Skip to main content

TAMWA ZNZ, ZAFELA, CYD na GIZ waipongeza Timu ya WARRIOR QUEEN kushiriki mechi ya Klabu Bingwa Afrika, Ethiopia.

Watekelezaji wa program ya Michezo kwa Maendeleo Zanzibar (S4D) wanawatakia kila la kheri timu ya Warrior Queens ya Saateni, Mkoa wa Mjini Magharibi, Unguja katika mashindano ya Klabu Bingwa Afrika kwa upande wa ukanda wa Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) yanayotarajiwa kufanyika nchini Ethiopia kuanzia tarehe 17 mpaka tarehe 31 Agosti mwaka huu 2024.


Timu ya Warrior Queens itaiwakilisha Zanzibar katika mashindano hayo na inatarajiwa kuondoka nchini kuelekea Ethiopia siku ya Alkhamis, tarehe 15 Agosti 2024. Tunaamini kuwa wataiwakilisha Zanzibar kwa fahari kubwa na kurudi nyumbani wakiwa washindi.


Pamoja na kuwapongeza wadau wote waliofanikisha timu hii kukamilisha mahitaji ya safari hiyo, TAMWA ZNZ inasisitiza umuhimu kwa wadau wote kuendeleza usawa wa kijinsia kwa kuzisaidia timu za wanawake na kukuza vipaji vyao ili kujenga jamii inayothamini na kuinua michango ya wanawake.


Bado ipo haja kwa wadau wote wa michezo, ikiwemo serikali, taasisi binafsi, na wadau wengine, kuongeza nguvu katika kuzisaidia timu za wanawake ili kuwawezesha wachezaji wetu wa kike kushiriki na kushinda mashindano mbalimbali, ndani na nje ya nchi.


Kufuzu kwa klabu ya WARRIOR QUEENS kwenye mashindano hayo kunatokana na klabu hiyo kuchukua ubingwa wa ligi kuu soka Zanzibar upande wa wanawake msimu wa 2023/2024 ambapo jumla ya timu 10 za wanawake zilishiriki.


Program ya S4D inatekelezwa kwa mashirikiano na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA ZNZ), Jumuiya ya Wanasheria Wanawake Zanzibar (ZAFELA), Kituo cha Mijadala kwa Vijana (CYD), kwa mashirikiano makubwa na Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Ujerumani - (GIZ) - chini ya Wizara ya Ushirikiano wa Kiuchumi na Maendeleo (BMZ).


Kila la kheri WARRIOR QUEENS!!!


Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...