MAKALA NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA
Mwaka 1992 Tanzania ilianzisha mfumo wa vyama vingi vya siasa kutoka
mfumo wa chama kimoja cha siasa ambacho kilikuwa ni TANU kilichokuwa
kikiongozwa na Rais wa Kwanza wa Tanzania Mwalimu Julias K. Nyerere, na hapo
ndipo utitiri wa vyama vipya vya siasa ukaanza hadi kufikia vyama 21, ambapo
vitatu kati ya hivyo vikiwa vyama vikuu ambavyo ni Chama cha Mapinduzi-CCM Chama
cha Demokrasia na Maendeleo –CHADEMA na Chama cha Alliance for Change and
Transparency ACT Wazalendo.
Ukubwa wa chama na ushindi unatokana na wingi wa wafausi ambapo
wingi kwa kiasi kikubwa hupimwa katika mikutano ya Umma ya vyama ambapo
asilimia kubwa ya wafuasi huonekana kuwa ni wanawake kuliko wanaume hususan
vijana hilo hujidhihirisha kila kifikapo kipindi cha kampeni kwa ajili ya
Uchaguzi Mkuu.
Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi - CCM wanakadiriwa kufikia 8,432,980
Tanzania huku idadi ya Wanawake ikikadiriwa kufikia 6,124,735 asilimia 68% kati
ya wanachama wote, hii inadhihirisha kuwa idadi ya wanachama wanawake ni kubwa
kuliko wanaume
Katika za vyama mbalimbali vya siasa zinatoa haki sawa ya
uanachama na uongozi kwa jinsia zote kwa mazingatio ya hoja ya kutumiza umri wa
miaka 18 na kuwa mwanachama hai wa chama husika
Katiba ya ACT- WAZALENDO Ibara ya 8 (1) imesema “Uanachama wa ACT
Wazalendo utakuwa kwa raia wote wenye umri wa kupiga kura bila ya kubagua
jinsia,kabila,dini au hali yoyote, ibara hiyo inakwenda sambamba na Katiba ya Chama
Cha Mapinduzi Ibara ya 16 ambayo imeeleza kuwa “Kiongozi wa CCM ni kila
mwanachama mwenye dhamira yeyote katika CCM aliyechaguliwa au kuteuliwa kwa
mujibu wa Katiba.
“Maoni ya Wananchi”
Maoni ya wananchi yanalenga kuwa jinsia ya kike kwenye vyama vya
siasa hutumika tu kama daraja la wanachama na viongozi wanaume kufanikisha
malengo yao ya kushika nyadhifa mbalimbali ndani ya vyama na kulifanya kundi la
wanawake kama wapiga debe na mtaji wa kisiasa.Jambo hilo linadhihirishwa na Rajabu
Otham Ali,58 mkaazi wa Mgogoni Chakechake ambaye pia ni mwanachama wa Chama cha
Ukombozi wa Umma -CHAUMA licha ya sheria zilizoweka wazi kuhusu suala la jinsia
kwenye katiba za vyama vya siasa lakini suala hilo halijaweza kufikiwa kwa
vitendo katika vyama vingi vya siasa nchini“Mimi niko kwenye siasa tangu
mwaka 1980 na vyama vyote vina kanuni na katiba ambazo zinawaongoza ambazo
zimezungumza vizuri kuhusu suala la usawa kijinsia ndani ya vyama lakini bado
wanawake wanatumika tu kama mtaji wa viongozi katika vyama na ambaye anapata
fikra za kugombea nafasi fulani anakubwa na vitisho hata kama ni mwana chama
halali na ana uwezo” Amesema Rajab ambaye uzoefu wake unaonesha suala la
wanawake kupewa nafasi ni si sehemu ya uhalisia wa katiba na kanuni za vyama
vingi.
Wanawake ndio nguzo imara kwenye kampeni,kupiga kura na hata
kwenye ushawishi kama ambavyo Aisha Ali Massoud 42, mama wa watoto 8 mkaazi wa
Vitongoji Mchangani Wilaya ya Chakechake Mkoa wa Kusini Pemba ni mfuasi wa
Chama Civil United Front -CUF kwa muda miaka 20 amesema viongozi wengi wakubwa
wa vyama vya siasa nchini ni wanaume.“Nina miaka 20 ndani ya chama cha CUF na
najitoa kwa hali na mali maana hata nyumba yangu muda mwengine hutumika kama tawi
la chama lakini kujitoa kote huko sina nafasi yoyote na hata nikaitaka sidhani
kama nitaipata maana naangalia hao wanawake wenzangu wanavyofanyiwa” Amesema
Aisha ambaye kwake siasa ni maisha.
Hali ya kujiona mfuasi haiku kwa Aisha tu bali hali hii pia
inaonekana kwa Nachia Ali Jamal 45, Mkaazi wa Shehia ya Wambaa ambaye ni Mjumbe
wa Halmashauri Kuu Mkoa wa Kusini Pemba kupitia Chama Cha ACT WAZALENDO ameendelea
kutoa ushuhuda kuwa bado wanawake kwenye vyama vya siasa wana mchango mkubwa katika
maendeleo ya vyama hivyo lakini umuhimu katika kushika nafasi za uongozi ndani
ya chama ni jambo linalowekwa kisogoni.“Binafsi kinachonifanya niendelee kuwa
mwanachama hai na kushiriki shughuli mbalimbali za chama changu ni kwasababu
nimetoka nacho mbali sana tangu enzi za Mwalim Seif “ Nachia ameendelea kusema
kuwa.”Ukweli kwamba bado wanawake hususan tunaoishi vijiji hatupewi fursa za
kuwa viongozi kwenye chama na hizo nafasi tunazopewa ni zile tu ambazo wenyewe
wanajua kuwa hatuwezi kuwa sehemu ya nguvu ya maamuzi ndani ya chama jambo hili
ndilo linachangia wanawake kuwa madalali wa wanaume kwenye chaguzi”.Amemaliza
Nachia.
“Viongozi wa vyama vya Siasa “
Suala la wanawake kutumia kama daraja na wenye ushawishi kwenye
siasa linaweza linaonekana kuwa ni suala la kawaida ila viongozi wa kiasa
wanaliona hili tofauti,Ashloo Massoud Khamis Katibu Mwenezi, Siasa na Mafunzo
Wilaya ya Chake chake amesema elimu inayotolewa kwa vijana ndani ya CCM
imesaidia kwa kiasi kikubwa kuongeza usawa kijinsia kwasaabu wanawake wanapata
elimu ya kutambua haki na wajibu wao.”Kwenye chama ukiangalia utagundua wanawake
sasa wanashika nafasi mbalimbali za uongozi kuanzia ngazi za tatawi, wadi,
Jimbo, Wilaya hadi Mkoa” Ashloo ameendelea kusema kuwa “Kwanza nikiri kuwa ni
kweli wanawake ni wengi ndani ya chama kuliko wanaume na wanawake ndio tegemeo
la chama chetu na CCM ndio chama kinachojali na kuzingatia usawa wa Kijinsia
kuliko chama kingine chochote Tanzania,wanawake tunawapa nafasi katika chama
chetu” Amemaliza Ashloo.
Lakini licha ya kuwepo kwa dhana ya wanawake kutumika kama daraja
kwenye vyama vya siasa, vipo baadhi ya vyama ambavyo vimepiga hatua kuhusu
suala la usawa wa kijinsia katika nafasi za Uongozi, Katibu wa Chama Cha ACT WAZALENDO
Mkoa wa Chakechake kichama Saleh Nassor Juma amesema chama chao kinawathamini
wanawake na kuwapata nafasi. “Nataka nikuhakikishe kama kuna chama ambacho kinajali,
kuheshimu na kinazingatia usawa kijinsia ni chama chetu cha ACT Wazalendo kumbuka
kuwa Mwenyekiti wa ACT Wazalendo.
Ili kuondosha dhana ya utumwa kwa wanawake kwenye siasa wapo wadau
mbali mbali ambao hukosa usingizi katika kuhakikisha wanawake nao wanakuwa
viongozi katika Nyanja zote kuanzia ndani ya vyama vya siasa, taasisi binafsi na
taifa kwa ujumla
Dina Juma Makota ni Mratibu wa Jumuiya ya Utetezi wa Kijinsia na
Mazingira Pemba (PEGAO) amesema kupitia mradi wa Uhamasishaji Wanawake Katika
Uongozi (SWIL) wamefanikiwa kuwafikia wanawake 1289 ambao wamehamasika na kujiunga na vyama vya siasa na kuweza
kugombea nafasi mbali mbali ndani ya vyama vyao.
“Kupitia mradi wa SWIL tumeweza kuwafikia Wilaya zote za Pemba hususan Vijijini ambako ndiko kuna changamoto kuwa zinazowakabili wanawake kutokushiriki kwenye vyama vya siasa ambavyo ndio Daraja kuu la kuingia kwenye bahari ya Uongozi, hivyo basi ziara hizo zimeweza kuleta mabadiliko makubwa mno kwani tumeweza kuwafikia akina mama zaidi 1289 ambao wamepata muamko mkubwa na kuanza kujiunga katika jumuiya zao na vyama vya siasa na baadhi wameanza kugombea nafasi mbali mbali za uongozi ndani na nje ya vyama” amesema Mratibu wa Pegao



Comments
Post a Comment