Na Nihifadhi Abdulla, Zanzibar.
WAANDISHI wa habari wametakiwa kuwashajihisha wanawake kuingia kwenye michezo huku wakizigatia maadili na silka za Kizanzibari kwa kujiheshimu na kulinda hadhi yao
Yamesemwa hayo na Mkurugenzi wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake TAMWA Zanzibar Dk Mzuri Issa wakati akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari juu ya kushajihisha wanawake kushiriki kwenye michezo yaliyofanyika katika Ofisi za TAMWA Mkoa kusini Unguja.
Amesema waandishi wananafasi kubwa ya kusikilizwa kwenye jamii hivyo ni vyema kwenda kuyatendea kazi wanayoelekezwa ili lengo liweze kufikiwa
Kwa upande wake mkufunzi wa mafunzo hayo ambae pia ni Mjumbe wa Bodi ya TAMWA Bi Hawra Shamte amesema kuna mitazamo mbalimbali katika jamii zinamkwamisha mwanamke kushiriki michezo hivyo anaimani waandishi wakitumia kalamu zao vizuri kuelimisha jamii dhana ya michezo kwa maendeleo itapatikana
Amesema uwepo wa sera ya Michezo ya mwaka 2018 ni kielelezo kuwa Serikali inazingatia sekta hiyo na inaendelea kuweka mikakati katika kushughulikia tofauti za kijinsia kwa maendeleo ya taifa
Nae mtaalam wa michezo kutoka Shirika la maendeleo la Ujerumani (GIZ) Makame Amir Mgeni Amesema ni wakati sasa jamii kuelimishwa kumruhusu mwanamke kushiriki kwenye Michezo kwani inafaida kiafya, mwili na akili.
Mradi wa Michezo kwa maendeleo unaolenga kukuza usawa wa kijinsia katika sekta hiyo unatekelezwa na TAMWA ZANZIBAR, Kwa kushirikiana na Shirika la GIZ.


Comments
Post a Comment