Skip to main content

UKOSEFU WA VIWANJA RASMI VYA MICHEZO MASKULINI, WAKATISHA NDOTO ZA WANAFUNZI WAKIKE KUWA WANAMICHEZO.

 Michezo ni sehemu ya Maisha na moja kati shughuli zinazomfanya mwanadamu kufurahia Maisha kuwa na afya imara, kukuza ufahamu na hata ukakamavu wa mwili.

Kuna aina nyingi ya michezo ingawa baadhi ya michezo huendana na utamaduni na jamii fulani, kwa mfano mchezo wa Ngware ni mchezo maarufu kwa jamii ya Micheweni, mchezo wa YOGA katika jamii nyingi za Kichina, Nage, Kobole, Bao la Kete, Karata, Drafti huku mpira wa miguu ukiwa mchezo maarufu duniani kuliko mchezo mwengine wowote licha ya mchezo huo kuwa na idadi ndogo ya wanawake.

 

Maskulini ni sehemu muhimu ya kukuza michezo kwa wanafunzi hususan wanafunzi wakike kwani kutokana na utamaduni na mila nyingi za kiafrika watoto wakike hawapati muda wa kutosha kushiriki michezo wakiwa nyumbani kutokana na majukumu ya kazi na mitazamo mibaya kwa baadhi ya wanajamii walio wengi.

 

Miongoni mwa malengo ya mchakato wa kufanya mapitio, kufupisha na kuandika upyaya Mtaala wa Elimu ya Msingi Zanzibar mwaka 2008/2009 ili uendane na Sera ya Elimu Zanzibar ya mwaka 2006 ni:-

·      Kugundua vipaji vya kila mwanafunzi kuanzia umri mdogo ili kuvidumisha na kuviendeleza

 

Malengo ya kupitia mtaala wa elimu yam waka 2008\2009 ili kuendana na Sera ya Elimu yam waka 2006 ni kugundua vipaji vya kila mwanafunzi kuanzia umri mdogo ili kuvidumisha na kuviendeleza ingawa hakuna sehemu kwenye Mtaala huo hautaja kabisa suala la michezo kwa wanafunzi.

 

Ukosefu wa viwanja vya michezo kwa Skuli nyingi za msingi na sekondari kunachangia kwa kiasi kikubwa kufifia kwa vipaji vya michezo kwa wanafunzi wakike.

 

Kwa mujibu wa mwalimu wa Skuli ya Uweleni na Kocha wa timu ya mchezo wa mpira wa kikapu katika Skuli hiyo Mohammed Salim Khamis, alisema Skuli zote za Pemba ni Skuli ya Maziwa ya Ng’ombe Micheweni.

 

Miongoni mwa skuli hizo sizizo na viwanja vya michezo ni Skuli ya Sekondari Uweleni Mkoani, Msingi Kunguni Wambaa, Skuli ya msingi Nanguji, Skuli ya msingi mahuduthi Shehia ya Mkungu, Skuli ya msingi Minazini.

 

Maimuna Fatawi Khamis, ni mwanafunzi wa kidato cha tatu Skuli ya Sekondari Uweleni, alisema anapenda kucheza mpira wa kikapu (Baskateball) na anajihisi anakipaji cha hali cha kucheza mchezo huo lakini kukosekana kwa kiwanja cha kuchezea mchezo huo skulini kwao kumesababisha kushindwa kushiriki kucheza mchezo huo na kudumaza ndoto yake ya kufika mbali kupitia mchezo huo.

Salma Mohammed Bakar, mwanafunzi wa darasa la nne skuli ya msingi Mahuduthi, alisema kutokuwepo kwa kiwanja cha michezo katika Skuli yao kumezima ndoto za wanafunzi wengi wakike kushiriki katika michezo Pamoja na kufanya vizuri kwenye mashindo mbali mbali ya michezo ikiwemo Tamasha la Elimu Bila ya Malipo

 

Mkuu wa divisheni ya Michezo na Utamaduni kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Kisiwani Pemba Mzee Ali Abdalla, alikiri kuwepo kwa changamoto kwa baadhi ya Skuli kukosa Viwanja vya michezo hali inayosababisha wanafunzi hasa wakike kushindwa kushiriki katika michezo mbali mbali.

 

“Kwakweli suala la kukosekana kwa viwanja vya michezo kwa baadhi ya Skuli hilo ni tatizo kwasababu huwezi kushiriki mashindano mbali mbali ya michezo bila ya kuwa na viwanja vya michezo na ndio maana Serikali ikaitaka Wizara ya Elimu kumiliki ardhi ya kutosha ili inapojenga Skuli iwe na nafasi ya kuwepo kwa kiwanja cha michezo ili wanafunzi waweze kushiriki kwenye michezo” alisema

 

Mwalimu wa Skuli ya Sekondari Uweleni na Kocha wa timu ya mchezo wa mpira wa kikapu (Basketball) katika Skuli hiyo Mohammed Salim Khamis, alisema ukosefu wa kiwanja cha kufanyia mazoezi ya mpira wa Kikapu kwa wanafunzi wakike wa Skuli hiyo kunawasababishia wanafunzi hao usumbufu wa kuingia Skulini hapo mara mbili pamoja na kutumia wa Umoja ni nguvu katika kufanya mazoezi.

 

“Tuna jumla ya wanafunzi wakike ishirini na tatu ambao wanashiriki mchezo wa mpira wa Kikapu na wanafanya vizuri kwenye mashindano mbali mbali lakini changamoto inayotukabili ni hatuna kiwanja cha kufanyia mazoezi katika mazingira ya Skuli tunalazimika kutumia kiwanja cha Umoja ni Nguvu jambo ambalo baadhi ya wanafunzi wanaona shida sana Kwenda kule lakini kama tungekuwa na kiwanja chetu hapa hapa nadhani wanafunzi wangejitokeza kwa wingi zaidi” alisema

 

Aliongeza kwa kutoa ushauri kwa Wizara ya Elimu na mafunzo ya amali Zanzibar kuzingatia ujenzi wa viwanja vya michezo maskulini ili wanafunzi wapate fursa ya kushiriki michezo mbali mbali hali itakayosaidia kugundua na kukuza vipaji vyao.

Msaidizi mwalimu Mkuu wa Skuli ya Msingi Uweleni Khamis Mohammed Ussi, alisema miongoni mwa hatua walizozichukua katika kuhakikisha wanapata uwanja wa kufanyia michezo katika skuli hiyo ni kuongea na uongozi wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar ili kuona changamoto hiyo inatatuliwa.

 

Mkuu wa divisheni ya michezo na utamaduni Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Pemba Mzee Ali Abdalla, alisema mpango wa Wizara ya Elimu imeandaa mkakati wa kutambua maeneo yake ya ardhi nakupata hati miliki ili kuwa na maeneo ya kutosha katika kuweka miundombinu mbali mbali ikiwemo viwanja vya michezo.

 

Akizingumzia suala la baadhi ya Skuli ukosefu wa viwanja rasmi vya kufanyia michezo, alisema suala hilo ni changamoto kwa Skuli nyingi kwani kutokuwepo kwa viwanja rasmi kunachangia wanafunzi kutokushiriki katika michezo ipaswavyo.

 

“Tuelekee kule ambako Serikali inataka michezo ni fursa michezo, michezo ni somo kama masomo mengine na inatakiwa kuwa na maabara yake na maabara ya michezo ni viwanja sisi tunaamini na tunatambua umuhimu wa viwanja maskulini lakini maendeleo siku zote hayaji tu kama homa bali ni hatua kwa hatua” Mkuu wa Divisheni ya michezo na utamaduni Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Pemba



Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...