Skip to main content

Wanawake watakiwa kuelewa matumizi sahihi ya mitandao ili kuepuka ukatili wa kijinsia.

Habari Na, Thuwaiba Habib.



Mkurugenzi wa Zaina Foundation Zaituni Njovu amewataka waandishi wa habari kuwahamasisha wananchi namna bora ya matumizi ya mitandao ili kuepukana na ukatili wa kijinsia.


Ameyasema hayo katika mafunzo ya kuelimisha waandishi juu ya matumizi sahihi ya mitandao yalioandaliwa na zaina foundation huko hotel ya verde Mtoni Wilaya ya Magharib "A" Unguja alisema tumewapatia elimu waandishi wa habari juu ya matumizi sahihi ya mitandao ya kijamii lengo ni kuwaelimisha jamii ili kupunguza changamoto za ukatili ya kinjisia ambao unafanyika mitandaoni kwa njia tofauti.


"Alisema watu hutumia mitandao kufanya udhalilishaji kwa wanawake kuweza kutuma picha na maelezo ambazo zinaweza kuwa kweli au sio za kweli kwa lengo tu la kumchafua heshima mtu jambo ambalo husababisha msongo wa mawazo, kashfa, kunyanyapaliwa na jamii, na hata kujiuwa"


Aidha alisihi wanahabari kufahamisha jamii kuachana na tabia ya kueka picha za watoto wao mitandaoni kwani zinaweza kutumiwa vibaya na kuongezeka ukatili wa kijinsia.


Unapoeka picha ya mtoto mtandaoni ina kuwa ni hatari kwa sababu mtu yoyote anaweza kutumia sura hiyo kwa malengo tofauti yenye dhamira mbaya.


Alisema kwa mujibu wa utafiti walizofanya zinaonesha kuwa asilimia 51%ya watoto wameshadhalilishwa na 85% kufanyiwa unyanyasaji yote hayo yametokea baada wazazi kutuma picha za watoto wao kwenye mitandao. 


Pia aliwataka wanajamii kuacha kijirekodi picha chafu wakiwa katika mahusiano kwani baada ya uhusiano kuvunjika huzituma mitandaoni na kusababisha taharuki kwa jamii pamoja na familia.


Nae Afisa Program kutoka zaina foundation Dorina Mathayo aliwasisitiza waandishi kutumia password mazubuti ambayo itakuwa vigumu wengine kuielewa ili kujihakikishia usalama wa kazi zako.


"alisema password lazima ichanganye nambar, maneno na maneno maalumu ili watu wasijuwe kwa urahisi"


Aidha aliwataka waandishi kuepuka kubadilishana password pamoja na vifaa vya kazi ili kuweza kujilinda na kuweka usalama wa mambo yao hasa kwa kipindi hichi kinachoelekea uchaguzi.


Kitu cha kwanza unatakiwa uwe na password tofauti tofauti na iwe siri yako usibadilishane na hata watu wa karibu kwani kufanya hivyo kutasaidia watu kujilinda zaidi.


Pia aliwasihi kuweza kuwa makini na maongezi yanayoongea na ujumbe wanazotuma katika simu kwasababu mitandao ina kawaida ya kuhifadhi kumbukumbu za vitu inaweza kukupatia shida bila ya kutarajia.


Kwa upande wao waandishi wa habari mwanaisha bakari wa Zbc na kazija Mwinyi wa asalamu fm wamesema ni vizuri kupatiwa mafunzo hayo kwani wameweza kuelewa namna ya kujilinda na vipi unaweza kumkatili mtu kijinsia pamoja na kutobadilishana vifaa vya kazi ili kujihakikishia usalama 

 

Aidha waliwaomba zaina foundation licha ya kuwapa wao jukumu la kuelimisha jamii lakini na wao waweze kufanya mafunzo hayo kwenye maeneo mbali mbali hapa nchini ili kushirikiana kwa pamoja kusambza elimu hiyo.

Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...