Skip to main content

Kamati ya kitaifa GEF yazipongeza MIF, TAMWA ZNZ kuwezesha Wanawake Kupata Haki za Kiuchumi.

 ZANZIBAR.


KAMATI ya Kitaifa ya Ushauri kuhusu utekelezaji wa Programu ya Kizazi Chenye Usawa wa kiuchumi (GEF) imezipongeza taasisi zinazowezesha upatikanaji wa haki za wanawake na watoto Zanzibar kwa jitihada zake za kukuza haki na usawa wa kiuchumi kwa makundi yote.


Pongezi hizo zimekuja kufuatia ziara ya kamati hiyo kutembelea taasisi za Mwanamke Initiatives Foundation (MIF), na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA ZNZ) iliyolenga kufuatilia utendaji wa taasisi hizo katika kuchangia ufikiaji wa kizazi chenye Usawa wa Kiuchumi.


Abeida Rashid Abdallah, mjumbe wa kamati hiyo ambaye pia ni Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Zanzibar alisema taasisi hizo zinafanya kazi kubwa ya kuisaidia serikali kufikia malengo yake ya kujenga kizazi chenye usawa wa kiuchumi kwa wanawake.


Alieleza, “tumefurahishwa sana na tumeona kazi kubwa inayofanywa na taasisi hizi katika kukuza haki na usawa wa kiuchumi kwa kuwajengea uwezo wanawake kuzifikia fursa mbalimbali za kiuchumi.”


Alishauri licha ya juhudi kubwa kuchukuliwa lakini bado wanawake wengi wanakabiliwa na tatizo la udhalilishaji wa kiuchumi na kuzitaka taasisi hizo kuendelea kuweka mkazo kwenye elimu ya kupinga udhalilishaji wa kiuchumi katika shughuli zao.


Nae Mohamed Jabir, mjumbe wa kamati hiyo alisema kamati imeridhishwa zaidi na namna ambavyo taasisi hizo hasa TAMWA ZNZ imesaidia kuwaondoa wakulima wa viungo kutoka kwenye kilimo cha mazoea hadi kilimo cha kibiashara.


“Wametuonesha ni namna gani TAMWA ZNZ wanachukua juhudi za serikali kusaidia kufikia malengo yake ya kizazi chenye usawa wa kiuchumi hasa kwa kuwawezesha wanawake kwenye kilimo biashara cha Viungo,” alieleza Jabir.


Kwa upande wake Mwajuma Magwiza, alizishauri taasisi hizo kubuni vipaumbele vipya vya kuwawezesha wanawake kuzifikia fursa zaidi za kiuchumi hasa kwenye sekta ya utalii.


Magwiza alisema, “nashauri hizi taasisi zinazotoa elimu ya ujasiriamali ziongeze kipengele cha kuwafundisha lugha wajasiriamali ili wawe na uwezo wa kuzungumza na watu mbalimbali bila kiwazo kwani tumeona licha ya kazi kubwa wanayofanya bado lugha ni changamoto kwa wanawake wajasiriamali wengi.” 


Katika hatua nyingine, Abdallah Duchi mmoja wa wajumbe GEF walioshiriki ziara hiyo alitaja miongoni mwa mapungufu yaliyobainika ni kutokuwepo kwa mazingira wezeshi kwa watu wenye ulemavu kuzifikia fursa zilizopo.


“Taasisi za kutoa huduma zinapaswa kuboresha mazingira yake ili kuwezesha ufikiaji wa makundi yote hasa watu wenye ulemavu kwasababu maeneo mengi tuliyofika hata ofisi zake bado hazijazingatia watu wenye mahitaji maalumu kufika bila kikwazo,” alieleza, Abdallah Duchi.


Mapema afisa uwezeshaji wanawake kiuchumi wa TAMWA ZNZ, Nairat Abdalla, aliieleza kamati hiyo kuwa mradi wa Viungo ulilenga kuwawezesha wanawake kukuza uchumi kupitia kilimo cha kisasa ambapo zaidi ya wanawake 2,000 wamefanikiwa kuzalisha mazao mbalimbali ikiwemo Vanilla.


Kamati hiyo katika ziara yake ya kufuatilia utekelezaji wa Programu ya Kizazi chenye Usawa Zanzibar imefanikiwa kutembelea taasisi za umma na binafisi, ikiwemo vikundi vya wanawake wajasiriamali wanaotekeleza afua za kizazi chenye Haki na Usawa wa Kiuchumi.

Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...