Skip to main content

'KAIJE' NGULI WA MCHEZO WA KUOGELEA.

 Makala Na, Hassan Msellem- Pemba


Kuogelea ni miongoni mwa michezo maarufu duniani na ni mchezo unaoshindaniwa kikanda, kitaifa na hata kidunia.


Lakini linapokuja suala kuogelea machoni mwa wengi tunawaona wanaume pekee ndio washiriki vinara wa mchezo huo, licha ya uchache wao wapo kwa Wanawake ambao wana uwezo na vipaji vya hali ya juu katika mchezo wa kuogelea.


Hamu na shauku ya Kaije ni kuwa kama Nguli wa mchezo wa kuogelea Dunia Bakulaben Patel mwanamke mwenye umri wa miaka 80 ni bingwa wa kuogolea kutoka Surat Magharibi mwa India, ambaye alianza kuogelea akiwa na umri wa miaka 58 na tangu wakati huo ameshinda karibu medali 500 katika mashindano ya kitaifa na kimataifa. Pamoja na hamu ya kuwafundisha wengine, anataka kuweka rekodi ya dunia.

 

Kwa mujibu wa ripoti ya shirikisho la mchezo wa kuogelea duniani (fina) zaidi ya nchi 80 hushiriki mashindano ya kuogelea huku mataifa kama vile finland, australia, japan, urusi na marekani yakiongoza katika mashindano hayo yanayojumuisha zaidi ya waogeleaji 200 huku wanawake wakiwa asilimia 30 tu hali inayoashiria idadi ndogo ya ushiriki wa wanawake katika mashindano hayo.


Kila mchezo hua na mitindo na mwembwembwe zake za kucheza na mchezo wa kuogelea nao una mitindo mbali mbali kama vile freestyle, backostroke, breaststroke, butterfly na side stroke.

 

Licha ya gwiji wa kuogelea kwa sasa kaije said bakari wapo wanawake ambao waliwahi kushika hatamu kupitia mchezo wa kuogelea kisiwani pemba akiwemo bi. Hija kombo kutoka kojani, rukia omar kutoka kisiwa cha kokota, time haji kutoka kijiji cha shamiani mwambe, mwanaidi kaasim kutoka kisiwa panza na maimuna juma kutoka kisiwa cha makoongwe.

 

Kaije Said Bakari ni mama aliyebarikiwa watoto saba akiwa na umri wa miaka 32, anaishi Kijiji cha Tumbe Mbuyuni Shehia ya Tumbe Mashariki Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba, ni nguli wa mchezo wa kuogelea sio kwa mji wa Tumbe tu bali hata Kisiwa cha Pemba kwa ujumla na mwalimu mchezo wa kuogelea kwa wanawake wenzake zaidi ya mia tatu Kisiwani Pemba.

Wa kwanza kushoto ni Bi. Kaije Said Bakari akiwa na wanawake wenzake ambao aliwafundisha kuogelea.

Kipaji cha Kaije cha kuwa mashuhuri wa kupiga mbizi kiliibuka kupitia mradi wa The Panje ambao uliotoa fursa ya mafunzo ya kuogelea kwa wanawake 20 wa Mji wa Tumbe, na Kajie kuibuka kinara kwenye mafunzo hayo na kupatiwa fursa ya mafunzo mengine ya kuogelea yaliyofahamika kwa jina la master training na hapo ndipo nyota ya Kaije ya kupiga mbizi ikaanza kung’aa.


Zaidi ya wanawake na wasichana 335 kutoka maeneo mbali mbali Kisiwani Pemba walipatiwa mafunzo ya kuogelea kutoka kwa Bi. Kaije na kuwa na uwezo mzuri wa kuogelea na kushiriki mashindano na mabonanza na kupata zawadi zilizowafanya kuwapa ari, moyo na hamasa ya kupenda mchezo wa kuogelea.


“Nimefanikiwa kutoa mafunzo ya kuogelea kwa wanawake na wasichana zaidi ya 300 maeneo mbali mbali kwa wanawake na wanafunzi wa skuli ikiwemo hapa petu Tumbe wanawake 100 wanafunzi 60, Fundo wanawake 30, Njau wanawake 20 na wanafunzi 120, Shumba Mjini 20, Tundauwa wanawake 15, Makangale wanawake 10, Kojani walimu 4 na wanafunzi 16, Chwale walimu 4 na wanafunzi 16” alisema


Mchezo wa kuogelea umemtoa Kaije katika dimbwi la ufukara na umasikini wa kiwango cha juu na kumfanya aishi Maisha ya kati na kati kwani umefanikiwa kujenga nyumba ya kisasa ya tofali badala ya kuishi kwenye hema na familia yake kama mkimbizi, kumpa mkate wake wa kila siku pamoja na kusomesha Watoto wake.

 

“Mchezo wa kuogelea umenitoa mbali sana nilikuwa fukara sana nilikuwa naishi kwenye banda ambalo ni saw ana hema kama mkimbizi mimi na familia yangu lakini nashukuru kupitia mchezo huu wa kuogelea nimefanikiwa kujenga nyumba ya kisasa, nina uwezo wakula mara tatu kwa siku pamoja kuwasomesha Watoto wangu licha ya kwamba nina mume lakini mimi ndio nakuwa mchango mkubwa zaidi katika familia yetu” Kaije Said Bakar kinara wa mchezo wa kuogelea Tumbe Pemba


Licha kipaji cha kuogelea alichobarikiwa Kaije alisema suala la kutokuwepo kwa mashindano na mabonanza ya kuogelea ya kila mwaka pampoja na kukosekana kwa klabu zinazosimamia mchezo wa kuogelea Kisiwani Pemba ni jambo linalomkosesha usingizi kila uchao kwani alisema kukosekana kwa mambo kunawafanya wanawake wenye vipaji vya kuogelea kutokupata hamasa ya kuendelea na mchezo huo, hivyo ameomba wadau wa michezo kuanzisha klabu maalumu itakayosimamia na kuanzisha mashindano ya kuogelea kwa wanawake.

 

Alisema “kwakweli waogeleaji wanawake wa Pemba tunakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo kukosekana kwa klabu maalumu zinazotusimamia na kukosekana kwa mashindano yatakayotuwezesha kuonesha vipaji vyetu ili tuweze kutambulika na kujipatia kipato”

 

Mize Hamad Sadiki na Fatma Hamad Ali ni miongoni mwa wanafunzi wa Bi. Kaije walisema mafunzo ya siku kumi tano yalitosha kumuwezesha kuwa na uwezo mzuri wa kuogelea na sasa wanaendelea na shughuli zao za upandaji wa mwani katika kina nirefu cha maji pamoja na kushiriki katika mashindano ya kuogelea na kuibuka washindi.

 

“Bi. Kaije kwetu tunamuona kama mwanamke wa mfano katika jamii yetu ya Tumbe mashariki kutokana na kujitoa kwake kutusaidia wanawake wenzake kutufundisha kuogelea hadi kufikia kiwango na sisi kuwafundisha wenzetu, kufanya shughuli zetu za upandaji wa mwani katika kina kirefu pamoja kushiriki mashindo yaliyoandaliwa na taasisi ya Milele Zanzibar Foundation na kupata zawadi sio jambo dogo kwetu” walisema 

 

Lakini licha uwezo na kipaji kizuri cha kupasua Bahari (kuogelea) alichojaaliwa Kaije, alisema anakabiliwa na ombwe la simanzi kwa kutokuwepo kwa mashindano maalum ya mchezo wa kuogelea ili kuonesha uwezo wake, kutambulika na kujipatia kipato, na kuwaomba wadau na taasisi husika za Serikali kuanzisha mashindano hayo alau kwa mwaka mara moja ili kukuza vipaji vya wanawake kwenye mchezo wa kuogelea Kisiwani Pemba.

Sio wanaume wengi katika jamii zetu wanaowaunga mkono wake zao wanapofanya vitu vya tofauti kama ilivyozoeleka lakini kwa upande wa bwana Mwinyi Ali Mussa ambaye ni mume Gwiji wa kuogelea Tumbe Mashariki Kaije Said Bakar, alisema kwake ni fahari kuona mke wake ni kiongozi kwa wanawake wenzake kwenye mchezo wa kuogelea kwani umemsaidia kwa kiasi kikubwa kujikwamua kimaisha pamoja na kutoa elimu ya kuogelea kwa wanawake wenzake na hata wanaume.

 

Alisema “Unajua kazi ni kazi za Bahari kwahivyo kujua kuogelea ni jambo muhimu sana sio kwa wanaume wala wanawake kwahivyo mke wangu kuwa na uwezo mzuri wa kuogelea kiasi ya kuwafundisha wanawake wenzake pamoja na kushiriki warsha mbali mbali kupitia mchezo wa kuogelea kwangu ni fahari na sio kwangu tu hata kwa jamii ya Tumbe kwa ujumla”

Kaije Said Bakari, akiwaonesha mitindo mbali mbali ya kuogelea wanawake wenzake wa Tumbe mashariki.

Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...