Skip to main content

Walimu waiomba wizara kutenga bajeti kuwezesha michezo maskulini.

Na, Hassan Msellem, Pemba 


Walimu wa Skuli ya msingi Michakaini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, wameiomba Wizara ya elimu na mafunzo ya amali Zanzibar kuandaa bajeti maalumu kwenda maskulini Ili kusaidia Klabu za Michezo.


Wakizungumza na mwandishi wa Habari hizi, Mwalimu wa somo la michezo Habiba Juma Jafar na Mwalimu Subira Abdalla Saleh, walisema kutokana changamoto za ukosefu wa fedha na mazingira rafiki ya kufanyia michezo inawalazimu katika mashindano ya elimu ya malipo pekee jambo linalochangia kurudisha nyuma harakati za michezo skulini hapo.


"Hapa Skuli tunaprogramu za michezo mbali mbali ikiwemo michezo ya mpira wa miguu kwa wanaume, mpira wa wavu, kuimba utenzi, ngonjera, mbio za magunia nakadhalika lakini ukiangalia tunashindwa kuendeleza michezo hii kwasababu tunakosa bajeti za mazingira rafiki ya kuendeleza maana hapa Skuli hakuna mazingira ya Uwanja ya kushiriki michezo yote hiyo"

Alieleza faida ya kushiriki katika mchezo kwa wanafunzi hususan kwa wasichana mwalimu wa somo la afya na michezo katika Skuli hiyo Fatma Haji Ali, alisema michezo Ina faida nyingi kiafya ikiwemo kuepukana na maradhi mbali mbali na udumavu wa akili pamoja na kuongeza ufahamu kwa wanafunzi.

"Kwakweli Kuna faida nyingi sana kwa wanafunzi kushiriki katika Michezo miongoni mwa faida hizo zipo za kiafya lakini pia za kimaisha kwa upande wa afya mwanafunzi anayeshiriki michezo anakuwa na afya imara kwani anapata ushangamfu wa kimwili, kiakili, ufahamu pia unaongezeka lakini inaweza kumpa ajira pindi akimaliza masomo" 

Nasra Juma Rajab ni mwanafunzi wa darasa la tano anayeshiriki michezo wa mpira wa kikapu na nage alisema michezo imewezesha kuwa na afya mzuri, uchangamfu pamoja na kuongeza ufahamu katika masomo.

"Napenda sana michezo kwasababu napata kuchangamka, afya mzuri lakini hata ufahamu wangu unakuwa mzuri, naomba uongozi wa Skuli uendelee kuimarisha michezo ili tuzidi kufika mbali kimichezo hususan michezo tunayoweza kushiriki wanafunzi wakike ikiwemo mchezo wa netball, kuimba, kusoma utenzi na nage" 


Arkam Abdi Hamza, ni mwanafunzi wa darasa na mchezi nguli wa mpira wa miguu katika Skuli ya msingi Michakaini, amewaomba wanafunzi wenzake kushiriki katika michezo inayochezwa skulini hapo Ili waweze kunufaika na faida za michezo ikiwemo kuwa na afya imara ya kimwili na kiakili pamoja kupata zawadi mbali mbali ikiwemo madaftari, viatu, sare pamoja na Fedha.


"Nawaomba wanafunzi wenzangu wapende michezo kama ninavyopenda Mimi kwani kupitia michezo nimepata faida nyingi nimewahi kupewa viatu, madaftari, mkoba na pesa kupitia mashindano ya elimu bila ya malipo yaliyomalizika hivi karibuni"


Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...