Skip to main content

TAMWA ZNZ, ZAFELA, CYD Zasherehekea Michezo kwa Maendeleo na Usawa wa Kijinsia Zanzibar.

JAMII imetakiwa kutilia mkazo ushiriki wa watoto katika michezo mbalimbali ili kuwajengea uwezo na kukuza ujuzi wa sitadi za maisha ktika kukabiliana na vikwazo mbalimbali ikiwemo udhalilishaji wa kijinsia.



Hayo yameelezwa na wadau katika kongamano la mashindano ya riadha kwa wanafunzi wa skuli mbalimbali za Zanzibar yaliyoandaliwa na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA ZNZ) kwa kushirikiana na Idara ya Michezo, Jumuiya ya Wanasheria Wanawake Zanzibar (ZAFELA), Taasisi ya Maendeleo ya Mashirikiano ya Ujerumani (GIZ) na Kituo cha Mijadala kwa Vijana (CYD) kwa lengo la kuhamasisha usawa wa kijinsia katika michezo.


Akizungumzia juhudi za kuimarisha usawa wa kijinsia na kuhamasisha michezo kwa maendeleo, Dkt. Mzuri Issa, Mkurugenzi wa TAMWA ZNZ, alisisitiza umuhimu wa kuendeleza na kuhamasisha michezo kwa wote ili kukuza ushiriki wa jinsi zote katika michezo.


"Tuwe mifano mizuri ya kuwa na heshima katika jamii, kwasababu sisi tuna nafasi ya kupata mawaidha sehemu mbalimbali ya stadi za maisha. Hivyo tuna kila sababu ya kuendeleza kuimarisha na kuhamasisha michezo kwa wote," alisema Dkt. Issa.

Kwa upande wake, Wanu Ali Makame, Meneja Idara ya Mitaala na Vifaa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, alibainisha kuwa katika kutilia mkazo umuhimu wa Michezo kwa Maendeleo, wizara imeweka somo maalum linaloelezea masuala ya Michezo.


Alieleza, “tuna somo maalum linaloelezea masuala ya Michezo Kwa Maendeleo. Tunaweza tukacheza na tukasoma kwa salama na amani bila kuathiri hulka na tabia ya mtu yeyote yule aliyetuzunguka.”


Hija Ramadhan kutoka Shirika la GIZ aliongeza kuwa jitihada za kutengeneza usawa wa kijinsia ni pamoja na kuhakikisha waadau wanashirikiana kuwalinda watoto na wanawake dhidi ya ukatili.


"Lengo hili tunaweza kulifikia kwa kutumia mbinu tofauti ikiwemo Michezo kwa Maendeleo," alisema Ramadhan.


Katika hafla hiyo hayo wanafunzi walipata fursa ya kushiriki mbio fupi na washindi kuzawadiwa zawadi mbalimbali ikiwemo medali na madaftari ya kusomea.


Mashindano hayo yamewaleta pamoja wadau mbalimbali ikiwemo wanafunzi kutoka skuli za Unguja, wanamichezo, walimu wa michezo, na wadau wa masuala ya usawa wa kijinsia yakiambatana na kaulimbiu “Wakati ni sasa! Wekeza katika elimu na michezo kwa watoto wote”, ikiwa ni hatua muhimu katika kuhakikisha michezo inatumika kama chombo cha kuleta maendeleo na usawa katika jamii.


Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...