Skip to main content

TAMWA ZNZ, Idara ya Michezo WEMA, ZAFELA, GIZ na CYD Kuandaa Mtoto wa Afrika Marathon.

 Ni katika kuadhimisha Siku ya Mtoto wa Afrika Zanzibar.



CHAMA cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA ZNZ) kwa kushirikiana na Idara ya Michezo, Jumuiya ya Wanasheria Wanawake Zanzibar (ZAFELA), Taasisi ya Maendeleo ya Mashirikiano ya Ujerumani (GIZ) na Kituo cha Mijadala kwa Vijana (CYD), inatarajia kuadhimisha ya siku ya kimataifa ya Mtoto wa Afrika tarehe 29 Juni 2024 kwa kuandaa mashindano ya riadha kwa wanafunzi wa skuli mbalimbali za Zanzibar.


Maadhimisho hayo yatawahusisha jumla ya washiriki 150 ambapo kati ya hao watakaoshiriki mashindano ni wanafunzi 75 kutoka katika skuli za Unguja ambazo zimeshajiandaa kushiriki mashindano hayo.


Tukio hili muhimu ambalo linalenga kuhamasisha usawa wa kijinsia katika michezo litawaleta pamoja wadau kutoka taasisi za kierikali na zisizokuwa za kiserikali ikiwemo wanafunzi kutoka skuli mbalimbali za Unguja, wanamichezo, walimu wa michezo, na wadau wote wa masuala ya usawa wa kijinsia.


Maadhimisho haya yanatoa fursa kwa wasichana kuonesha vipaji vyao na uwezo wao wa kushiriki katika michezo mbalimbali, pamoja na kujadili changamoto na vikwazo vinavyowazuia kushiriki katika michezo na kuhimiza uanzishwaji wa madawati ya jinsia katika taasisi za michezo.


Mashindano haya ya riadha yataanza saa 12 na nusu asubuhi, yakianzia maeneo ya Forodhani na yataishia katika viwanja vya Mnazi Mmoja Zanzibar yakishirikisha wanafunzi wa jinsia zote  kutoka skuli mbalimbali za Unguja.


Kaulimbiu ya wadau katika maadhimisho ya mwaka huu ni Wakati ni sasa! Wekeza katika elimu na michezo kwa watoto wote”. Tukio hili linatarajiwa kuleta mwamko na kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa kuwapa nafasi sawa watoto wote kushiriki katika michezo, bila kujali jinsia zao. Mashindano hayo yatatoa washindi watatu zaidi wanawake na watatu wanaume na kutambuliwa rasmi.  


Tunaamini kuwa michezo ni nyenzo muhimu ya kuleta usawa wa kijinsia na kuwawezesha watoto wa kike na wa kiume kujifunza stadi za maisha, kujenga ujasiri, na kushirikiana kwa amani na kuheshimiana.


Tunawaalika wanahabari, wazazi, walezi, na wananchi wote kujitokeza kwa wingi kushuhudia na kuunga mkono tukio hili la kihistoria katika kukuza usawa wa kijinsia na kuwawezesha watoto wote kufikia ndoto zao katika Nyanja mbali mbali bila vizuizi vyovyote.


Imetolewa na Idara ya mawasiliano,

TAMWA ZNZ.

Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...