Skip to main content

Vikundi vya Hisa Kuwasaidia Watu wenye ulemavu kujua haki zao.

KWA muda mrefu watu wenye ulemavu wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ukosefu wa elimu ya masuala ya kifedha kulingana na hali zao jambo ambalo linawafanya kushindwa kushughulikia vikwazo vyao katika jamii.



Katika kubakiliana na hilo, jumla ya vikundi 20 vya kuweka na kukopa vya watu wenye ulemavu vimeanzishwa kwa lengo la kujiendeleza kiuchumi na kuondokana na utegemezi kupitia mradi wa KIJALUBA iSAVE unaotekelezwa na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA ZNZ) kwa kushirikiana na Shirikisho la Jumuiya za Watu wenye Ulemavu Zanzibar na Chama cha Watu wenye ulemavu nchini Norway (NAD) katika Mkoa wa Kusini Unguja.


Vikundi hivyo vinavyoundwa na idadi ya wanachama 30 vikijumuisha wanawake na wanaume, wanachama wamewezeshwa kuanzisha na kujishughulisha katika miradi mbalimbali ya ujasiriamali ikiwemo utengenezaji wa sabuni na mafuta ya mwani bila kujali hali zao za ulemavu.


Baadhi ya vikundi vilivyoanzishwa ni pamoja na TUTAMBUWANE kilichopo Jambiani Mkadini, MWANZO MGUMU Michamvi Kae na kikundi cha NYOTA YA BAHATI kilichopo shehia ya Bwejuu.


Afisa Msaidizi wa mradi huo kutoka TAMWA ZNZ, Khairat Haji alisema mradi umetoa mafunzo mbalimbali kwa vikundi hivyo kwa lengo la kuwajengea uwezo watu wenye ulemavu kujua haki zao na kukabiliana na vikwazo mbalimbali katika jamii.


Alieleza wanufaika wamejengewa uwezo wa elimu ya kuweka na kukopa kwenye vikundi, umuhimu wa kuweka akiba, jinsi ya kutumia mikopo, elimu ya biashara na mbinu za kuendesha biashara zao kwa kulingana na hali zao.


"Tumetoa mafunzo mbalimbali kwa lengo la kuwajengea uwezo watu wenye ulemavu kujua haki zao, umuhimu wa kuweka na kukopa na jinsi ya kutumia mikopo na kufanya biashara na kuziendesha,"alieleza Khayrat Haji, Afisa Msaidizi wa Mradi wa Kijaluba.


“Lengo kuu la mradi limefanikiwa kwa kiasi kwa sababu haikuwa jambo rahisi kubadilisha mitazamo iliyojengeka katika jamii kwamba watu wenye ulemavu ni wa kupokea zaidi misaada badala ya kujishughulisha na kujiongezea kipato katika kujikwamuwa kiuchumi, Khayrat alisema.


Nae Afisa uwezeshaji kiuchumi kupitia mradi wa KIJALUBA iSAVE, Muhidin Ramadhan Muhidin alisema mradi unaendelea na zoezi la kuvisajili vikundi vyote vilivyopo chini ya mradi huo kupitia Idara ya Ushirika ili viweze kutambulika kisheria.


Alibainisha, “lengo la kuvisajili vikundi hivyo ni kupata fursa ya kufungua akaunti Benki na kuhifadhi fedha zao ili ziwe katika mazingira bora na salama,” alieleza Muhudin.


Ramadhani Haji, Mwenyekiti wa Kikundi cha Ushirika TUTAMBUWANE alieleza uwepo wa mradi umewasaidia watu wenye ulemavu kutatua baadhi ya changamoto zinazowakabili wao wenyewe ikiwa ni pamoja na kusomesha watoto na kuhudumia matibabu ya wagonjwa.


“Kupitia mfuko wa jamii, fedha zetu tunazoweka tumetatua matatizo mbalimbali. Tulipata maafa baadhi ya nyumba zetu kuingia maji na tukapata mkopo, pia wagonjwa waliolazwa walifaidika na mkopo huo kupitia jamaa zao waliojiunga kwenye vikundi," alieleza mwana kikundi huyo.


Kijaluba iSAVE Zanzibar ni mradi jumuishi unaotekelezwa Zanzibar na TAMWA Zanzibar kwa kushirikiana na SHIJUWAZA na Chama cha Watu wenye ulemavu nchini Norway (NAD) katika wilaya mbili za Chake chake kwa upande wa Pemba na Kusini kwa Unguja ukiwa na lengo la kuwezesha watu wenye ulemavu na kuwajengea uwezo kuhusu mitazamo chanya ya ushiriki katika shughuli za kujipatia kipato kupitia vikundi vya kuweka na kukopa.


MWISHO.

Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...