa kumshinda na mchezaji kutoka kikosi cha JKU Zanzibar ambaye hawalingani na kimo chake wala umri wake, ambaye aliibuka mshindi wa kwanza.

Kaije Seif Bakari ni mwalimu wa kikosi cha timu ya kuogelea ya Tumbe Mashariki ambayo msichana Amina anashiriki, amesema timu yao imekuwa ikifanya vizuri katika mashindo mengi na kuvutia watu wengi kutokana na umahiri wao wakuogelea na kuwepo kwa muogeleaji mdogo huyo mwenye kipaji cha ajabu

“kwakweli timu yetu ni mzuri sana kwasababu mashindano mengi tunayoshiriki tunashinda na watu wengi wanavutiwa na uwezo wetu wa kuogelea na kushiriki katika mashindano haya tunajisikia Faraja sana na tunaahidi kufanya vizuri zaidi kwa mashindano yajayo”

Bi. Kaije anasema wakati wanaanzisha klabu hiyo yenye jumla ya wanawake kumi wanaoogelea walipitia wakati mgumu kwani walikosa ushirikiano kutoka kwa jamii kwa kile wanachoamini kuwa wanawake hawapaswi kushiriki mchezo wa kuogelea kama wanaume

‘’Tumeanzisha timu hii lakini hatukuwa tunakubalika katika jamii tulionekana kama tumekosa kazi au wahuni tu lakini hatukurudi nyuma na tukaendelea kujipa moyo na kufanya mazoezi zaidi kwani tulikuwa na malengo yetu ikiwemo kujiokoa pindi inapotokea ajali ya kuzama maana sisi ni wavuvi lakini pia tuliamini ipo siku tutajipatia kipato kupitia kuogelea na leo tumeshuhudia tayari tumepata shilingi laki saba sio kidogo” Bi. Kaije

Kwa upande wake Maratibu wa Kamisheni ya Utalii Kisiwani Pemba Hamad Amini, amesema walipata taarifa ya kuwepo kwa kikundi cha akina mama hao kupitia mwandishi Blog ya Pemba Post na ripota wa Mawio Hassan Msellem ambaye aliwaibua akina mama hao ndipo nao walipoonda kuna haja ya kuwatambua na kuwaunga mkono kwa kuwapa fursa ya kushiriki katika mashindano hayo ya Bonanza la Utalii Pemba ili kuonesha uwezo walionao na kutoa motisha kwa wanawake wengine Kisiwani Pemba

‘’Ni miaka mingi sana tulikuwa tunafanya Bonanza hili lakini hatukuwahi kuwa na kikundi ya wanawake wanaogelea Pemba lakini kuwepo kwa kikundi hicho kwakweli ni faraja kubwa, taarifa za kuwepo kwa kikundi hichi nilizipata kutoka kwa mwandishi wa Habari Hassan Msellem ambaye alikuja ofisini kwetu na akanipa taarifa za kuwepo kwa akina mama hawa ndipo tukapanga kwenda kuwaona na kweli tulikutana nao na tukawaahidi kushiriki katika mashindano ya kuogelea katika Bonanza la Utalii Pemba linalofanyika Novemba kila mwaka” mratibu wa Kamisheni ya Utalii Pemba

Alisema licha ya kuwa ni mara ya kwanza kutoa fursa kwa wanawake kuonesha uwezo wao wa kuogelea lakini wameonesha uwezo nzuri katika mchezo huo na kuwavutia wengi na kuahidi kuendelea kutoa fursa kwa wasichana na wanawake mashindano hayo kila mwaka ili kujipatia fursa za maendeleo

Kuibuliwa kwa kikundi hicho cha akina wanawake wanaoshiriki vyema mchezo wa kuogelea kumetokana na uendeshwaji wa mradi wa usawa wa kijinsi kwenye michezo visiwani Zanzibar unaosimamiwa na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA) upande wa Zanzibar kwa lengo la kuhakikisha wasichana na wanawake wapata haki sawa ya kushiriki katika michezo

Khairat Haji Ali, kutoka Chama Cha Waandishi wa Habari wanawake Tanzania (TAMWA) Zanzibar amesema Tamwa imekuwa ikikutana na makundi mbali mbali ya wananchi na watendaji wa Serikali na taasisi za Kiraia katika kujenga uwelewa zaidi kwa jinsia ya kike kushirikishwa katika michezo ili kuimarisha ustawi wao

“Kwa muda mrefu tumeona wasichana na wanawake wanakosa fursa ya kushiriki na kushirikishwa katika masuala ya michezo, hivyo basi tumeona sasa ni muda muafaka wa kukaa pamoja jamii, Serikali na taasisi za kiraia ili kujenga uwelewa wa kuwashirikisha wanawake kwenye michezo ili kuimarisha ustawi wanawake katika Nyanja mbali mbali ikiwemo afya na maendeleo” alisema

MWISHO.

Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...